MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Mrema atua Loliondo kuimarisha afya yake  Send to a friend
Monday, 14 March 2011 08:21

Waandishi Wetu
MWENYEKITI wa TLP, Augustine Mrema, ametinga Loliondo kwa Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT),  Ambilikile Mwasapile kunywa dawa na kutamba ni kwa ajili ya kuongeza nguvu ya mwili kupambana na ufisadi.

Mrema, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), alisema jukumu alilokabidhiwa kuzunguka nchi nzima ni kubwa linalohitaji kuimarisha afya yake.

“Kazi niliyokabidhiwa ni kubwa, kuzunguka nchi nzima kupambana na ufisadi kunahitaji kuimarisha afya yangu,” alisema Mrema na kuongeza:

“Bila kuimarisha afya huwezi kufanya kazi hii niliyokabidhiwa, waeleze Watanzania kuwa nimeimarisha afya sasa nikupambana na mafisadi kwenye halmashauri nchini kwa kwenda mbele.”

Alisema Watanzania wanatakiwa kumshukuru Mungu kwa ‘kuwashushia’ Mchungaji mstaafu Ambilikile Mwasapile (76), kwa sababu hawatumii gharama kubwa zaidi ya 500.

“Kama angekuwa Marekani tungeenda kwa Sh500? dawa yake haina kuchakachua unakunywa. Dawa nimekunywa na nimerudi na picha nimepiga naye ” alisema Mrema kwa kujiamini.

Hata hivyo, Mrema hakubainisha magonjwa yanayomsumbua hadi kwenda kwa Mchungaji Mwasapile, ingawa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu. Siku za hivi karibuni vigogo wengi wa Serikali na CCM wamekuwa wakienda Loliondo kwa ajili ya tiba.

Serikali itegemee maajabu
CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, amesema Serikali itegemee maajabu zaidi ya tiba za asili kuliko ya Loliondo, kwa kuwa wananchi wamechoka na ubabaishaji wa sekta ya afya.Profesa Lipumba alisema hayo juzi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Profesa Lipumba, umati unaoendelea kufurika kwa Mchungaji Mwasapile ni kiashiria kwamba Watanzania wamekata tamaa na huduma za afya zinazotolewa na Serikali.

“Ikiwa Serikali haitajali huduma muhimu za afya kwa wananchi wake, tutarajie mengi zaidi ya haya ya Loliondo,” alisema Lipumba.

Alisema wananchi wakichoka na kukata tamaa na chombo chenye dhamana ya kuwahudumia, watatafuta njia mbadala ya kujikwamua na tatizo kama ilivyokuwa Loliondo.

Profesa Lipumba alieleza kuwa kasi ya watu kwenda kutafuta tiba mbadala kwa mchungaji, inaonyesha kuwa Watanzania wameshakata tamaa na huduma za afya zinazotolewa hospitalini.

"Kimsingi hii ni dalili ya wazi kuwa, sekta ya afya imeshindwa kazi. vinginevyo isingewezekana watu watoroke hospitalini kwenda Loliondo," alisema.

Profesa Lipumba alisisitiza kuwa watu kukimbia tiba za hospitali na kwenda kutafuta tiba mbadala ni aibu kwa taifa hasa kwa sekta ya afya ambayo imeajiri watu na kuwalipa mishahara kwa kazi hiyo.

“Ni kiashirio kibaya sana kwa taifa  kuona watu wakiwa wanatorosha wagonjwa wao hospitalini  kutafuta tiba mbadala," alisema.

Profesa Lipumba aliongoza kuwa umati uliojaa Loliondo unaonyesha picha halisi kuwa, Watanzania wengi ni wagonjwa, lakini sekta ya afya haina uwezo wa kuwahudumia.

Profesa Lipumba ametoa kauli hiyo huku maelfu ya watu yakiendelea kumiminika Loliondo kupata tiba ya mchungaji huyo aliyoeleza kuwa aliigundua kwa njia ya maono.

Ongezeko la watu wanaoelekea Loliondo limezidi hasa baada ya Serikali kubariki tiba hiyo inayotolewa katika  kijiji cha Samunge wilayani Ngorongoro.

Mchungaji, Mwasapila juzi alipongeza uamuzi wa Serikali kuondoa tishio la kuzuia kutoa dawa kwani watu wengi wamekuwa wakinufaika na dawa na mahitaji yanaendelea kuwa makubwa.
 
