Mashabiki watua kibabe hoteli ya Simba

Muktasari:

  • Simba inashuka dimbani leo saa 10 jioni kucheza mechi yake dhidi ya Nkana Rangers huku mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi waliosafiri wakitarajiwa kuipa sapoti ya nguvu wakiwa dimbani.

Mashabiki wa Simba wamewasili katika Hoteli ya Milford saa 07:11 mchana ambapo kikosi cha timu hiyo kiliweka kambi.

Mashabiki hao wa Simba waliwasili katika hoteli hii na basi kubwa kama la kusafiri mkoani ambalo walikodiwa na uongozi wa Simba.

Mashabiki hao walikuja na basi la Simba ambalo walipata nalo ajali jana wakiwa njiani kuja hapa Kitwe na basi hilo muda huu lipo gereji kwa matengenezo.

Mara baada ya kufika hapa hotelini mashabiki wa Simba walifika hapa hotelini huku wakipiga ngoma.

Mara baada ya kumaliza kupiga ngoma walishuka na kuanza kucheza mbele ya hoteli hii na muda huu wapo nje ya hoteli wakisubiri timu ili waongozane nayo uwanjani.