
| UN yatajwa uhalifu wa mtandao | Send to a friend |
| Friday, 05 August 2011 09:09 |
|
WASHINGTON, Marekani AFP Hiyo ni kutoka na utafiti uliofanywa na kampuni inayojihusisha na masuala ya usalama wa Kompyuta McAfee ambao wamekuwa wakichunguza vitendo hivyo. Kampuni hiyo iligundua zaidi ya wahanga 72, ambao tayari walishaathirika na uhalifu huo kupitia njia hiyo ya mtandao wa internet. Kampuni hiyo ilitaja Mashirika makubwa ukiwemo Umoja wa Mataifa kwa kuwa wakuu wa moja kati ya matukio makubwa kabisa ya uhalifu kupitia katika mtandao wa internet. Pia ilizitaja Serikali za Marekani,Canada, India na Korea Kusini pamoja na mashirika makubwa kama vile kamati ya Kimataifa ya Olimpiki kwamba ni miongoni pia mwa wale waliyokabiliwa na matukio hayo. Kampuni hiyo ya McAfee hata hivyo haikutaja wale ambao inadhani wanahusika na vitendo hivyo vya uhalifu wa mtandao, lakini kuna wasi wasi kuwa huenda China ikawa inahusika. Awali wizi wa mtandao ulitawala sana hususan katika mabenki duniani huku ukisababisha hasara za mabilioni ya pesa. Inasemekana pia wanaotumia wizi wa aina hiyo ni wale wezi wa kimatifa ambao pia wanauwezo mzuri wa kucheza na masuala ya komputa vilivyo. Shirika hilo katika taarifa yake lilisema kuwa kwa hali inavyoonekana baa hilo litaendelea hadi mwisho wa mwaka huu. Aidha Umoja wa Mataifa ulisema idadi ya vifo vya wakimbizi wa kisomalia wanakimbilia Kenya, inazidi kuongezeka. Mikoa hiyo mipya mitatu iliyotajwa na Umoja wa Mataifa kuwa katika hali mbaya huko Somalia ni pamoja na Afgoye, Shabelle ya kati na mji mkuu Mogadishu, ambako wiki iliyopita waasi wa Al Shabaab walipambana na kikosi cha Umoja wa Afrika AMISOM kinachoiunga mkono serikali ya mpito nchini humo. Mkoa wa Afgoye pekee una zaidi ya wasomali laki nne, na hivyo kuufanya kuwa na kambi kubwa kabisa duniani ya watu wasiyo na makaazi pamoja na kuwepo kwa juhudi kubwa zinazofanywa na makundi ya kutoa misaada. Alisema ni nusu tu ya dola billioni mbili zinazohitajika na Umoja wa Mataifa kusaidia hali hiyo ndizo zilizoahidiwa na mataifa wahisani |














