Mastaa Kane, Ronaldo wakutana Bernabeu

Muktasari:

  • Real Madrid walisawazisha bao kupitia kwa mshambuliaji wao, Cristiano Ronaldo mchezo ulioisha kwa sare.

Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo na mwenzake Harry Kane wa Tottenham, walionyesha kazi jana Jumanne kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa iliyoisha kwa sare ya bao 1-1.

Mastaa hao walikutana dimbani huku kukiwa na mipango ya uongozi wa Madrid kumsajili Harry Kane kwa dau lolote ili kuhakikisha anaitumikia miamba hiyo ya Hispania.

Tottenham ndiyo inaongoza kwenye kundi lao ikiwa na poiti saba, pia wakifuatiwa na Real Madrid wenye pointi saba, huku nafasi ya pili wakiwa BVB Dortmund wenye pointi moja sawa na Apoel Nicosia wenye pointi moja mkiani.