Diamond kuongoza mashambulizi

Muktasari:

  • Diamond anatamba na nyimbo zake mpya ambazo ni I Miss You, Fire na Eneka alioutoa kimya kimya mapema wiki hii.
  • Wasanii wakubwa wanaotamba ulimwenguni watalipamba jukwaa katika Tamasha hilo litakalofanyika katika Viwanja vya Leaders, Julai 22 mwaka huu.

Ikiwa imebaki wiki moja kuelekea ile sikukuu ya aina yake, Kampeni ya Castle Lite Unlocks, Diamond Platnumz kwa mara ya kwanza atatumbuiza nyimbo zake tatu alizoziachia hivi karibuni.

Diamond anatamba na nyimbo zake mpya ambazo ni I Miss You, Fire na Eneka alioutoa kimya kimya mapema wiki hii.

Wasanii wakubwa wanaotamba ulimwenguni watalipamba jukwaa katika Tamasha hilo litakalofanyika katika Viwanja vya Leaders, Julai 22 mwaka huu.

Wasanii hao ni Future kutoka Marekani na Casper Nyovest wa Afrika Kusini. Wengine kutoka hapa nyumbani ni Vanessa Mdee, kundi la Weusi na Navy Kenzo. Meneja uhusiano wa wateja wa kampuni ya Tanzania Brewaries Limited (TBL) kwa Afrika Mashariki, George kavishe anasema ili mashabiki wafurahie siku hiyo waanze kununua tiketi mapema au kushiriki katika bahati nasibu zinazoendelea.

“Kwa mara nyingine tena tunawakumbusha wapenzi wa muziki, hasa walioko katika Jiji la Dar es salaam na maeneo ya karibu kujiandikisha kwa wingi kwani tukio hilo la aina yake linakaribia” alisema Kavishe.

Akitangaza washirika wa tamasha hilo, Kavishe alipongeza mchango wao akisema kwamba wametekeleza jukumu kubwa katika mafanikio ambayo kampeni hiyo imefikia mpaka sasa.

Alitaja wadhamini hao kuwa ni Tigo Tanzania, Clouds FM, CFAO Motors, Marlboro na Serena Hotel Dar es Salaam.

“Tunawashukuru washirika wetu kwa kukamilisha juhudi zetu katika kuelekea kwenye tamasha la nne la muziki ambalo nina hakika kuwa litakuwa ni chanzo cha mabadiliko makubwa katika tasnia ya muziki wa ndani”, amesema Kavishe.

Jinsi ya kununua tiketi

Kavishe amewashauri wapenzi wa muziki kununua tiketi kupitia Tigo Pesa kwa namba namba 0674 444 444 na kwenda kuzichukua katika Tigo Shop yoyote katika Jiji la Dar es salaam.

Amesema watumiaji wa mitandao mingine ya simu wanaweza kununua tiketi kwa kuchagua “mitandao mingine” katika menyu ya simu pesa zao na kununua kwa kupitia namba hiyo hiyo ya malipo.

“Manunuzi ya tiketi yanaenda kwa kasi sana kwa hiyo ninawasisitiza watu wote kununua tiketi zao sasa kwa sababu hili ni tukio ambalo haupaswi kukosa.

Alisema mashabiki wategemee burudani ambayo haijawahi kutokea hapa Tanzania: “Tumeandaa tamasha hili katika viwango vya hali ya juu, . Usalama na mpangilio utakuwa wa kipekee,” anasema.

a Kavishe.

“Gharama ya tiketi ni Tshs 20,000 lakini wateja watakaolipa kwa Tigo Pesa watafurahia punguzo la bei la Sh5,000,” alisema Kavishe, huku akiongeza kwamba kwamba wateja wataweza kujipatia tiketi zao kutoka katika maduka ya huduma kwa wateja ya Tigo (Tigo shop) yaliyopo karibu nao.

Alizitaja sehemu ambalko wanaweza kwenda kuchukua tiketi zao kuwa ni pamoja na: Mlimani City-Mlimani City Mall, Makumbusho (mkabala), Palm Beach Residence-Ocean Road, Nkurumah- Nyerere Road- Gold Star, Buguruni-Rozana, Quality Center-Quality Center Mall, JM Wall- Hotel Harbor View, Masaki- Haille Selassie Road, Kariakoo-Msimabazi/Pemba Street, Manzese Darajani, Kigamboni-Ferry, Tegeta-Kibo Complex na Mbagala- Oil Com Gas Station.