“Tunamshukuru Waziri William Lukuvi kwa kuruhusu dawa iendelee kutolewa na kutoa ahadi ya kuleta huduma mbalimbali muhimu katika kijiji hiki,” alisema Mchungaji Mwasapile.

Chakula, malazi
Mmoja wa wasaidizi wa mchungaji huyo, Peter Dudui alisema jana kuwa kuanza kupatikana hudumu muhimu katika eneo hilo kama chakula, vyoo na mahala pa kulala kumechangia kupunguza wimbi la vifo vya wagonjwa.
 
“Sasa vifo hakuna, wagonjwa wanaokuja wanapata huduma kama chakula na maji na pia wanapata mahali pa kulala. Ingawa sehemu za kulala ni chache zinasaidia sana,” alisema Dudui.

Ijumaa wiki iliyopita, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi alitangaza kuwa Serikali imeruhusu Mchungaji Mwasapile kuendelea na huduma zake za tiba na kwamba itatoa ushirikiano wa kusimamia na kujenga mazingira mazuri ya kuendelea kutoa huduma.

Tamko hilo lilitolewa wakati ambapo tayari kulikuwepo na tetetsi kwamba Serikali imekusudia kumsimamisha Mchungaji huyo hadi hapo uchunguzi maalumu wa kitaalamu utakapofanywa kwa dawa yake.

Tangazo hilo la Serikali ambalo limetolewa wakati bado wataalamu wa afya wanachunguza dawa hiyo, limehamasisha maelfu kwa maelfu kumiminika kupata tiba.

Msururu mirefu ya magari yanayotoka Arusha mjini kuelekea katika kijiji hicho ambacho sasa kinaiitwa 'Kijiji cha Babu', jana ilionekana katika barabara ya Arusha hadi Ngorongoro.

Walioshuhudia msafara huo mrefu walisema kitu kibaya walichoshuhudia kwenye msafara huo ni madereva walombele kutoruhusu wenzao wanaookuja nyuma yao kwa kasi kutokana na kila mmoja kujaribu kuwahi kufika kabla ya mwingine kunywa dawa.

Baadhi ya watu walioshuhudia misafara hiyo, walisema ni vigumu madereva kuwaruhusu wenzao wanaokuja nyuma kwa hofu ya kuchelewa kwenye foleni ya dawa.

Imeandikwa na Midraji Ibrahim, Hussein Issa na Elizabeth Ernest


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Tuesday, 15 March 2011 08:34
 

Comments 

 
0 #49 2011-03-16 13:51
Jamani mimi naona hamna kazi ya kufanya wewe unayekatisha watu tamaa ya kwenda kunywa dawa kwani umelazimishwa wewe uende acha watu wenye matatizo yao waende kwa babu wewe haikuhusu na wala hulazimishwi kwenda kwa babu, isitoshe hapo ulipo una magonjwa zaidi ya 5 ipo siku na wewe utapanda bus mwenyewe na kwenda huko kwa babu bila hata ya kuwaambia ndugu zako.
Quote
 
 
0 #48 2011-03-15 10:02
nachoka! kwa nini la babu wa loliondo limekuwa gumzo? mbona miujiza toka kwa mzee wa upako, kakobe na wengineo haizungumzwi. mimi naona hapa ni kwamba Mungu anajidhihirisha kwamba anaweza hata yale ambayo katika hali ya ubinadamu ni magumu. pia Mungu haonekani kwa wenye "title" kubwa kubwa tu bali hata kwa wasio na title yupo kwa sababu yeye ni wa wote wenye mwili na haangalii umaarufu wa mtu wala fedha. hata YESU alizaliwa katika hali duni ya umasikini katika mji mdogo wa nazareth! leo la babu wa loliondo kwa nini iwe shida.
Quote
 
 
0 #47 2011-03-15 09:51
Quoting Yahya Msangi:
Ngoja atakapotokea mganga wa Kanisa Katoliki, Morovian Church, Anglican, Jamii Islamiya, Budha, n.k. nao wadai wameoteshwa ndio tutajua u[NENO BAYA] si mpaka uache kwenda shule!



cha kushangaza wewe unayeendekeza udini, hata wenzako wa dini yako wamejaa loliondo. cha msingi ni kwamba kama hujapata ugonjwa unaokusumbua, waache wanaokwenda loliondo kunywa dawa waendelee kwenda. sidhani kama mtu aliyesumbuka miaka 20 kwa ugonjwa wowote akipata tiba ataangalia hayo unayosema wewe. HERI YA WEWE MWENYE AFYA NJEMA.
Quote
 
