MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa ATCL hoi bin taabani: Serikali
BOOKMARK THIS PAGE
ATCL hoi bin taabani: Serikali  Send to a friend
Tuesday, 02 August 2011 19:47

NDEGE zote zilizonunuliwa miaka  37 wakati wa kuanzishwa kwa Shirika la Ndege Tanzania(ATCL), hazifanyi kazi, Bunge lilielezwa jana.Akijibu swali la nyongeza kutoka kwa David Kafulila (NCCR-Mageuzi- Kigoma Kusini), Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu alisema  shirika hilo lilianzishwa mwaka 1973 na kupewa  ndege 11 kama kianzio, lakini kwa sasa hakuna hata moja inayofanya kazi.

Katika swali lake, Kafulila alitaka kujua kuna ndege ngapi zinazofanya kazi na akahoji ni kwa nini kwa muda mrefu Tanzania inashindwa kuwa hata na ndege moja kama ilivyo kwa nchi ndogo kama Burundi.Awali, katika swali la msingi,  Rukia Ahmed (Viti Maalum-CUF) alitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kusafisha menejimenti pamoja na shirika hilo.

Mbunge huyo pia alitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kufufua Shirika la ndege la Tanzania kutokana na shirika hilo kuonekana kuelekea kufa.Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athuman Mfutakamba alisema  Serikali  inatambua na kutafuta namna bora ya kulifufua shirika hilo ili liweze kuwa imara kama ambavyo Watanzania wanatarajia.

Alisema kuwa Serikali iko katika mchakato wa kuteua menejimenti na bodi mpya ambayo itakuwa na uwezo wa kusimamia Kampuni ya Ndege ya Tanzania ili iweze kufikia malengo.

Naibu Waziri alisema kwa sasa Serikali inatarajia kuipatia kampuni vitendea kazi na mtaji wa kujiendesha ili iweze kuendeshwa kwa biashara bila ya kutegemea ruzuku kutoka serikalini.Alisema serikali iko mbioni kumpata mbia mahiri na mwenye uwezo wa kubadilisha ATCL iweze kutoa huduma za hali ya juu kwa ufanisi mkubwa sambamba na kampuni zingine nchini.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri, ndege iliyokuwa kwenye metengenezo nchini Afrika ya Kusini, inatarajia kurudi nchini Agosti 8 kwa kuwa sasa iko tayari kwa ajili ya kutoa huduma.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
+1 #9 2011-08-03 22:21
uwekezaji wowote usiokuwa na uwajibikaji ni sawa na kutupa pesa au kutwanga maji kwenye kinu kitu cha kwanza cha kufanya kabla serikali haijawekeza kodi za wananchi ATCL inabidi kuwakamata na kuwashugulikia wale wote waliolifikisha shirika hilo hapo lilipo. bila ya hivyo hao wapya wataoingizwa watafanya kama wenzao kwani hakuna kilichowafika wenzao kwao wao wataogopa nini kufuata nyayo za wenzao?dawa ya ATCL ni kupewa mtu binafsi kwa maana mtu binafsi hawezi kuruhusu ubadhirifu mfani mzuri PRECISION AIR.
Quote
 
 
+1 #8 2011-08-03 20:40
MKITAKA KUJUA CCM NI CHAMA CHA MADUNGAEMBE, NAOMBA MNUKUU HOTUBA NA MANENO ALIYOYASEMA WAZIRI BUNGE HILI. KISHA SUBIRINI BUNGE LA JULAI MWAKANI NAWAHAKIKISHIA ATARUDIA MANENO HAYAHAYA "serikali inampango madhubuti wa kumpata mbia amabye ataliwezesha shirika lijiendeshe kibiashara"
NI MANENO KAMA HAYAHAYA MIMI NILIYASIKIA MWAKA JUZI, HIVYO HAWA CCM HUA SI WATEKELEZAJI WANACHEZA NA AKILI ZETU, WANACHOKIFANYA NI COPY AND PASTE ZA HUTUBA NA EDITING.
JAMANI JIULIZENI KWANI KUTEUA BODI HUA INACHUKUA MIEZI AU MIAKA MINGAPI WAKATI SERIKALI INAWAJUA WATU NA CV ZAO ZINAJULIKANA?
Quote
 
