UTI hatari kwa wajawazito, inaweza kuporomosha ujauzito

Muktasari:

  • Inaelezwa mambo yanayochangia kuugua ugonjwa huo ni urethra kuwa fupi. Urethra ni mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kupeleka nje. Na mrija huo upo, karibu na njia ya haja kubwa, hal, ambayo hurahisisha uwezekano wa bakteria kuingia katika mfumo wa mkojo na kusababisha maradhi ya UTI

Utafiti wa kisayansi uliofanyika unadhihirisha wanawake hasa walio vunja ungo wapo katika hatari ya kupata maradhi ya UTI ukilinganisha na wanaume.

Inaelezwa mambo yanayochangia kuugua ugonjwa huo ni urethra kuwa fupi. Urethra ni mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kupeleka nje. Na mrija huo upo, karibu na njia ya haja kubwa, hal, ambayo hurahisisha uwezekano wa bakteria kuingia katika mfumo wa mkojo na kusababisha maradhi ya UTI.

Hatari ya UTI

UTI ni moja ya maradhi hatari hasa pale yanapowakumba wajawazito. utafiti unaonyesha takribani asilimia 40 ya wanawake wanaishi na UTI ambayo haijatibiwa na huwasababishia wapate matatizo mbalimbali yanayohatarisha maisha yao na ya mtoto wakati na hata baada ya ujauzito.

Sababu zinazomfanya mjamzito kuwa katika hatari ya kuugua UTI

Kutoweza au kupoteza uwezo wa kukamilisha haja ndogo kikamilifu, matatizo katika mirija ya mkojo yanatokana na mawe katika figo, kukunjamana kwa mirija ya urethra na ureta, mimba kugandamizwa ureta pamoja na matatizo katika mfumo wa fahamu, kushuka kwa nguvu kinga ya mwili, hali ambayo huuweka mwili katika hatari ya kushambuliwa na maradhi mbalimbali. Ugonjwa wa kisukari pamoja na vipimo vya hospitali visivyo salama anavyohudumiwa mjamzito huweza kuchangia maradhi hayo na kuvimba kwa kuta za urethra.

Mambo mengine yanayochangia ni pamoja na kushuka kwa kinga ya mwili, ujauzito kukandamiza mirija ya mkojo na kibofu. Bakteria wanaopanda kutoka kwenye mrija unaotoa mkojo nje, yaani urethra na kuingia kwenye kibofu kisha kuzaliana. Hali hii husababisha UTI kwenye kibofu.

Sababu nyingine ni pale bakteria wanapotoka kwenye mfumo damu na kuelekea kwenye figo.

Mfano wa bakteria hawa ni Escherichia coli, proteus, pseudomonas, Klebsiella na Staphylococcus hasa kwa wenye ugonjwa wa kisukari.

Sehemu za mfumo wa mkojo zinazoathiriwa na UTI.

Mrija unasafirisha mkojo kutoka kwenye kibofu kuelekea nje unapovimba, husababisha urethritis.

Kuvimba kwa kibofu husababisha cystisis. Kuvimba kwa mirija inayotoa mkojo kwenye figo kupeleka kwenye kibofu yaani ureters husababisha ureteritis na uvimba kwa figo husababisha pyelonephritis.

Namna ya kujitambua kuwa tayari una UTI.

Mtu aliye na maambukizi ya UTI mara nyingi huugua homa mara kwa mara na hupatwa na maumivu ya mgongo hasa eneo la kiuno, kujisikia kichefuchefu na kutapika hasa wakati bakteria wanapoanza kushambulia kwenye figo, kupata hamu ya kukojoa mara kwa mara, maumivu ya kichwa, uchovu wa mwili mzima, maumivu wakati wa kukojoa, kukojoa mkojo uliochangamana na damu na usio na harufu ya kawaida, maumivu wakati wa tendo la ndoa na maumivu sehemu za kibofu. Unapopatwa na dalili hizo, muone daktari mapema.

Matatizo yananayosababishwa na UTI wakati wa ujauzito.

Ugonjwa huo ni hatari kwa mjamzito kwani unaweza ukasababisha mimba kutoka kama hautatibiwa mapema.

Na wakati mwingine husababisha mjamzito akajifungua mtoto kabla muda na wengine hujikuta wakijifungua mtoto akiwa na uzito mdogo wa chini ya uzito wa kawaida wa kilo 2.5 yaani njiti.

Lakini wapo ambao pia huwasababishia motto akafia tumboni pamoja na kupungukiwa damu na maji.

Namna ya kujikinga na UTI.

Ili kujikinga na mhi hayo, madaktari wanashauri mtu anywe maji ya kutosha, kwa siku isiwe chini ya lita moja na nusu. Pia aepuka kula vyakula vyenye sukari nyingi ikiwamo kunywa pombe, chocolate na vyakula vyenye kahawa.

Inashauriwa kujenga tabia ya kukojoa mara ubanwapo na mkojo. Kwa kufanya hivyo kutasaidia kupunguza uwnwa mkojo awahi kwenda kujisaidia badala ya kuubana ni hatari.

Inashauriwa kujenga tabia ya kuoga na kukojoa kabla na baada ya tendo la ndoa. Kufanya hivyo husaidia kuondoa bakteria walioko sehemu za siri.

“Epuka tendo la ndoa kama bado upo katika matibabu ya UTI na baada ya kukojoa usifute bali kausha sehemu zako siri ziweke safi na kavu muda wote na kama utazifuta hakikisha unafuta mbele kuelekea nyuma,” inaelekezwa.

Ni vizuri kuepuka kuvaa nguo za ndani zinazobana na hakikisha zile uzivaazo ni safi. Nguo za ndani aina ya kotoni zinapendekezwa zaidi kutumika sambamba na kula vyakula vyenye vitamini C kama matunda aina ya machungwa huwa na asidi ambayo husaidia kuondoa bakteria.

Dk kammu Keneth, anapatikana kwa namba 0759 775788.