 
+1 #46 2011-03-15 09:33
Muache Mungu aitwe Mungu jina lake limidiwe ufalme wake umefika Loliondo,kila anaye amini atapona.
Quote
 
 
+1 #45 2011-03-15 08:32
KUNA WAHESHIMIWA MAWAZIRI WENGI PAMOJA NA MAOFISA WAO BILA KUSAHAU FAMILIAZAO, AFYA ZAO ZINAMIGOGORO, BADALA YA KUPOTEZA FEDHA ZA SERIKALI BURE KWA KUKIMBILIA KWENDA KUTIBIWA NJE YA NCHI WANATAKIWA WAWAHI LOLIONDO.
Quote
 
 
0 #44 2011-03-15 05:59
Quoting albert:
Nashangaa na yule anayesema anakatisha huduma inayotolewa na huyo mtumshi wa mungu kwani hajalazimisha mtu yo yote kwenda kunywa dawa ni hiyri yako na imani yako,babu hana cha kuangalia cha dini wala ukabila wewe kama una mambo yako achana na mtumishi wa wa mungu.Viongozi wote tunawaomba pia mjaribu kufuata utaratibu wa kwenda kupanga line kama wagonjwa wengine,hata kama wewe ni nani,kila mmoja na shida zake siyo kwa kuwa wewe ni mbunge ama waziri eti ukapate watu wengine wamekaa siku tano wewe umeenda ukaanza ile mambo yenu ya kuchakachua.Pale hakuna cha rais wala mbunge ama awe nani,kazi kama ukienda pale usije ukajaribu kuchakachua ukitumia uongozi wako,wengine wanaona aibu kukaa kwenye foleni,ugonjwa ni wako hata kama wewe ni kiongozi wa nchi usiogope kama ni tiba unahitaji na mambo yatakuwa boa unaona aibu nani?Hata mimi nataka kwenda kumwona huyo mtumishi wa mungu ikapte kikombe cha shiling ya tsh500 tu,huoni huyo mtumishi hana tamaa ya pesa?Naona kati ya wale baadhi ya wale waliotaka kumkatiza ni watu wa kutaka kitu kidogo kutoka kwa babu,ama alipie [TRA]HAWAJUI YULE NI MTUMISHI WA KWELI NA VILE AMEAGIZIWA NA MUNGU WAKE HATAKI UTAJIRI NI YEYE NA MAAGIZO YAKE KUTOKA KWA MUNGU.Ndugu ujue kila kitu mungu ndiye anapanga na kumchagua atakayetoa huduma ya tiba, wewe unayetaka ifanyiwe utafiti toka mwanzo ulikuwa wapi?Mh Mrema ameshapongeza huduma inayotolewa na babu,pamoja na viongozi wengine wengi ingali hawataki wajulikane, ila mabo yao yalikuwa mabaya sana sasa hivi wanasema kila kitu ni BOA mambo yote ni shwari.Na kama ni watu kufa ungekuta ni mamilioni ya watu wamekufa.loliondo loliondo loliondo ni mambo yote.USIPOTESE WAKATI WAKO HATA USIFICHE UGONJWA WAKO UKAPATE KIKOMBE CHA MIA TANO TU NA MAISHA YAKO YANARUDI KUWA FRESH.


Albert, una uhakika gani kuwa kaoteshwa na Mungu? au kwa sababua alikuwa Askofu ndo unaamini tu alichosema. Subiri matokeo. Dawa ya weza kuponya si kwa sababu kaoteshwa na Mungu, ni kwa sababu ya nguvu ya mti bwana. Hata wewe ukienda kuchimba utapona baba. Km hujajua tabia ya waganga wa mitishamba ndo hii. Lazima akupe masharti magumu. Sasa asipofanya hivi atawapata wapi wateja wakati miti iko porini? Babu yangu katibu sana watu tena magonjwa magumu kama bandama na ini. Lakini baadhi ya mashart unaona ni katika kuhakikisha watu wanakuja kwake tu. Sasa hayupo nasi twaendelea kunywa na tunapona bwana.

