|
Maandamano yavunja mazungumzo ya uchumi Ulaya |
Send to a friend |
|
Monday, 19 September 2011 08:46 |
|
VIROSLAV,Poland WAKATI Mawaziri wa Fedha wa Nchi zinazotumia sarafu ya Euro walipokutana mjini Virostlav ,nchini Poland watu zaidi ya 40,000 wamevamia mazungumzo ya mzozo wa uchumi.
Waandamanaji hao eneo lililokuwa linatumiwa na mawaziri hao wa fedha kwa lengo la kupinga mazungumzo hayo,ambayo yalikuwa yakiongozwa na Rais wa kundi la Mataifa hayo Jean Claude Juncker.
Mawaziri wa Fedha wa Nchi zinazoitumia sarafu ya euro walikutana mjini Virostlav nchini Poland kwa mazungumzo ya siku mbili kuhusu mzozo wa madeni katika nchi zao.
Kutokana na kiasi cha waandamanaji 40,000 wanaopinga hatua za kubana matumizi walikwamisha shughuli katika mji huo hapo juzi.
Mazungumzo hayo yalilazimika kumalizika mapema kutokana na maandamano hayo licha ya kuwa na ulinzi wa kutosha.
Pia katika kikao hicho mawaziri hao wa fedha waliamua kuahirisha uamuzi kuhusu uwezekano wa mkopo wa pili kwa Ugiriki hadi mwezi Oktoba. Rais wa kundi la Mataifa hayo Jean Claude Juncker alisema Umoja wa Ulaya na shirika la fedha la kimatiafa IMF zinahitaji kuona mageuzi yakiendelezwa nchini Ugiriki kabla ya kutolewa awamu nyingine ya mkopo.
Wakati huo huo waziri wa fedha wa Marekani Timothy Geithner ambaye alihudhuria mazungumzo hayo, aliziomba nchi zinazotumia sarafu ya euro kuendeleza mipango itakayoinua uchumi wa nchi hizo badala ya kuangalia sana tatizo la matumizi ya serikali.
Mawaziri hao walipinga vikali matamshi hayo na kuiambia Marekani kutatua matatizo yake. Wakati huo huo waziri wa fedha wa Ujerumani kwa mara nyingine tena alitoa wito wa kutozwa kodi kwa biashara za fedha miongoni mwa nchi 17 zinazotumia sarafu ya euro.
Wolfgang Schauble aliliambia gazeti la kila jumapili nchini Ujerumani la Bild am Sontag kuwa kodi hiyo itapangwa baadaye mwaka huu licha ya upinzani mkali kutoka mataifa kama vile Marekani na Uingereza.
Waziri mwenzake wa Ubelgiji, Didier Reynders alimuunga mkono akisema kuwa kodi hiyo inahitajika kuyatuliza masoko. Waungaji mkono hatua hiyo kama vile nchi za Ujerumani, na Ufaransa zinaamini kuwa kodi hiyo itasitisha ulanguzi,na kusaidia kupatikana fedha zitakazoweza kutumika kutoa mikopo kwa mabenki katika wakati wa mizozo katika siku zinazokuja. Wapinzani wanalalamika kuwa kodi ya aina hiyo itahamishia biashara kwenye masoko ya nchi ambazo hazitozi kodi
|