 
+1 #7 2011-08-03 17:30
hahahahaa wananichekesha wanajifanya wamesahau kuwa wao ndio waliua ATCL....nakumbuka 1998 nilipanda ile boeing yenyewe na twiga wake lkn...sera mbovu za CCM ndio zimefikisha hilo shirika hapo, kwanza waliuza zile fokker 2 au 3 hivi, then wakapiga bei zile twin otters halafu wakaingia ubia na south african airways ambapo ndio ikawa mwisho wa shirika letu......Mimi nawaombea kwa Mungu walaaanike wote walioua hilo shirika halafu hapo bungeni wanajifanya hamnazo tunakumbuka
Quote
 
 
+1 #6 2011-08-03 14:42
Suala la ATC itaendelea kuwa historia hata kama itapewa mtaji. huwezi kuingia akilini shirika lilikuwa na ndege 11 alafu zimekufa zote tena enzi hizo hakukuwa na ushindani hv sasa itaweza? kwanza wahujumu wa ATC ni hao hao mafisadi kwa wana hisa Precision air hivyo wataendelea kuiwa ATC ili Precision air inendelee kudumu.
Quote
 
 
+1 #5 2011-08-03 09:35
Serikali hata ukiipa ATCL mtaji wa mabilioni ya shillingi bila usimamizi mathubuti haisaidiii. shida ya ATCL haikuwa mitaji, shida ni usimamizi mbovu. Rwanda air inakuja juu, Precision air wako mbali sana, kwa sababu ya usimizi bora.
Quote
 
 
+2 #4 2011-08-03 09:04
Hi swala la mheshimiwa kusema wanatafuta mbia mahiri na njia bora ya kutafuta uwekazekaji ATCl ni sawa na kuweka mvinyo mpya kwenye bilauri ya zamani.Mfumo ni ule ule.Inasikitisha sana kuona kila mkukicha tunambiwa zilezile ngojera na hekaya zile zile za Abunuasi.Kwa nini wasisifunnze kwa nchi kama Ethiopia (Ethiopia Airline) au basi wauzie kwa Precision air kwani mwaka hadi wananunua ndege mpya,kwani wanajua sana kuna soko la usafri wa hapa TZ.Hivi watawala wetu wanatupeleka wapi?Mwaka jana nilipata fursa ya Kwenda Uholanzi,nilish angaa sana kuona ile nchi ya kibepari miaka mingi lakini usafiri wa Basi,treni upo chini ya uangalizi wa serikari and best in Europe,usisahau shirika lao kubwa la KLM na midege yao airbus.We need visionary and selfless leaders in TZ!!!!!
Quote
 
 
+1 #3 2011-08-03 06:43
Kweli halli mbaya nchini kwetu TANZANIA mpaka mtu some time unalia.Mimi nipo nchini CHINA wenzutu wamekeza sanaaaaaaaaa kwenye usafiri NDEGE mpaka nikaogapa first time to be in DOHA(QATAR)and CHINA.Madini tunayo TZ still bado masiki MUNGU ATUPE NINI JAMANI
Quote
 
 
+2 #2 2011-08-03 06:19
Hivi mnajua kuwa huyu bwana Mfutakamba ambaye ni waziri wa kikwete ana uraia wa marekani? Alipokwenda kusoma alibadilisha uraia na mpaka sasa hivi bado anao.
Quote
 
 
+1 #1 2011-08-03 04:15
Kwakweli CCM inatisha yaani Mwalimu alinzisha shilika na ndege 11 limekufa hawa ma -fa-la wameshindwa kuongoza kabisa 'Serikali iko katika mchakato wa kuteua menejimenti na bodi mpya ambayo itakuwa na uwezo wa kusimamia Kampuni ya Ndege ya Tanzania ili iweze kufikia malengo.hapo kama kweli Kikwete anayo akili achague vijana wapya toka chuoni kuanzia bodi hadi wafagiaji vijana kwa ndege mpya, hawa wazee wametulostisha kabisa yaaani Tanzania tunaiuwa wenyewe,dawa ni kawa uwa wote walitufikisha hapo yaaani inaumiza sana sana sana sana sana.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner