MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa TIC yataka kilimo kimarishwe nchini
BOOKMARK THIS PAGE
TIC yataka kilimo kimarishwe nchini  Send to a friend
Thursday, 02 September 2010 22:12

Sadick Mtulya

MKURUGENZI Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Emmanuel Ole Naiko amesema  kama juhudi za makusudi hazitachukuliwa kuendeleza sekta ya kilimo, ni vigumu uchumi wa  nchi kukua kwa asilimia kati ya nane na kumi kwa mwaka.
 
Aliyasema hayo jana jijini  Dar es Salaam katika maadhimisho ya siku ya wahandisi yanayofanyika kila  mwaka, ambapo mpango wa Kilimo Kwanza ulizungumziwa.

“ Kama juhudi za makusudi hazitachukuliwa  kuendeleza sekta ya kilimo, ni vigumu uchumi wa nchi ukakua kwa asilimia kati ya nane na kumi kwa mwaka,’’ alisema Naiko.

Alisema hali hiyo inatokana  na  zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania  kuwa wakulima.

 “ Kama wakulima wetu hawatapata bei nzuri ya kuuzia mazao, kipato chao kitazidi kushuka  hivyo itakuwa vigumu,  kuondokana na umaskini,” alisema Naiko ambaye pia ni makamu wa rais wa umoja wa vituo vya uwekezaji duniani .
 
Alifafanua kwamba  kilimo cha mashamba makubwa ya biashara kwa kiasi kikubwa ndicho  kitaiwezesha Tanzania na pamoja na nchi za Afrika  kwa ujumla, kushindana na wakulima wa nchi za magharibi ambao wanapata  ruzuku kutoka serikalini.

“Kulingana na hali ya uchumi wetu ulivyo sasa, hatuwezi kumudu kutoa ruzuku kwa wakulima wetu, ili tupiganie kuwepo  katika biashara hasa katika kipindi hiki cha utandawazi, ni lazima tuwe na wakulima wakubwa ili waweze kushinda na wenzao wa nchi nje,’’ alisema.

 Mwaka mmoja sasa umepita tangu kuzinduliwa kwa mpango wa Kilimo Kwanza, ambapo katika  mwaka wa fedha 2010/11, bajeti ya kilimo imepanda kwa asilimia 8.1  na kufikia Sh11.1 trilioni.

 
Bajeti kwa ajili ya kujenga miundombinu ya umwagiliaji imeongezeka kutoka Sh21 bilioni mwaka 2009/10 hadi Sh23 bilioni mwaka 2010/1.1
 
Tayari  hadi sasa serikali imefanikiwa kuongeza eneo linalomwagiliwa kutoka hekta 264,388 mwaka 2005 hadi 331,490 mwaka 2010.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner