MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa CWT kutoa tamko utata wa malipo ya walimu
BOOKMARK THIS PAGE
CWT kutoa tamko utata wa malipo ya walimu  Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 08:44

Gedius Rwiza
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT),kimesema kuwa Jumatatu ijayo kitatoa tamko kuhusu utata unaoendelea katika ulipaji wa madai ya walimu sehemu mbalimbali nchi.

Hatua hiyo ya CWT imekuja baada ya walimu wengi kuilalamikia Serikali kwa kushindwa kuwalipa fedha zao kama walivyohakikiwa jambo ambalo limesababisha baadhi ya walimu kufanya mgomo, ambapo walimu 54 wa Halmashauri ya Rungwe wamefutwa katika orodha ya malipo hayo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Rais wa CWT,Gratian Mukoba alisema kuwa kikao cha Baraza la CWT kilifanyika mwishoni mwa mwezi Januari na kwamba walikuwa wakisubiri kuendelea kukusanya taarifa za ulipaji wa fedha hizo na kwamba hadi sasa kuna malalamiko mengi kutoka halmashauri mbalimbali.

“Ni kweli hali sio nzuri katika mchakato mzima wa ulipaji wa fedha za walimu ambazo Serikali ilikubali kuanza kuzilipa. Tunapokea malalamiko mengi na baadhi ya walimu wanafutwa katika orodha ya malipo wakati Serikali ilituma fedha hizo kulingana na uhakiki ilioufanya, lakini kuna watu wengine wanaojitokeza kuvuruga mchakato huo,”alisema Mukoba.
 

Wakati hayo yakiendelea uongozi wa CWT Manispaa ya Ilala umeilalamikia Serikali kwa kuwapelekea walimu fedha pungufu ikilinganishwa na idadi ya walimu wanaotakiwa kulipwa.

Katibu wa CWT, Manispaa ya Ilala James Manyama alisema kuwa shule za msingi zilitakiwa kupata Sh 193 milioni lakini wamepelekewa Sh120 milioni  ambazo ni za likizo kwa walimu ni 836.

Alisema kuwa kwa upande wa shule za Sekondari Sh61 milioni zimefikishwa kwao badala ya Sh131 jambo alilosema linawapa mtihani mgumu.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #1 2012-02-04 09:11
Mukoba acheni kuwafanya walimu ni sehemu ya kujipatia umaarufu. Nao ni wanadamu hawa siku watakayochoka mtajuta. Wewe huna msimamo hata kidogo kwani mlipotangaza mgomo usitishwe wakati hamjaona malipo mlitarajia nini. Kimsingi mlipaswa kuona malipo yamefanyika ndipo mgomo usitishwe. Sijaelewe elimu yako ila hiyo mbinu haihitaji hata cheti cha form four. Ni wakati tu ndio utaamua kati ya haki na batili. "They will be after you brothers because only the time can determine the reality"
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner