
| Rais Nkurunzinza aahidi kusimamia sera ya kilimo | Send to a friend |
| Wednesday, 20 April 2011 08:40 |
|
Nkurunzinza alisema sera bora ya kilimo itasaidia kukua kwa sekta hiyo na kupanua soko la mazao ya jumuiya kimataifa. “Tunatakiwa kuboresha na kuongeza ujuzi katika kilimo ili kukuza soko letu la kimataifa,” alisema. Katika mkutano huo viongozi wa EAC, walimteua Dk Richard Sizibera wa Rwanda kuwa Katibu Mkuu mpya wa jumuiya hiyo na Dk Enos Bukuku, kuwa Naibu katibu mkuu wake. Akizungumza baada ya kuapishwa, Sizibera alisema atasimamia sera za jumuiya hiyo na kuboresha soko la pamoja. Sizibera alisema suala la ushuru wa pamoja nao ataendelea kuboresha na kusimamia jumuiya ya EAC kuwa bora zaidi. “Nitaendeleza yale yaliyokuwa yamepangwa na katibu aliyemaliza muda wake na kuboresha mengine,” alisema. Hata hivyo, Sezibera alisema hajui ni changamoto atakazokutana nazo hadi atakapoanza kazi rasmi. |



Boniface Meena











Comments