Gosby : Rapa anayeamini katika elimu

Muktasari:

  • Staili ya muziki aina ya trap ambayo imeibuka miaka ya karibuni imeonekana kushika kasi kwa kiasi kikubwa huku Bongo nao wasanii mbalimbali wa Rap wakiifanya japo imekuwa na mapokeo hafifu.

Wimbo Monifere alioimba akimshirikisha Vanessa Mdee katika kiitikio ulimtambulisha katika ramani ya Bongo Fleva lakini upekee wake ni aina ya muziki anaoimba.

Staili ya muziki aina ya trap ambayo imeibuka miaka ya karibuni imeonekana kushika kasi kwa kiasi kikubwa huku Bongo nao wasanii mbalimbali wa Rap wakiifanya japo imekuwa na mapokeo hafifu.

Moja ya wasanii wanaosifika kwa kufanya trap kali ni Gosby.

Alikoanzia

“Nilianza Muziki tangu nikiwa shule tena nilikuwa naimba kipindi hicho, lakini baadaye nilianza kurap na watu wakawa wanapenda zaidi sababu kwa kipindi hicho nilikuwa nafanya sana remix za wasanii wengine kwenye miaka ya 2007,”

“Wimbo wangu wa kwanza kupata mafanikio ulikuwa ni Everyday ambao niliutoa mwaka 2012 ulipendwa sana na baadaye zikaanza kuja na nyingine ambazo zilifanya poa pia kama BMS,” aliongeza.

Mgogoro na B Hitz

Kipindi fulani Gosby alikuwa akifanya kazi zake katika studio za B Hitz ambazo zinamilikiwa Hammy B chini ya mtayarishaji Pancho Latino.

Akizungumza uhusiano wao anasema kuwa wapo freshi “Mimi na B Hitz tuko freshi tofauti na watu wanavyofikiria na hakuna shida yoyote ile yale matatizo yaliyokuwepo mwanzo yalishaisha na maisha yanaendelea,” anafafanua

Mixtape yake

“Mixtape yangu inakuja mwezi Machi mwakani au pia inaweza kuwahi sababu kuna vitu tunaweka sawa,”

Wimbo wake na Izzo B

Kolabo yake na Izzo B inayokwenda kwa jina la Oh No anasema ilifanyikwa kama zali tu lakini imekuwa poa.

“Hii ngoma kuna watu walinizingua niliotaka kufanya nao, hivyo nilipodondoka kwa Izzo B yani fasta jamaa akanibariki na mashairi yake kwenye ngoma yangu,” alisema.

Elimu na muziki

“Mimi elimu yangu nimeishia chuo na nilianza muziki tangu nikiwa shule na sikuacha shule nimeweza kufanya yote na kwa ubora na kuna mambo naona kabisa elimu inachangia kwa namna muziki wangu ninavyofanya,”

“Nawashauri sana na bado nitaendelea kuwashauri rapa wengi, kamwe wasijaribu kuacha shule sababu ya muziki nawaambia unaweza kufanya vyote kwa wakati mmoja ni wewe kupanga muda vizuri basi,”

“Kwanza muziki ukiwa na elimu kidogo inasaidia katika mambo mengi hata uwasilishaji na ujuzi wako unakuwa vizuri sana,” aliongeza

Kimya kwenye gemu

“Nimekaa kimya kidogo kwenye gemu sababu nilikuwa nafanya mambo mengine ambayo yalikuwa yananibana kuweza kufanya muziki lakini kwa sasa nimeshapanga mambo yangu vizuri na ndio maana nimeachia dude hilo ambalo video yake inakuja baada ya kama wiki mbili,”