Liverpool, Man City wasubiri wabaya wao Ulaya

Muktasari:

  • England ilikuwa na timu tano katika hatua ya 16 bora zimetoka tatu na kubaki mbili tu

Liverpool, Manchester City na vigogo Ulaya wanajiandaa kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa itakayopahwa mjini Nyon leo mchana.

Liverpool na Manchester City ndiyo timu pekee zinazopeperusha bendera ya Ligi Kuu England pia kuna uwezekano wa kucheza wenyewe.

Kuanzia hatua hii ratiba ipo wazi kwa timu za nchi moja kukutana au kucheza na timu uliyokuwa nayo kundi moja.

Timu nane zilizosalia katika mashindano hayo ukiangalia rekodi yao na mafanikio katika mashindano hayo:

BARCELONA

Lionel Messi ndiyo tishio zaidi akisaidiwa na Luis Suarez. Kwa sasa wanaongoza La Liga kwa tofauti ya point inane hivyo wanaweza kuweka akili yao katika Ligi ya Mabingwa zaidi.

Kocha: Ernesto Valverde

Mchezaji Nyota: Lionel Messi

Mafanikio yao: Ubingwa 1992, 2006, 2009, 2011, 2015.

 

BAYERN MUNICH

Kocha Jupp Heynckes ametwaa taji hili akiwa na  Real Madrid na Bayern. Sasa anataka kunyakuwa taji hilo kwa mara ya tatu.

Kocha: Jupp Heynckes

Mchezaji Nyota: Robert Lewandowski

Mafanikio yao: Ubingwa 1974, 1975, 1976, 2001, 2013

JUVENTUS

Pamoja na kushindwa kuonyesha kiwango cha kuridhisha dhidi ya Tottenham, lakini wamefanikiwa kusonga mbele.

Kocha: Massimiliano Allegri

Mchezaji Nyota: Paulo Dybala

Mafanikio yao: Ubingwa 1985, 1996

 

LIVERPOOL

Walikuwa bora zaidi kwa Porto wamefuzu kwa hatua hiyo wakiwa na rekodi ya kutopoteza mechi hadi sasa. Washambuliaji wake watatu Mo Salah, Roberto Firmino na Sadio Mane wamefunga kila mechi.

Kocha: Jurgen Klopp

Mchezaji Nyota: Mohamed Salah

Mafanikio yao: Ubingwa 1977, 1978, 1981, 1984, 2005

MAN CITY

Kocha Pep Guardiola amethibisha ubora wake kwa kutegeneza timu ya ushindi. Tayari wanakaribia ubingwa wa Ligi Kuu England, hivyo akili ya City sasa ni kutamba Ulaya.

Kocha: Pep Guardiola

Mchezaji Nyota: Kevin De Bruyne

Mafanikio yao: Nusu fainali 2016

 

REAL MADRID

Swali kuhusu hatma ya Zinedine Zidane, litasahaulika kama atafanikiwa kutwaa taji la tatu mfululizo.

 Kocha: Zinedine Zidane

Mchezaji Nyota: Cristiano Ronaldo

Mafanikio: Ubingwa 1956, 1957, 1958, 1959, 1960, 1966, 1998, 2000, 2002, 2014, 2016, 2017

 

ROMA

Baada ya kuondolewa hatua hiyo dhidi ya Chelsea na Atletico Madrid, safari hii imevunja mwiko kwa kuichapa Shakhtar kwa sheria ya bao la ugenini katika hatua ya 16 bora.

Kocha: Eusebio Di Francesco

Mchezaji Nyota: Edin Dzeko

Mafanikio yao:  Washindi wa pili 1984

 

SEVILLA

Mara ya mwisho kufuzu kucheza robo fainali ilikuwa 1958, Sevilla wamerudi upya baada ya kuiondoa Manchester United.

They are not the side that won three straight Europa Leagues but have responded well to former AC Milan boss Vincenzo Montella.

Steven N’Zonzi is the midfield powerhouse and Wissam Ben Yedder, who scored two against United, has been a real surprise package.

Kocha: Vincenzo Montella

Mchezaji Nyota: Wissam Ben Yedder

Mafanikio Yao: Robo fainali 1958, 2018