Juisi ya stafeli hutibu mfumo wa fahamu

Muktasari:

  • Stafeli hustawi katika ukanda wa kitropiki na tunda hilo hufanana kidogo na tunda la topetope ambalo nalo lina kiasi kikubwa cha sukari ya asili.

Hivi ulishawahi kujiuliza matunda yapi yawe rafiki kwako na familia yako? Jibu usinipe ila bado hujachelewa naomba uanze sasa kwa kula Stafeli kwani ni tunda lenye faida nyingi mwilini kama yalivyomatunda mengine. Asilimia 12 ya tunda hilo lina sukari ya asili ambayo ni salama kwa mlaji na kwamba ni chanzo kikuu cha Vitamini C, madini ya chuma na Niacin Riboflavin.

Stafeli hustawi katika ukanda wa kitropiki na tunda hilo hufanana kidogo na tunda la topetope ambalo nalo lina kiasi kikubwa cha sukari ya asili.

Tunda hili hutibu matatizo ya mfumo wa fahamu, shinikizo la damu, msongo wa mawazo na saratani.

Utafiti uliowahi kufanyika unaonyesha juisi yake pia hutibu saratani kwa haraka, kwa sababu inanguvu mara 10,000 zaidi ya tiba ya mionzi katika kuzuia seli za saratani.

Hata hivyo, wagonjwa wa saratani wanapokuwa katika tiba ya hospitalini wanashauriwa kula tunda hilo kwa ajili ya kupunguza makali ya dawa za saratani anazotumia pamoja na maumivu.

Stafeli linakirutubisho aina ya Annona Muricata kinachoweza kukabiliana na maradhi ya saratani katika mwili wa binadamu.

Mbali ya kuwa ni chanzo kikubwa cha vitamini, tunda hilo hutibu maumivu ya nyama za mgongo, hurekebisha usawa wa kiasi cha damu na sukari mwilini na huongeza kinga ya mwili.

Faida nyingine hudhibiti ukuaji wa bakteria, virusi, vijidudu nyemelezi na hutibu majipu na uvimbe, huongeza stamina ya mwili na kurahisisha kupona haraka na hufukuza chawa.

Majani yake hutumika kama chai.

Majani hayo hutibu pia kuharisha damu, mafua na husaidia mfumo wa umeng’enyaji wa chakula.

yanatumika pia kutibu maumivu ya mishipa. Mtumiaji unatakiwa kuyasaga mpaka yalainike kisha yapashe jikoni na kupaka katika eneo la mshipa wenye maumivu.

(Hadija Jumanne)