MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Familia 23,000 zafaidika na Pride
BOOKMARK THIS PAGE
Familia 23,000 zafaidika na Pride  Send to a friend
Saturday, 04 February 2012 08:45

Happy Lazaro, Arusha
ZAIDI ya familia 23,000 nchini zimenufaika na mikopo ya fedha, mifugo na zana za kilimo zinazotolewa na shirika   lisilokuwa la Kiserikali la Pride Tanzania lenye makao yake jijini Arusha na kuboresha maisha yao.

Mkurugenzi  Mtendaji wa Pride Tanzania, James Obama alisema hayo  alipokuwa akielezea mafanikio na changamoto za  mpango wa mikopo vijijini tangu uanzishwe mwaka 2007 .

Obama alisema mwaka 2007 Pride Tanzania iliamua kuelekeza nguvu zake kwa wakulima vijijini ili kuwapatia  mikopo hiyo ambayo huilipa wakati wa mavuno kwa nia ya  kuwawezesha kuinua na kuboresha shughuli zao za uzalishaji mali .

Alisema Pride ambayo imekuwa ikijihusisha na utoaji wa fedha kwa wajasiriamali tayari imeshatoa mikopo ya mifugo kupitia vikundi vya wakulima na wafugaji wa Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga ambako Shirika la Pride Tanzania limewapa mikopo  ya ng'ombe wa kisasa na sasa wanazalisha maziwa mengi ambayo wanayauza viwandani.

Alisema Pride Tanzania, mwaka 2007 ilipanua shughuli zake za utoaji mikopo kwa awamu, ambapo awamu nyingine ya mikopo ya zana za kilimo ilianza kutekelezwa mwaka 2009  wilayani Kilolo huko Iringa.

Aliongeza kuwa, baada ya mafanikio kupatikana Pride ilipanua huduma zake  za utoaji mikopo ya zana za kilimo  katika Wilaya za Kilosa, Morogoro vijijini na Mvomero mkoani Morogoro, ambapo wakulima katika wilaya hizo  wamenufaika na  mikopo hiyo.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner