Messi: Sitaki kupangwa na Hispania

Muktasari:

  • Ratiba ya Kombe la Dunia 2018 itapangwa mwezi ujao.

Moscow, Russia. Wakati Hispania ikiwa kundi la pili katika upangaji wa ratiba ya Kombe la Dunia itakayofanyika Desemba 1, Lionel Messi amesema angependa Argentina isipangwe pamoja na Hispania.

Pamoja na kufuzu kwa shida kwa fainali hizo za 2018, Russia bado Argentina  imepangwa kundi la kwanza shukrani kwa kazi kubwa ya Messi aliyofanya katika mechi ya mwisho dhidi ya  Ecuador.

"Ningependa tusikutana na Hispania katika hatua ya makundi kwa sababu ni timu ngumu zaidi kucheza naye," aliimbia TyCSports.

Argentina kwa sasa inajiandaa kwa mechi mbili za kirafiki dhidi ya Russia na Nigeria.

Messi ametumia nafasi hiyo kuweka mambo sawa kuhusu tetesi kwamba yeye ndiye anayepanga wachezaji na makocha wa timu ya taifa.

"Wakati wanapozungumzia kuhusu marafiki wa Messi inanifanya nicheke tu," aliongeza. "Wanasema kuwa ndiye ninayechagua makocha na wachezaji wa kuchezea Argentina, huo ni uongo.

"[Javier] Mascherano, [Angel] Di Maria, [Lucas] Biglia ni wachezaji wakubwa duniani, madai hayo ni kuwavunjia heshima. Hivyo sivyo nilikuwa mimi hata kidogo.