Babu mjanja- kapitia Mungu wa Kanisa. Sasa nani atakuwa na shaka? Sioni tafauti ya Babu na Fatma wa Singida enzi hizo za uhai wake. DAWA MOJA MAGONJWA YOTE
Quote
 
 
0 #43 2011-03-15 03:55
MBONA MNA HANGAIKA KWANI NI KIPI CHA AJABU HAYA NDIO MAAJABU YENYEWE MNATAKA MAAJABU KAMA YA OSAMA BIN LADDEN AU? MUNGU MWACHENI AITWE MUNGU KWANI HATA ANGEKUWA MGANGA WA KINYEJI ANATAEGEMEA NINI? YOTE YA HAYA YAKO CHINI YA MBINGU KWA HIYO MASWALI MENGI NI KUAMINI MUNGU HAWEZI SHETANI AKAKUPA NGUVU ZA KUPONYA WATU KIASI HICHO HATA UKIOMBEWA UNAPONA KWA NGUVU ZA MUNGU MSISHANGAE BWANA HAYA MAMBO YAPO TANGU ENZI ZA ADAMU NA HAWA YESU KWA UWEZO WA MUNGU ALIPONYA VIPOFU JE ALIKUWA VIPI? PIA WALIKUWEPO WATU KAMA HUYU LEO ASIYEAMINI HABARI NDO HIYO.
NA BADO YATAKUJA MENGINE MAKUBWA KULIKO HILI SIJUI MTASEMA NINI,HAPA NI KUMSHUKURU MUNGU ANGALIA TIBA YA 500 ULIONA WAPI 300 KATIKA KAZI YA MUNGU KANISANI 100,WASIDIZI WAKE,100 YA KWAKE HAINA GHALAMA NDO MAANA MUNGU AMEMPA UNGEKUWA WEWE NA MIMI UNGEHISI UTAJILI ALFU UNGEONEKANA TAPELI KWA MUDA MFUPI UNGERUDISHA PESA ZA WATU ACHA BWANA
Quote
 
 
-3 #42 2011-03-14 23:55
Quoting MWL. SEMPOLI:
BADO AKILI YANGU HAIJAKUBALI KAMA KINACHOFANYWA NA HUYU BABU KINAHUSIANA NA MUNGU ANAYETAJWA KATIKA BIBLIA,NIMEBOBE A KATIKA KUSOMA BIBLIA LAKINI BADO SIJASHAWISHIKA KUAMINI HILI LA KUOTESHWA NA MUNGU KWAMBA MTI FULANI UNA DAWA,HAKUNA KITU KAMA HICHO KATIKA BIBLIA,HAO MAASKOFU WAKE PIA WAMEPOTOKA LABDA KAMA WANA BIBLIA YAO TOFAUTI,HUYU MZEE KAMA ANAFANYA HUDUMA YAKE ASITAJE HABARI ZA MUNGU,ASEME TU YEYE NI MGANGA NAFIKIRI ATAELEWEKA ZAIDI KWA WASOMI WA BIBLIA,LABDA ALIOGOPA KUTAJA KWAMBA YEYE NI MGANGA MAANA DINI YAKE HAIMRUHUSU!NA IKIONEKANA ASKOFU AMEKWENDA KWA MGANGA ITAKUWA FEDHEHA! NO NINYI MAASKOFU TAYARI MMEKWISHLITUKAN A JINA LA BWANA,MNAHITAJI TOBA.


Wewe nenda zako kwa maji marefu hakuna anae kukataza. Elimu yako ya biblia uliyo nayo ni ya kwa maji marefu na Yahaya wako mkatabiriane huko. Hata kama utaliamini lile dafrtari lenu hakuna wakukuuliza. Usimbue watu saa hizi. Imani yako ndio itakayokuponya.
Quote
 
 
0 #41 2011-03-14 23:45
hakika ya Prof Lipumba yana ukweli ndani yake kwani seriali bila kuwa makini itajikuta hata wale waliotakiwa kufanyiwa operation nao wakatoroka na kwenda kwa Babu.Lakini pia ni dalili ya tiba za mahosipitali yetu kuwa duni na kutokuwa na uhakika. Hakika lipumba umenena kwa hili lakini
Quote
 
