MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Wabunge 143 hawachaguliki uchaguzi 2010  Send to a friend
Tuesday, 27 April 2010 23:32

Said Powa

WABUNGE 143 kati ya 232 wanaotoka katika majimbo ya uchaguzi hawachaguliki, hivyo ni vigumu kurejea bungeni baada ya uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu, kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Mpango wa Utafiti na Elimu ya Demokrasia Tanzania (Redet).

Utafiti wa taasisi hiyo iliyo chini ya Idara ya Sayansi ya Siasa ya Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam unaonyesha asilimia 61.7 ya wabunge wa bunge la sasa hawatachaguliwa tena.

Wakijibu swali lililoulizwa katika utafiti huo kuhusu uchaguzi mkuu ujao kama watachagua mbunge wao aliyepo sasa, asilimia 39.3 ya wananchi ndio waliosema watachagua mbunge wa sasa, wakati asilimia 61.7 ya wote waliyohojiwa walisema hawatamchagua mbunge wa sasa.

Utafiti huo ambao ulifanywa kwa ajili ya kutafuta maoni ya wananchi kuhusu uchaguzi mkuu ujao, ulishirkisha wilaya 52 na kuhoji watu 2600 ikiwa ni watu 50 kutoka kila wilaya.

Akisoma matokeo ya utafiti huo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Dk Bernadeta Killian alisema kuwa waliyohojiwa pia walikuwa na maoni tofauti.

Alisema asilimia 38.3 walisema watachagua mgombea mwingine wa chama chake, asilimia 8.7walisema watachagua mgombea wa chama kingine, asilimia12.4 walisema hawajaamua bado na asilimia 2.9 walitoa majibu mengine tofauti.

Kutokana na hali hiyo, mtafiti huyo wa Redet alisema kuwa karibu asilimia 62 ya wabunge wa sasa hawatachaguliwa tena majimboni mwao.

Utafiti huo pia unaonyesha kuwa Rais Kikwete na  chama chake cha CCM wanaendelea kushika nafasi ya juu kutokana na maoni ya wananchi hivyo kuashiria kuwa CCM itarejesha wabunge wengi na mgombea huyo wa urais atashinda kwa kishindo.

Kwa mujibu wa utafiti huo, waliohojiwa walitakiwa kutoa maoni yao katika swali lililoulizwa kuwa mwezi Oktoba mwaka huu utafanyika Uchaguzi Mkuu, "kama uchaguzi huo ungefanyika leo wewe ungemchagua mgombea wa chama gani?"

Asilimia 77.2  (1997) ya waliohojiwa walisema watamchagua mgombea wa urais wa CCM, asilimia 9.2 (237) ikisema itamchagua mgombea wa CUF, asilimia 4.2  (109) mgombea wa Chadema, wakati asilimia 8.7 walisema bado hawajaamua ni mgombea wa chama gani watampigia kura.

Kwa upande wa wabunge, inaonyesha CCM itapata upinzani mkali katika baadhi ya maeneo kwa kuwa utafiti huo unaonyesha asilimia kushuka ikilinganishwa na ya urais. Asilimia 68 ya waliohojiwa walisema watachagua mgombea ubunge wa chama hicho.

Asilimia 10.2 watachagua mgombea CUF na asilimia 8.6 watachagua mgombea wa Chadema wakati vyama vingine vikitajwa kwa idadi ndogo sana na matokeo hayo yamekuwa yakijirudia kwa asilimia hizo hata kwa madiwani.

Kuhusu uchaguzi wa urais, wahojiwa walitakiwa kumtaja mtu mmoja ambaye wangependa awe rais. Rais wa sasa, Jakaya Mrisho Kikwete ameendelea kuwabwanga wengine waliotajwa kwa kujikusanyia asilimia 66.9.

Kikwete amefuatiwa kwa mbali na Profesa Ibrahim Lipumba wa CUF aliyepata asilimia 6.7, Freeman Mbowe (3.1) na Dk. Asha Rose Migiro asilimia 0.7.

