MwanzoContactsEmail
Home Biashara Biashara za Kitaifa Serikali yatoa Sh30 bn utafiti wa Sayansi
BOOKMARK THIS PAGE
Serikali yatoa Sh30 bn utafiti wa Sayansi  Send to a friend
Tuesday, 19 April 2011 09:22

Elizabeth Ernest
SERIKALI imetenga Sh30 bilioni kuwezesha wanafunzi wa Teknolijia ya Mawasiliano (ICT), kufanya tafiti mbalimbali za maendeleo ya mawasiliano.

Fedha hizo zimetolewa na Wizara ya Sayansi na Teknolojia na Mawasiliano kupitia mfuko wa Utafiti na Maendeleo ambao utawasaidia wanafunzi wa fani ya ICT .

Akizungumza kwenye wiki ya Maonyesho ya Chuo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (CoICT), kuadhimisha miaka 50 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jana, Naibu Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Charles Kitwanga, alisema wizara yake inahitaji tafiti nyingi zinazohusu mawasiliano.

 “Mimi natoa wito kwenu wanafunzi mchangamkie hizi fedha za utafiti na mkazifanyie kazi ili tuweze kupata wataalamu wengi zaidi kwenye mawasiliano,” alisema.

Kitwanga alisema CoICT, bado ni chuo kipya kina kozi mbalimbali za mawasiliano zitakazosaidia kuhamasisha mawasiliano kwa dunia nzima.

Aliwataka wanafunzi wa chuo hicho kutumia ujuzi wa taaluma yao kujiajiri na kuwaajiri wengine, sio kusubiri kuajiriwa ili kuongeza tija na ufanisi wa kile walichojifunza.
 
Maonyesho ya chuo hicho ni pamoja na machapisho mbalimbali yanayohusu masuala ya umeme, mawasiliano, sayansi ya kompyuta, uhandisi na kituo cha teknolojia ya habari.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #2 2011-04-19 18:24
nyinyi viongozi sio kama mnatoa hela hio kwa ICT only hapa nchini kuna tafiti muhimu sana na zenye faida kubwa kwa taifa lkn bado mpo kimya.Kwa mfano nchi inakabiliwa na majanga mbali mbali ya Climate change and environment ambayo haya yanaleta athari kwa watu wote. ikiwa ni pamoja na mafuriko na ukame wa ambao utasababisha uhaba wa chakula na maji jee huyo Engineer wenu na ujuzi wake ataweza kuishi bila kupata kula au ataishi wapi ikiwa nchi itakubwa na majanga kama Tsunami, Gale force winds, Hurricane and others. Mnatakiwa muangalie wapi muhimu kabla ya kutenda,
Quote
 
 
0 #1 2011-04-19 10:38
Tunajua imetegwa fedha hiyo kuimarisha mawasiliani ya chama tawala CCM ili kushinda tena uchaguzi mwaka 2015.Katika afya na mawasiliano kipi kingetakiwa kitengewe fedha nyingi?. Huu usanii wa CCM utaisha tu. Unatengea Mawasiliano Bilioni 30 wakati wananchi wako afya mbaya.Tunawajua sana!
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner