Wanatakiwa kuchangamkia fursa hizi

Muktasari:

Anaweza kukuza mtaji mdogo alionao ili kufanikisha ndoto kubwa uliyonayo, lakini inaweza kuchukua muda mrefu. Unaweza kuomba mtaji kwa ndugu na jamaa, lakini njia hii haina uhakika kwa kuwa inategemea na hali.


Ni ndoto ya kila mjasiriamali kukuza mtaji wake. Zipo mbinu mbalimbali ambazo anaweza kutumia kufanikisha malengo haya.

Anaweza kukuza mtaji mdogo alionao ili kufanikisha ndoto kubwa uliyonayo, lakini inaweza kuchukua muda mrefu. Unaweza kuomba mtaji kwa ndugu na jamaa, lakini njia hii haina uhakika kwa kuwa inategemea na hali.

Kuna njia mbadala inayotumiwa na wajasiriamali wengi duniani ambayo ni ufadhili wa mitaji (fellowships and grants) inayotolewa na mashirika mbalimbali duniani.

Kwa wajasiriamali wanaoperuzi mitandaoni mara kwa mara huenda wameshakutana na fursa hizi na huenda wapo wanufaika. Kwa wale ambao ndio kwanza wanasikia habari hizi, wakati ndio huu wa kujaribu bahati yao katika hizi chache.

 

1.Microsoft #INSIDERS4GOOD East Africa Fellowship 2017

Kampuni ya Microsoft inafahamika kwa kusaidia kupitia Taasisi yake ya Bill & Melinda Gates Foundation. Taasisi hii ipo katika nchi za Kenya, Uganda na Tanzania kuwezesha mapinduzi ya wajasiriamali wanaojihusisha na ugunduzi (innovation).

Wajasiriamali 25 watachaguliwa katika mradi huo wa miezi sita na baada ya hapo wataunganishwa katika masoko ya dunia.

Kama unadhani unakidhi mahitaji ya ufadhili huu tembelea tovuti hii:

https://windowsinsiders.azurewebsites.net/Fellowship/EastAfrica

 

 

2.African Entrepreneurship Award

Hii ni nafasi nyingine kwa wajasiriamali wanaotaka kuanzisha biashara zao.

The African entrepreneurship inatafuta mawazo ya biashara kutoka barani Afrika. Unachotakiwa kufanya ni kuingia katika tovuti yao na kuwasilisha wazo lako la biashara.

Mawazo yote ya biashara yatapitia mchujo mara nne na watakaopita wataitwa nchini Morocco kuwasilisha mawazo yao na kupewa mtaji.

Unaweza kuwasilisha wazo tembelea: https://africanentrepreneurshipaward.com/eligibility/

 

 

3. The Tony Elumelu Foundation Entrepreneurship Programme

Mfanyabiashara wa Nigeria, Tony Elumelu ameanzisha mpango wake wa miaka 10 wa kuwawezesha wajasiriliamali 10,000 kwa kuwapa mitaji.

Alianzisha The Tony Elumelu Entrepreneurship Programme 2010 kwa kutenga dola za marekani 100.

Kila mwaka wajasiriliamli 1,000 hupewa mitaji kwa wajisiliamli wenye mawazo ya biashara au biashara zenye umri usiozidi miaka mitatu.

Programu hii hutoa mtaji wa dola za Marekani 5,000 ambazo ni wastani wa Sh10,000. Unachotakiwa kufanya ni kuwasilisha wazo lako kabla ya Machi 1, mwaka huu.

Omba fedha hizo hapa: http://tonyelumelufoundation.org/Programme/


4. Anzisha Prize for African Youth Entrepreneurs

Vijana 15 wa umri kati ya miaka 15 na 22 wananafasi ya kujishindia dola za Marekani 100,000 ambazo ni wastani wa Sh250 milioni kwa ajili ya kuendeleza mawazo au biashara zao.

Washindi watapewa mafunzo katika nchi mbalimbali kabla ya kukabidhiwa fedha zao kwaajili ya kuanzisha biashara.

Kijana anayetaka kushiriki anaweza kutembelea tovuti ya Anzisha:

http://youtheconomicopportunities.org/announcement/8474/fellowship-anzisha-prize-african-youth-entrepreneurs

 

 

5. Unreasonable East AFrica Fellowship

Ni programu inayowezesha kutoa mafunzo na misaada kwa biashara zinazoanza kuchipua na mashirika yasiyojiendesha kwa faida. Kila mwaka kwa miezi 10 huendesha mafunzo, kuyaktuanisha mashirika ba wafadhili na kuendesha harambee kwa ajili ya kuyasaidia mashirika hayo.

Kwa mashirika yanayohitaji mafunzo na misaada hii ndiyo sehemu sahihi ya kuwamo kwaajili ya kukukua na yanayojiendesha kwa faida ni sehemu sahihi ya kukutana na wadau.

Kwa namna ya kujiunga tembelea: http://unreasonableeastafrica.org/