Wengine ni Salim Ahmed Salim asilimia 0.7, Dk Willibrod Slaa asilimia 0.6, Zitto Kabwe asilimia 0.6, Seif Sharrif Hamad asilimia 0.5, Dk. Ghalib Bilali asilimia 0.5 na Balozi Ali Karume 0.3.

Aidha, utafiti huo ulihoji kuhusu utendaji kazi wa Rais Kikwete katika kipindi cha miaka mitano na kuonyesha kuwa asilimia 49 ya waliyohojiwa wanaridhishwa sana na utendaji wake, asilimia 36.5 wanaridhishwa kiasi wakati wasioridhika kabisa ni asilimia 13.1 na wasiojua kitu kuhusu suala hilo ni asilimia 1.1

Takwimu hizi zikilinganishwa na tafiti zilizopita za Redet inaonekana kiwango cha kuridhika na utendaji kazi wa Rais Kikwete miongoni mwa wananchi kimeanza kupanda. Oktoba 2009 ilikuwa asilimia 67.4, Oktoba 2007 ilikuwa asilimia 44.4, Novemba 2008 ilikuwa asilimia 39.5 na Machi 2010 ilikuwa asilimia 49.3.

Kuhusu imani ya wananchi kuhusu utendaji kazi wa viongozi na serikali, utafiti huo unaonyesha kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewabwaga viongozi wengine akiwemo Rais Kikwete.

Kwa mijibu wa utafiti huo, Pinda anaongoza kwa asilimia 61.2 , akifuatiwa na Rais Kikwete mwenye asilimia 58.8 (1528).

Wengine ni Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein aliyepata asilimia 46.8, mawaziri (25.7) madiwani (44.5) na wabunge ni 38.7 .

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Thursday, 29 April 2010 13:14
 

Comments 

 
0 #43 2010-04-30 21:04
THE ISSUE IS TO GIVE COMMENTS ON REDET AND NOT MWEMA'S SUGGESTIONS THE MATTER IS NOT JUST WRITING BUT KNOWING WHAT YOUR WRITING THANKS SEE YOU "MADAM"
Quote
 
 
0 #42 2010-04-29 12:28
Inatia huruma kuongea yote lakini kwa kuwashauri tu, jaribuni kuweka mbali uhalisia wa maisha ya watu na hizo siasa zenu uchwara.Udokta wa kubambikizana usiwe chanzo cha kuwamaliza watanzania kimwili lakini pia kiroho.
Quote
 
 
0 #41 2010-04-29 12:27
vyeo vyenu hivyo vya kubambikizana, ni hatari sana kwa taifa letu.mmeanza kuua chuo kikuu kilichokuwa na heshima kitaifa na kimataifa chuo kikuu cha Dar es salaam, na sasa mnaelekea kuanza kuangamiza akili za watanzania. usomi wenu una mashaka sana kwani , research mlioifanya ni uongo, mmepika data kwa manufaa yenu na maswahiba wenu au mmehoji wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM?.Ni nani asiyejua kuanguka kwa hali ya uchumi wa wa Tanzania?, ni kiziwi ama kipofu gani asiyefahamu uswahiba unavyoitafuna hii nchi?. Tunatambua nyie nyote ni matunda ya uswahiba huo usio na tija kwa taifa letu wa kupewa vyeo hat kama hamna sifa, lakini kaeni mkijua kamwe hamtaweza kupumbaza akili za watanzania wote kama mlivyofanikisha kuua chuo chetu tukufu cha Dar es salaam.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Quote
 
 
0 #40 2010-04-29 12:23
Utafiti wa REDET ukifanyika vizuri zaidi majibu yake yanawezakuwaele keza wengi kumpigia kura yule aliyeshapimwa na wengi na kuonekana ni bora zaidi. Itatupunguzia influence ya wale wanaompigia huyu kwa sababu tu ya ni mwenzao ingawa sifa hana na wale wanopiga kura bila kuelewa vizuri tofauti za wanaopigiwa katika vigezo vya kupima kiongozi bora.
Quote
 
