Samatta kuwanoa vijana nchini, asaini mkataba

Muktasari:

  • Akizungumzia mkataba huo, Samatta alisema una lenga kuhamasisha vijana ili kuendeleza soka la Tanzania.

Nahodha wa Taifa Stars na mshambuliaji wa KRC Genk ya Ubeligiji, Mbwana Samatta ameingia mkataba maalumu na Benki ya DTB na pia ataendesha kliniki ya soka kwa mamia ya vijana zoezi lililofanyika kwenye viwanja vya Kituo cha Michezo cha Jakaya Kikwete, Kidongo Chekundu Dar es Salaam.

Akizungumzia mkataba huo, Samatta alisema una lenga kuhamasisha vijana ili kuendeleza soka la Tanzania.

"Nitakuwa balozi wa DTB (Diamond Trust Bank), nikifanya kazi mbalimbali za kijamii na masuala ya kimichezo," alisema Samatta muda mfupi baada ya kumaliza kutoa mafunzo ya soka jana.