Ajib ajisalimisha Yanga

Mshambuliaji  wa Yanga Ibrahim Ajib.

Muktasari:

  • Ajib ametua mazoezini asubuhi hii akiwa pamoja na wenzake.

Morogoro. Hatimaye mshambuliaji Ibrahim Ajib amewasili kambini Yanga Mkoani Morogoro.

Ajib ametua mazoezini asubuhi hii akiwa pamoja na wenzake.

Ajib alionekana kukimbia peke yake nje ya uwanja baada kukosa sehemu kubwa ya mazoezi na wenzake.

Kuwasili kwa Ajib kunafanya sasa kusalia mchezaji mmoja pekee Mohammed Issa 'Banka'  ambaye bado hajajiunga na timu hiyo.