
| Mkama, Kinana watajwa kubeba jahazi la CCM | Send to a friend |
| Sunday, 10 April 2011 23:51 |
|
Taarifa kutoka ndani ya kikao cha Halmashauri Kuu jana usiku mjini hapa zilidai kuwa Wilson Mkama ndiye aliyepewa jukumu la Ukatibu Mkuu wa CCM huku msaidizi wake kwa upande wa Bara akitajwa kuwa ni Abdulrahman Kinana, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, Katibu wa Fedha na Uchumi, Zakia Meghji na Katibu wa Oganaizesheni, Dk Rehema Nchimbi. Kuhusu Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, inadaiwa kuwa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete aliwasilisha jina la Saleh Ramadhan Feruzi, lakini lilikataliwa na wajumbe kutoka visiwani. Sekretarieti iliyojiuzulu ilikuwa inaundwa na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, Naibu Makatibu Wakuu bara na visiwani; George Mkuchika na Feruzi, Katibu wa Itikadi na Uenezi, John Chiligati, Katibu wa Fedha na Uchumi, Amos Makala,Katibu wa Oganaizesheni, Kidawa Saleh na Mambo ya Nje, Bernard Membe. Mkama akishirikiana na Profesa aliyefahamika kwa jina moja la Luhanjo, ndiyo waliofanya tathmini ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na kupendekeza kwamba lazima baadhi ya wanachama watoswe kuokoa chama hicho. Inadaiwa kwamba kujiuzulu kwa Kamati Kuu kulitokana na mvutano wa wajumbe ambao walionyesha kugawanyika, huku kundi moja likitaka Mbunge wa Igunga na Mjumbe wa CC, Rostam Aziz, Mbunge wa Bariadi Mashariki na mjumbe wa kamati hiyo, Andrew Chenge wajiuzulu na jingine likipinga. Baada ya mvutano mkali wa wajumbe hao na kuchukua muda mrefu, inadaiwa Rais Kikwete aliilazimisha kamati nzima kujiuzulu.Awali, ilidaiwa kuwa ajenda hiyo ya kuwataka wajumbe hao wawili wajiuzulu ingewasilishwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu, huku kundi linalodaiwa kupinga ufisadi likitaka wafukuzwe uanachama. “Tunaomba waandishi msituzibe tunataka kuwaona viongozi wetu, maana leo siyo sura tulizozoea wamejivua gamba,” walisikika wafanyakazi hao wakati Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete alipokuwa akiingia kufungua mkutano wa Halmashauri Kuu.Tofauti na kawaida yake ya misemo na uchekeshaji, sura ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba ilionekana ya upole wakati akimkaribisha Rais Kikwete. |
| Last Updated on Tuesday, 12 April 2011 07:38 |



Midraji Ibrahim, Dodoma











Comments
wewe unayejiita beano fingerprints hapa zinaonesha kuwa mtu yeyete akitoa maoni yanayopinga chadema unayapinga ukitumia majina tofauti. Je wewe unapata ni envelopmentaljo nalist (umepata bahasha) au developmental jonalistst?
Tunakuchora tu haha.
sasa zito wa kwenu ccm mmemtuma, tumemsthukia mnaanza bifu....tulia wewe tumenye gamba kilainiiiiiii....
wewe irene wanakulaumu bure binti yangu CHAKUPEWA. Wasamehe hawa hawajui kula yako unaipata kwenye upambe wa CCM hasa unapovaa kibwebwe kukatika ktk gari la wazi wkt wa kampeni kwa ujira wa t-shirt, kofia na kanga bila kusahau buku 2 na chupa ya maji uhai. Kwa ulivyo [NENO BAYA] unajiona mmoja kati ya wanaokula mema ya nchi na ndio maana unatetea ulichonacho poor you!! Ungekuwa na akili ningekusema sana kwa kosa la kutokuzitumia lkn kwa hali ilivyo juu ya nini nikulaumu mkataviuno wa chama usiejua haki zako? Ila kumbuka kuna umri utafikia dada yangu irene hutaweza tena kukatika na chama hakitoi pensheni kwa vilaza wa aina yako. Itafute elimu dada yetu irene ili ubongo wako uendane na jina lako zuri japo sura yako mbaya
bora umwambie anakurupuka tuu na kuongea utumbo
FOR SURE MAN U'R VERY OK NOTHING TO EXPECTFROM THESE NEW TOP LEADERS BUT THEY WILL CONTINUE DOING COMEDIAN ISSUES AS MAKAMBA USED TO DO WITH HIS ASOCIATE TOP LEADERS
Yetu macho!!!