 
-1 #40 2011-03-14 23:28
BADO AKILI YANGU HAIJAKUBALI KAMA KINACHOFANYWA NA HUYU BABU KINAHUSIANA NA MUNGU ANAYETAJWA KATIKA BIBLIA,NIMEBOBE A KATIKA KUSOMA BIBLIA LAKINI BADO SIJASHAWISHIKA KUAMINI HILI LA KUOTESHWA NA MUNGU KWAMBA MTI FULANI UNA DAWA,HAKUNA KITU KAMA HICHO KATIKA BIBLIA,HAO MAASKOFU WAKE PIA WAMEPOTOKA LABDA KAMA WANA BIBLIA YAO TOFAUTI,HUYU MZEE KAMA ANAFANYA HUDUMA YAKE ASITAJE HABARI ZA MUNGU,ASEME TU YEYE NI MGANGA NAFIKIRI ATAELEWEKA ZAIDI KWA WASOMI WA BIBLIA,LABDA ALIOGOPA KUTAJA KWAMBA YEYE NI MGANGA MAANA DINI YAKE HAIMRUHUSU!NA IKIONEKANA ASKOFU AMEKWENDA KWA MGANGA ITAKUWA FEDHEHA! NO NINYI MAASKOFU TAYARI MMEKWISHLITUKAN A JINA LA BWANA,MNAHITAJI TOBA.
Quote
 
 
+3 #39 2011-03-14 23:00
Hebu jambo lisilowahusu lisiwaume jaribu kuweni wastaaraabu imani yako ndiyo itakuponya.
Quote
 
 
-3 #38 2011-03-14 19:32
Hivi ccm na babu wapi kwa wapi. nchi imejaa wa[NENO BAYA] na wavivu wa kufikiri
Quote
 
 
0 #37 2011-03-14 17:56
Wakubwa hata Rais wa Gambia amedai anatibu.ukimwi kwa zaidi ya miaka minne.
Quote
 
 
0 #36 2011-03-14 16:54
mungu hafanyiwi mchezo ndugu yangu,ni aibu kuingiza siasa kwenye huduma ya mungu,biblia imesema ata yesu alipotua tu graundin wapo waliozani anakuja kufanya mapinduzi ya selikali zao za kifalme, lakini alikuja kwa wenye shida ya utukufu wa mungu na ndio hao wanao enda kufuata huduma kwa babu,we jiulize kwann watu wasiende kwa kakobe,lusekelo ,rwakatale, na wengineo ama kwa nn wasiende kwa ndodi mzee wa laki laki ama milion au unazani watu hawana hizo hela.jiangalie mwana achana na mambo yako ya ccm,
Quote
 
 
-3 #35 2011-03-14 16:50
Quoting smartboy:
Quoting Pius:
Hongera Mrema kwa kusema ukweli. Cuf kupitia Lipumba acheni longolongo zisizokuwa na maendeleo kama mmeishiwa cha kuongea bora mkakaa kimya. Acheni kutafutia umaarufu kwenye vitu visivyohitaji siasa. Sasa tiba ya Loliondo inahusika vipi na wananchi kuchoka na huduma za afya zitolewazo na serikali? Hivi pamoja na uprofesa ulionao umewahi kuona kuna hospitali kokote duniani inayotoa tiba ya kudumu ya kisukali au ukimwi? Acha longolongo zako.


Hahaha! Kaka Pius, ingekuwa Ulaya watu wangetoa wagonjwa hospitali kuwapeleka kwa babu?
Hii ni dalili tosha kuwa hakuna matumanini ndani ya hospitali zetu. Hakuna uhakikika kila anayekunya dawa ya Babu atapona ndugu yangu.. ni suala la muda na wakati ukweli utajulikana. Mbona wengi waganga km babu waliotamba na wengine pia wanatamba kuponya magonjwa sugu, lakini kadri muda unavyosogea watu wanajifunza kuwa hakuna dawa ni ubabaishaji tu. Huyu babu ni mganga wa mitishamba km walivyo wengine. Tofauti yake ni kuwa KAWATEKA WATU AKILI KWA KUDAI ETI KAOTESHWA NA MUNGU.

KWA TAARIFA YAKO/YENU KILA MGANGA WA MITIHAMBA HUNASIBISHA TIBAYA KE NA MUNGU. ILA BABU WA NGORONGORO KAWAPIKU WENZAKE KWA KUWA KAPITIA MUNGU WA KANISA AMBAO NI RAHISI SANA WATU KUAMINI BILA HATA KUFANYA UCHUNGUZI WALA KUPATA MATOKEO.
Huu ni usanii "eti Dawa Moja Magonjwa Yote"!!!!

kwani si wapo walio tibiwa na wamepimwa hawana tena vvu? au we kuamini unataka ufanyiwe nini ndo uamini? ila hulazimishwi coz kama huamini hulazimishwi kuamini ni bora ukae kimya ndugu yangu... kinacho kufanya usiamini najua ni kwasababu wewe imani yako sio sawa na ya babau yani wewe sio mkriso ndo maana ila nakuhakikishia utakuja kunywa hii dawa pamoja na kuto kuamini kwako
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner