Cannavaro auwazia ubingwa Yanga

Muktasari:

  • Asema Simba kuongoza ligi sio sababu ya timu yake ya Jangwani kuizuiwa kutwaa ubingwa.

Beki na nahodha wa Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema licha ya Simba kuongoza katika msimamo wa Ligi Kuu Bara, lakini bado kikosi chao kina nafasi kubwa ya kutetea ubingwa.

Canavaro amesema tofauti ya pointi mbili kati yao na Simba wanaongoza ligi ni kitu kilicho ndani ya uwezo wao kuiweza kuwashusha na sasa wanajipanga vyema kwa hatua hiyo.

Mkongwe huyo alisema mazoezi wanayofanya sasa ni maalum kwa kuhakikisha ligi itakavyoanza wanakuwa tayari ambapo endapo wenzao waliokuwa katika Micchuano ya Kombe la Chalenji watajiunga mapema watakuwa na maandalizi kamili kwa ligi.