Usajili Yanga ndiyo kwanza kumekucha
Muktasari:
- Katibu mkuu wa klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa alisema wanaendelea kusajili kwa kufuata orodha ya mahitaji ya kocha George Lwandamina .
Baada ya Yanga kumnasa Ibrahim Ajib, klabu hiyo imeibuka na kusema mambo bado na imewataka wanachama wake kuendelea kusubiri wachezaji wengine itakaowasajili.
Katibu mkuu wa klabu hiyo, Charles Boniface Mkwasa alisema wanaendelea kusajili kwa kufuata orodha ya mahitaji ya kocha George Lwandamina .
“Usajili bado unaendelea, ila hatuwezi kuweka majina wazi ya wachezaji gani tunaowahitaji, kuhusu Abdallah Haji Shaibu ‘Ninja’ mwalimu alimuona kwenye mashindano ya Mapinduzi, ndiyo maana tumemsajili.
“Kulikuwa na maswali mengi kuhusu usajili wake, tunajua nini tunafanya tena niweke wazi kuwa usajili wetu unaenda kwa mpangilio maalum,” alisema Mkwasa.