MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Serikali yataka VETA kudahili maradufu
BOOKMARK THIS PAGE
Serikali yataka VETA kudahili maradufu  Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 08:38

Zaina Malongo  
VYUO vya Elimu ya ufundi nchini (VETA), vimetakiwa kuongeza mara dufu  idadi ya wanafunzi inaowadahili kwa mwaka ili kusaidia Serikali kufikisha idadi ya wataalamu  635, 000 ifikapo mwaka 2025

Naibu Katibu Mtendaji Ofisi ya Rais Tume ya Mipango,  Clifford Tandari alitoa agizo hilo wakati wa mkutano na wanafuzi wa Kitanzania waliosoma  nchini Japan kwa msaada wa  Asasi ya Shirikisho la Maendeleo nchini Japan (JATA).
 Alisema kuwa Serikali imekuwa ikipata wataalamu wachache  kwa mwaka huku  mahitaji yake ywa kipindi hicho yakiwa wataalamu  635,000  kutoka katika vyuo vya ufundi nchini.  

Tandari aliwataka vijana kuchangamkia nafasi hiyo ili waweze kupata fursa hiyo akieleza kuwa Serikali imetoa ruzuku kwa vyuo vya ufundi nchini.

Alifafanua kuwa kutokana na ruzuku hiyo vyuo hivyo vinatakiwa kutoza Sh 60,000 kwa mwanafunzi anayesomea ufundi kwa nafasi ya kutwa na Sh 120,000 kwa mwananfunzi wa bweni badala ya kulipia 800,000  au  1,000,000 ilivyokuwa awali.

 Naibu Katibu huyo alisema kuwa katika kipindi cha miaka mitano ya mipango ya Serikali wamefungua milango kupitia soko huria la Afrika Mashariki (EAC), ili walimu kutoka katika nchi za Kenya, Rwanda na Burundi kuingia Tanzania na kusaidia kuziba pengo la walimu katika masomo hisabati na sayansi.
 
Alisema  kuingia kwa walimu hao nchini kutatoa nafasi kwa  wanafunzi  waliopo shuleni kupenda masomo ya sayansi ambayo alisema yanampa mwanafunzi nafasi ya kujiunga na vyuo vya ufundi ili baadaye nchi iweze kufikia wastani mzuri wa wataalamu.

Awali akizungumza katika mkutano huo Kaimu Mwenyekiti wa JATA Dk Peter Matesa alisema lengo la kukutanana kwao ni kutaka  kujadili mada mbalimbali zinazolenga masuala ya ufundi stadi na namna ya kuboresha  ufundi ili kupambana na umsikini.      

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner