MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Kombani: Daraja la Kilombero litajengwa
BOOKMARK THIS PAGE
Kombani: Daraja la Kilombero litajengwa  Send to a friend
Thursday, 20 May 2010 19:03

Samuel Msuya,Morogoro
SERIKALI imewahakikishia wananchi wa Wilaya za Ulanga na Kilombero, mkoani Morogoro, juu ya azma yake ya kukamilisha ujenzi wa daraja la Mto Kilombero, ndani ya kipindi kingine cha miaka mitano ya uongozi wa Rais Jakaya Kikwete.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa), Celina Kombani, akiwa katika  ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Jimbo la Ulanga Mashariki.

Waziri huyo pia ni mbunge wa jimbo hilo.

Kombani alisema katika kipindi cha muhula wa kwanza wa uongozi wa Rais Kikwete, serikali ilikuwa inakamilisha hatua za usanifu na upembuzi yakinifu wa ujenzi wa daraja hilo.

Alisema hatua hizo sasa zitafuatiwa na kuanza kwa ujenzi utakaofanyika ndani ya muhula wa pili wa serikali ya awamu ya nne.

Kauli hiyo ilikuja baada ya baadhi ya wananchi wa Ulanga, kumuuliza waziri huyo kuhusu mpango wa serikali kujenga daraja la Mto Kilombero, ambalo Rais Kikwete aliahidi kulinega.

 
Akiwajibu wananchi hao, Kombani alisema ujenzi wa daraja katika Mto Kilombero, uko katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) na kwamba lazima ufanyike.
 
Alisema tayari serikali imeshatumia zaidi ya Sh 800 milioni kwa ajili ya hatua za awali za ujenzi wa daraja hilo, likalomaliza kero ya wananchi wa wilaya hizo mbili, kuvuka katika mto huo mkubwa.

Waziri Kombani alisema kwa sasa serikali iko katika mchakato wa mwisho wa kulitafutia fedha daraja hilo ili ujenzi wake uanze mapema iwezekanavyo.
 
Aliwataka wananchi wa Wilaya za Ulanga na Kilombero, kuachana na baadhi ya wanasiasa wa vyama vya upinzani wanaodai kuwa daraja hilo halitajengwa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #4 2010-07-28 11:15
umoja wa [NENO BAYA] ccm
Quote
 
 
0 #3 2010-07-28 11:08
huyo mh.anatufanya watu wa ulanga wa[NENO BAYA] ndio maana kukifika wakati wa kqmpeni ndio anajifanya kutujursha habari za daraja mbona hapa katikati alikuwa asemi kwanini au uchaguzi unakalibia ndio yanamtoka yote ..ahache kutudanganya yeye kama anataka kula asfme maana sisi watu wakilombero bado hatujajitambua kuhusu nini maana ya vyama vingi ....tubadilike kila siku tunadanganya mpakalini?
Quote
 
 
0 #2 2010-07-12 09:27
Ndugu zanguni sisi wakazi wa kilombero tutadanganya mpaka tukome maana uchaguzi ukikaribia wana tuambia daraja la mto kilombero litajengwa lini maana inapofikatu uchaguzi ndiowana anza kuliongerea wanataka kuhuwatena nduguzetu kama mwanzo hao ndio ccm bwana kwenye kampeni ahadi nyingi vitendo hakuna watanzania tufanye uhamuzi uliosahihi uchaguzi unapofika hapo octoba kiongozi ambaye atufai tumpige chini wamezoea kula ruhwa hao ,sinamengi mzee wa kuponda kuhusu ukweli mnatudanganya tumechoka kudanganya tutafanya uhamuzi uliosahii
Quote
 
 
0 #1 2010-05-21 14:10
Mheshiwa Kombani acha hii danganya toto! kama unataka kura zetu tutakupa kwa sababu upinzani hauna nguvu sana katika Wilaya hii ya Ulanga. Ila hii ya kukupa kura zetu usitufanya kuwa sisi wapongoro [NENO BAYA]... la hasha!Ujenzi wa daraja hili umeshalizungumz ia mara ngapi miaka ya nyuma? kama hukumbuki tutakwambia.. Dr Shein alipofika huko Ulanga alitwanbia Nini? kama hukumbuki tutakukukbusha... Tunakuomba ukae kimya lakini siyo kutudanganya na kutufanya [NENO BAYA]... hizi bla bla za kabla ya uchaguzi tumechoka nazo.. tunataka vitendo sasa. Pesa za kumshafirisa Raisi nje ya nchi zipo, pesa za kuwafanya mawaziri wazunguke nchi nzima ili kueleza mafanikio ya Serikali zipo... pesa kwa ajiri ya daraja la mto kilimbero..? Tunaomba usituchafue wana Ulanga kwani tuna uchungu sana da swala hilo.
Mdau wa kata ya Ruaha, mahenge.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner