MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kimataifa Wakenya mbaroni wakituhumiwa kuiba NBC
BOOKMARK THIS PAGE
Wakenya mbaroni wakituhumiwa kuiba NBC  Send to a friend
Tuesday, 08 November 2011 09:30

Hadija Jumanne
WAFANYABIASHARA wawili raia wa Kenya wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala wakikabiliwa na shtaka la wizi wa Sh2.5 milioni katika benki ya NBC.

Washtakiwa hao Pius Kiroko (46) na Edward Kimata(48), wote wanakabiliwa na shtaka hilo wanalodaiwa kutenda Benki ya NBC tawi la Kichwele, Dar es Salaam.

Mwendesha Mashtaka Wakili wa Serikali, Credo Rugaju, alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo Oktoba 31, mwaka huu katika benki hiyo mkabala na mtaa wa Kisutu.

Rugaju alidai siku ya tukio saa 6:40 mchaka, washtakiwa wanadaiwa kuiba Sh2.5 milioni kutoka kwa Hemed Jafary.
Washtakiwa walikana kuhusika na tuhuma hizo, Hakimu Ester Mwakalinga aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 21, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Tuesday, 08 November 2011 17:33
 

Comments 

 
0 #7 2012-04-24 11:17
Sio kutozwa faini ya nusu ya pesa waloiba, ili iwe fundisho kwa wenzao wenye tabia kama yao vifungu vya sharia vifuatwe na kama havina kipengele kinacho-state sharia kali then wawape adhabu m'badala. Mtanzania ukibainika na kosa ili Kenya hususan Nairibi dunia nzima itatambua kuwa mtanzania kaiba Kenya kwa jinsi wanavyojua ku-pablish ila hapa TZ amani na upendo, hatutaki makuu. ndo maana hata kiongozi akigundulika kafanya ubadhirifu atachunguzwa then mambo yataisha hata onyo la mdomo hapewi, aaaaa, TANZANIAAAAAA, ni KISIWA CHA AMANI BWANA, HATUTAKI SHIDA WALA VURUGU.
Quote
 
 
0 #6 2012-03-27 14:16
Quote:
prison them as soon as possible coz are thieves........and they dont add any thing in our country apart from pooresting us.......


I'm still laughing since morning. pooresting! hahahaha dude! prison them!
Quote
 
 
+1 #5 2011-11-23 07:12
Aiseee, kiingereza hiki ni kikali hasa! "Prison" them na "pooresting" Hii kali hasa! Nadhani ulitaka kusema 'jail' them, na pengine ukitaka kueleza kwamba 'they make us poor.' Hata hivyo, taratibu tutafika tu mradi tunakuelewa maana yako ni nini.Quote:
prison them as soon as possible coz are thieves........and they dont add any thing in our country apart from pooresting us.......
Quote
 
 
+1 #4 2011-11-08 17:17
Nawapongeza wafanyakazi wote wa gazeti hili kwa kutia juhudi zenu kwa umoja wenu kutupa habari motomoto za kuelimisha na kujuza wananchi pasipo shaka. Pamoja na kazi nzuri kuna kasoro nimekuwa naziona katika uandishi (typing error) Mfano halisi ni huu mstari wa mwanzo (Heading)ktk habari hii ya Wakenya waliotuhumiwa kuiibia benk ya NBC Heading inasomeka kama mmoja lakini ktk habari ni wawili. Rekebisheni kasoro hizi ili tupate raha na kuburudika zaidi kama si sana. Kila kheri
Quote
 
 
0 #3 2011-11-08 15:50
prison them as soon as possible coz are thieves........and they dont add any thing in our country apart from pooresting us.......
Quote
 
 
0 #2 2011-11-08 12:17
Mbona wa EPA bado wanatamba?
Quote
 
 
0 #1 2011-11-08 10:14
Hao watu naomba sheria ifuate mkondo wake na ikibidi watozwe faini ya nusu waliyoipola
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner