VIDEO: Okwi, Chama, Dida hatihati kuivaa Prison

Muktasari:

  • Akizungumzia hatma ya wachezaji hao watatu Afisa Habari wa Simba, Haji Manara alisema Okwi ni majeruhi, huku Chama na Dida bado ITC zao hazijafika nchini.

Dar es Salaam. Simba uenda ikiwakosa nyota wake mshambuliaji Emmanuel Okwi, kipa Deogratius Munishi na kiungo Cletus Chama katika mchezo wa kesho dhidi ya Prison kutokana na sababu mbalimbali.

Akizungumzia hatma ya wachezaji hao watatu Afisa Habari wa Simba, Haji Manara alisema Okwi ni majeruhi, huku Chama na Dida bado ITC zao hazijafika nchini.

Mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, Okwi aliumia katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Mtibwa Sugar mwishoni mwa wiki.

Manara alisema Okwi ana asilimia 75% za kucheza mchezo huo baada ya kuzungumza na Daktari Yassin Gembe.

"Okwi aliumia mgongo lakini maendeleo yake ni mazuri mpaka hivi sasa, nimeambiwa kwamba suala la kucheza ni itategemea na mwalimu kama anahitaji kumtumia," alisema Manara.

Kuhusu kuchelewa kwa hati zao za uhamisho (ITC) Munishi ‘Dida’ na Chama, alisema suala hilo linafuatiliwa kwa ukaribu, lakini wachezaji hao wana asilimia chache za kucheza mchezo wa kwanza.