Maajabu ya bangili ya shaba na tiba ya ndani kwa mwili wa binadamu

Muktasari:

  • Kifupi, kama unadhani kuwa tiba na kinga za maradhi ni vidonge na sindano pekee, basi umepotea, ulizia tena upya maana binadamu ameumbwa kwa namna ya ajabu sana na anapopatwa na maradhi basi huhitaji tiba za aina nyingi sana kama vile tiba ya maji (Hydrotherapy) tiba ya kupakwa matope yaani (Mudtherapy) na nyinginezo nyingi tu ikiwemo hii ya kuvaa copper bracelet. Vazi hili linamfanya binadamu kujitibu maradhi mengi sana.

Binadamu ameumbwa kwa namna ya ajabu, anapopatwa na maradhi huhitaji tiba za aina nyingi ikiwamo ya maji (Hydrotherapy), ya kupakwa matope (Mudtherapy) na nyinginezo nyingi ikiwamo ya kuvaa bangili ya shaba (copper bracelet).

Bangili hii inamfanya binadamu kujitibu maradhi mengi. Lakini leo nitayadadavua maradhi matano.

Historia yake

Uvaaji wa bangili ya shaba uligunduliwa ni tiba kwa mvaaji toka enzi za kustaarabika kwa watu wa Misri ambao wanasadikika ndiyo waliosambaza ustaarabu huo duniani kote.

Kwa muda mrefu imani hiyo imeendelea kutumika duniani na mpaka sasa sayansi bado inakiri kuwa bangili hiyo ina tiba zisizoonekana zenye uwezo wa kuponya taratibu maumivu ya misuli na viungo kwa ujumla. Ukiacha hilo, bangili hiyo huimarisha kinga ya mwili na kuongeza kiasi cha nguvu za mwili wa mvaaji kimaajabu.

Kukakamaa na maumivu ya viungo

Sote tumewaona wanawake wa kimasai huvaa bangili hizo na ni aghalabu kuwakuta wakiugua maumivu ya viungo. Ni wanawake imara wanaomudu kuchunga makundi ya ng’ombe wakitembea kwa muda mrefu. Kwa taarifa, gari liitwalo Land Cruiser VX lilipewa jina la ‘Shangingi’ ikimaanishwa ni mwanamke wa kimasai yaani ‘Sangiki’ kutokana na uimara, umadhubuti na uzuri wa gari hilo.

Kinadharia, imebainika kuwa madini anayopata mvaaji wa bracelet hufyonzwa vizuri zaidi ya madini ayapatayo mtu anayemeza vidonge vya lishe kwa kuwa huenda moja kwa moja katika mfumo wa damu bila kupitia katika ini. Sote tumeshuhudia wavaaji wa copper bracelets ni wenye nguvu, afya njema, wasio na woga na hujiamini sana. Hii ndio nguvu isiyoonekana ya copper bracelet.

Kuimarisha afya ya mishipa na moyo

Binadamu anapopungukiwa na madini ya shaba na mazao yake huwa hatarini kuugua magonjwa yanaohusisha moyo na mishipa yitwao ‘Aortic aneurysms’ Sio siri, tafiti nyingi duniani zimeunyesha kuwa mtu akipungukiwa na madini ya shaba huvuruga mtiririko wa damu mwilini na hata kupandisha kiwango cha kolestro katika damu na kusababisha uharibifu kwenye moyo na njia za damu mwilini. Madini ya shaba mwilini hudhibiti na kuratibu fibers, collagen, na elastin hivyo kumlinda mtu na shambulizi dhidi ya Aortic aneurysms. Hapo utagundua kuwa kuvaa copper bracelet ni rahisi lakini kunaweza kukukinga na maradhi makubwa sana hasa kupooza ambayo ni magonjwa yanaotuua kwa kasi sana siku hizi. Ni aghalabu sana kumkuta mtu anayevaa copper bracelet kuugua maradhi ya moyo.

Kuimarisha mfumo wa kinga

Shaba ikivaliwa mwilini mwa binadamu hufyonzwa taratibu na kwa kiwango sahihi kabisa ambacho hungia katika mfumo wa damu, hivyo kumfanya mvaaji awe na uwiano sawa kati ya mwili na saikolojia yake. Hii hutokea kwa kuwa shaba huharakisha utoaji wa sumu na taka mwili na kuufanya mwili wa binadamu uzalishe ‘enzymes’ zinazotengeneza ‘Hemoglobin’ nyingi na kwa haraka inavyotakiwa. Hii ndio sababu ulipokutana na mtu aliyevaa copper bracelet ulimuona ni mwenye furaha na anayejiamini kwa lolote mbele yake. Jiulize, kwanini Ukihitaji kuunganishiwa umeme ni lazima ufunge nondo ya shaba na uichimbie ardhini ndipo utaunganishiwa huduma hiyo? Ni kwamba itasaidia kupambana na nguvu za umeme za ziada na kama ukikatika kila kitu cha umeme ndani ya nyumba kikiguswa huwa na shoti ya umeme.

Hupunguza uzee (Anti-aging)

Shaba ikivaliwa hutoa aina ya viuasumu viitwavyo ‘anti-oxidant properties’ ambavyo huzuia taka na sumu za mwili kuharibu seli za mwili na kuzilinda pia.

Kwa kudhibiti na kuratibu uzito wa collagen na elastic pamoja na fiber, shaba huweza kuzuia mwili wa mvaaji kuzeeka haraka na hivyo tumewashuhudia wavaaji wakionekana bado vijana wakati umri wao umeenda.

Hizi ni baadhi tu ya faida za kuvaa copper bracelet iwe kwa wanaume au hata wanawake.

Kwa kawaida huwezi kuona utendaji kazi wake kama miujiza ya kulala na kuamka ukakuta mabadiliko bali huchukua miezi miwili hadi mitatu mvaaji kugundua kuwa mwili wake umepata mabadiliko kiafya na toka hapo ataendelea kufaidi hasa kutougua mara kwa mara.

Upatikanaji:

Upatikanaji wa Copper Bracelets si mgumu na bei zake siyo ghali pia.

Wamasai hutembeza barabarani wakiziuza katika maeneo mengi ya mijini na hasa Jijini Dar es Salaam.

Ukiacha hao, unaweza ukaingia kwa sonara akakutengenezea na haitakuwa ghali kama dhahabu kwa kuwa madini ya shaba bei yake ni rahisi.

Ningependa kusikia toka kwenu wasomaji kutokana na sababu hizi tano tu tulizoziona leo hapa na kugundua kuwa vazi hili ni tiba, bado tu hatuna sababu ya kuidhinisha Copper Bracelet kuwa vazi letu la taifa? Tuonane wiki ijayo.

Dk John Haule (Dietition)

+255 768 215 956

Facebook/john.haule4