
| Benki ya Dunia kuboresha elimu nchi zinazoendelea | Send to a friend |
| Wednesday, 20 April 2011 08:25 |
|
Hadija Jumanne Aidha, benki hiyo imetoa msaada wa dola 750 milioni za Kimarekani kwa nchi zilizo chini ya Jangwa la Sahara barani Afrika na zilizo kusini mwa Asia ili kusaidia nchi ambazo mpaka kufikia mwaka 2015 zitakuwa hazijafikia kiwango cha elimu ya maendeleo ya milenia . Taarifa ya Benki ya Dunia iliyotolewa na Wizara ya Fedha ikimnukuu msemaji mkuu wa Benki hiyo, ilisema katika kipindi cha miaka 50 iliyopita Benki ya Dunia iliwekeza dola 69 bilioni za Marekani katika sekta ya elimu ambayo ni zaidi ya miradi 1500. Mwaka 2010 benki hiyo iliingia mkataba mpya wa zaidi ya dola 5 bilioni za Marekani ili kusaidia kuimarishwa kwa sekta ya fedha. Taarifa hiyo ilisema kuwa sekta binafsi ziliwekeza katika ushirikiano wa fedha wa kimataifa hadi kufikia dola 170 milioni za Marekani. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, ili kuzisaidia nchi kufikia kiwango cha elimu ya maendeleo ya milenia, Benki Kuu itaongeza misaada katika elimu ya awali kiasi cha dola 750 milioni za Marekani ambapo pesa hizo zitasaidia nchi ambazo mpaka kufikia mwaka 2015 zitakuwa hazijafikia kiwango cha elimu ya maendeleo ya milenia hasa kwa nchi kusini mwa Jangwa la Sahara, barani Afrika na zilizo Kusini mwa Asia. Alisema misaada mingine itakayo tolewa na Benki ya Dunia ni pamoja na kuboresha na kurahisisha upatikanaji wa elimu bora kwa watu waliopo ili kukidhi mahitaji kwa wote wanaohitaji huduma hiyo. |















Comments