Nanasi linavyousaidia mwili kukabili maradhi

Muktasari:

  • Nanasi ni miongoni mwa matunda yenye ladha nzuri mdomoni, lakini pia lina vitamini nyingi na virutubisho vyenye uwezo wa kuupa mwili nguvu na kuepuka kushambuliwa na maradhi.

Mwili unapokosa kinga imara, huwa katika hatari ya kushambuliwa na kila aina ya maradhi. Ili kukabilina na hali hiyo, tunda la Nanasi linazosifa za kukabiliana tatizo hilo.

Nanasi ni miongoni mwa matunda yenye ladha nzuri mdomoni, lakini pia lina vitamini nyingi na virutubisho vyenye uwezo wa kuupa mwili nguvu na kuepuka kushambuliwa na maradhi.

Kwenye Nanasi kuna kirutubisho aina ya Bromelain kinachopatikana kwa wingi na virutubisho hivyo hulifanya tunda hilo kuwa na umuhimu kwa kujenga na kuimarisha kinga ya mwili wa binadamu.

Ulaji wa tunda hilo mara kwa mara unamsaidia mlaji kujikinga dhidi ya ugonjwa wa kuvimba koo, baridi yabisi, gauti na hutibu matatizo ya tumbo na bandama.

Wataalamu wengi wa afya wanashauri ili binadamu upate kinga dhidi ya maradhi, anashauriwa kula tunda hilo kabla au baada ya mlo wake na wala asile nanasi na chakula kingine kwa wakati mmoja.

Usipofanya hivyo, virutubisho vilivyopo katika nanasi vitafanya kazi nyingine tofauti na ile iliyokusudiwa.

Nanasi lina virutubisho vya vitamin A,B na C na lina madini ya chuma, kopa na Phosphorous ambayo ni muhimu kwa afya ya binadamu.

Pia, tunda hilo hutibu matatizo ya ini, homa, vidonda vya mdomoni na husaidia kusafisha utumbo mwembamba.

Kwa wale wanaopoteza kumbukumbu, nanasi linao uwezo wa kutibu.

Linasaidia pia kutibu maradhi ya akili, kukosa mori, kutibu matatizo ya wanawake hasa ya upungufu wa hormoni na matatizo mengine ya sehemu za siri za mwanamke na husaidia kupata choo laini na kwa wakati.

Tatizo la upungufu wa damu pia linatatibiwa na nanasi ambalo pia husaidia kuongeza maziwa kwa wanawake wanaonyonyesha. (Hadija Jumanne)