Walimbwende watapeliwa kwa jina la Flaviana Matata

Muktasari:

KAMPUNI ya Compass Communications imewatahadharisha warembo  na wanamitindo wote nchini kutorubuniwa na genge la watu wanaotumia jina la Flaviana Matata kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.


KAMPUNI ya Compass Communications imewatahadharisha warembo  na wanamitindo wote nchini kutorubuniwa na genge la watu wanaotumia jina la Flaviana Matata kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Compass Communications, Maria Sarungi Tsehai amesema jana kuwa kuna genge la watu wanaotumia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa facebook ujulikano kwa jina la Flaviana Matata’s na kujipatika fedha kiasi cha sh. 200,000 kwa jila anayejiunga kwa lengo la kutafutiwa kazi au nafasi ya kufanya shughuli za wanamitindo nje ya nchi.

Maria alisema kuwa watu hao huwarubuni wasichana na kuwaahidi kuwatafutia kazi nje ya nchi kwa mgongo wa Flaviana na mmoja wa vijana hao amejitambulisha kama ‘kaka’ yake mwanamitindo huyo, jambo ambalo si la kweli.

Alifafanua kuwa baada ya kukutana na wasichana waliongia katika mtego huo, huwa wanaawalaghai kwa njia mablimbali na baadaye kulipa kiasi hicho cha fedha. Alisema kuwa hali hiyo imewaletea usumbufu wasichana wengi na kujikuta wakihaha kutafuta ukweli baada ya kutapeliwa.

“Compass Communications kama kampuni inayosimamia shughuli za Flaviana Matata inatoa tahadhari kwa umma kuwa Flaviana Matata hahusiki kwa njia yoyote na ukurasa huu au watu hawa.  Pia tunawatahadharisha wananchi kuwa wawe waangalifu kwani Flaviana Matata hayuko katika biashara ya kumtafutia mtu yoyote kazi ya  uanamitindo popote pake,” alisema Maria.

Maria alisema kuwa ukurasa halisi ya Flaviana Matata kwenye mtandaomwa Facebook ni “Flaviana Lavvy Matata” na kwa sasa wanendelea kushirikiana na vyombo husika kwa kutoa taarifa kuhusu uhalifu huo.