
| ‘Serikali, mashirika ziondoa kero kilimo na mifugo’ | Send to a friend |
| Saturday, 28 January 2012 08:51 |
|
SERIKALI imetakiwa kushirikiana na mashirika mbalimbali yanayojihusisha mifugo na kilimo ili waweze kuwasaidia kutatua kero mbalimbali zinazokabili sekta hiyo zilizodumu muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi hali iliyosababisha sekta hiyo kushindwa kutoa mchango mkubwa katika kusaidia kuleta maendeleo kwa jamii. Hayo yalibainishwa kwenye mkutano ulioitishwa na wadau wa sekta ya nyama nyekundu uliandaliwa kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Uholanzi (SNV) kushirikiana na Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) kwaajili ya kujadili mafanikio na matatizo yanayoikabili sekta hiyo uliofanyika mkoani Morogoro. Mratibu wa SNV, Silvanus Mruma alisema kuwa mfumo wa uingizaji wa chanjo nchini umekuwa ukisababisha kukosekana kwa chanjo za mifugo kirahisi hivyo kuiiasa Serikali kufanya utafiti juu ya usimamizi na uendeshaji wa utoaji chanjo nchini ili kupata ufumbuzi wa kero katika sekta hiyo inayoshikiliwa zaidi na wadau mbalimbali wa kilimo na ufugaji. Mruma alisema kuwa licha ya sekta hiyo kukumbwa na matatizo ya chanjo bado maofisa na wasimamizi wa sheria za mifugo wamekuwa wakikabiliwa na tatizo la kuingiliwa kiutendaji na wanasiasa hivyokushindwa kufanya kazi zao kwa ufanisi akieleza kuwa wakati umefikia kwa maofisa hao kusimamia sheria kwa kuwajibike kwa wizara ili wafanye kazi zao bila kuingiliana katika madaraka . Alisema kuwa baada ya kero hiyo kugundulika chama hicho kimeamua kuunda kikosi kazi kitakachoshirikiana na wadau mbalimbali wa nyama nyekundu kutatua kero hizo na kupata ufumbuzi wa matatizo yanayoikabili sekta hiyo. Alisema kuwa mkutano huo ulichagua kikosi kazi chenye wajumbe watano ambao kwa pamoja watahusika katika kusimamia utekelezaji wa mambo mbalimbali yatakayosaidia kuondoa kero zinazoimkumba sekta ya nyama nyekundu ikiwemo ya utoaji wa chanjo kwa wakati. Mbali na hayo kikosi kazi hicho kutasaidia ujengwaji wa majosho kwaajili ya mifugo na utoaji wa pembejeo za mifugo kwa wakati hali aliyosema itasaidia kuimarisha sekta hiyo na kutoa mchango katika kujenga uchumi kikamilifu. |













