Gakondo wadhamiria kuupa nguvu muziki wa asili

Muktasari:

Katika kuhakikisha wanalinda asili ya nchi yao wasanii nguli  nane wa muziki wa asili nchini Rwanda wameungana na kufanya kazi pamoja kwa lengo la kulinda na kuheshimu kazi yao hiyo.

Katika kuhakikisha wanalinda asili ya nchi yao wasanii nguli  nane wa muziki wa asili nchini Rwanda wameungana na kufanya kazi pamoja kwa lengo la kulinda na kuheshimu kazi yao hiyo.

Wasanii hao wameungana na kujipa jina la ‘Gakondo’ambapo mwanamuziki nguli wa muziki huo nchini humo, Intore Massamba ndiye aliyetoa wazo hilo badala ya kuimba msanii mmoja mmoja.

Kundi hilo lina wasanii mahiri wa muziki huo, Jules Sentore, Daniel Ngarukiye, Michel Ngabo, Manu-teta Kamaliza and Didier Bass-tamfun.

Akizungumza kwenye umoja huo, Massamba alisema kufanya kazi pamoja ni vizuri lakini kwa muziki wa asili ni bora wakafanya pamoja ili kuunusuru muziki huo na kuufanya uwe imara ndani ya jamii.

Alisema wanachofanya kwa sasa baada ya muungano huo ni kuandaa nyimbo ambazo watazirekodi kabla ya kuziingiza sokoni”tunataka kuhakikisha tunaufanya muziki wa asili wa Rwanda uchezwe sehemu mbali mbali Barani Afrika na nje ya Afrika.