 
+1 #39 2010-04-29 12:10
KAZI INAYOFANYWA NA REDET IKIBORESHWA ITAWEZA KUCHANGIA KUIMARISHA DEMOKRASIA NA UCHAGUZI WA VIONGOZI BORA KATIKA TAIFA LETU. WAFANYE TAFITI KULINGANISHA UBORA WA VYAMA NA VIONGOZI WAKE WATARAJIWA KWENYE CHAGUZI ZIJAZO KUENDANA NA VIGEZO MBALIMBALI AMBAVYO NI MUHIMU KATIKA KUPIMA SIFA YA UONGOZI BORA. TUAMBIENI NA KIONGOZI WAKE HUYU AMEPATA ...% KWENYE KIGEZO HIKI, ..... NA ...% KWENYE KIGEZO HIKI.
MAJIBU KAMA HAYO YATAKUWA YANAMWELIMISHA MPIGA KURA ILI AWEZE KUTUMIA VIZURI ZAIDI FURSA YAKE KATIKA KUCHAGUA KIONGOZI BORA NA NIKUIMARISHA DEMOKRASIA HAPA TANZANIA.REDET ISHIRIKISHE WATAALAMU WENGI ZAIDI KATOKA FANI MBALI MBALI NA WAPEWE UWEZO ZAIDI WA KUWAWEZESHA KUBORESHA TAFITI ZAO ILI ZITO MAJIBU YANAYOONYESHA VIONGOZI WATARAJIWA WANAVYOTOFAU[NE NO BAYA] KATIKA VIGEZO MUHIMU VYA KIONGOZI BORA.

MAJIBU WALIOTOA HAPA HATUSAIDII KATIKA HILO.
Quote
 
 
+1 #38 2010-04-29 11:50
[quote name="MWEMA Boy'
Pamoja na kusomeshwa shule ya English medium bado hujui English! Grammer hiyo PTU! andika kiswahili tu ijulikane moja! Bird Brains!
Quote
 
 
+1 #37 2010-04-29 11:26
REDET FANYENI TAFITI ZA MAANA: TUPENI MAJIBU YAFUATAYO.
KADRI SIKU ZINAVYOKWENDA:
1. Demokrasia inaimarika au inapungua;
2. Ubora wa maisha unaongezeka au
unapungua
3. Ubadhirifi na uizi wa mali za uma
unaongezeka au unapungua
4. Ubora wa viongozi wa kisiasa na
kiserikali unaongezeka au unapungua
Kwenye mazingira tuliyo nayo kwa sasa ambapo kuna demokrasia ya chama kimoja tawala kinachosindikiz wa na utitiri mkubwa wa vyama vidogovidogo visivyokuwa na uwezo, kuruhusu mgombea binafsi kungeimarasha demokrasia au hapana.
Quote
 
 
0 #36 2010-04-29 10:54
REDET MMEKOSA KAZI. UTASHINDANISHAJ E TIMU ZA VIJANA CHEKESHEA NA SEKONDARY KATIKA MPIRA WA SOKA. UPINZANI KWETU HAKUNA, WAKO CCM PEKE YAKE....NI CHAMA KIKUBWA, KILIWAHI KUWA NA UONGOZI BORA NA MUADILIFU LAKINI SASA KINAONGOZWA NA WASIOKUWA NA UWEZO, MWELEKEO NA NIA NJEMA KWA TAIFA HILI...WABINAFSI.REDET TUAMBIE NI YUPI SASA ATAKAYETUFAA HUKO CCM. TUNATAKA MABADILIKO HATUWEZI KUENDELEA KAMA ILIVYO SASA...TUNATAKA KIONGOZI BORA ...ENOUGH IS ENOUGH
Quote
 
 
0 #35 2010-04-29 09:44
ccm mmefulia,hamtaw eza kushinda uchaguzi unaofuata tena,miakla ya nyuma kazi yenu ilikuwa kuiba kura ili mshinde,mwaka huu ulinzi utakuwa imara sana na hamna tena nafasi ya kuiba kura kama mlivyozoea siku za nyuma.
Quote
 
 
-2 #34 2010-04-28 21:35
TUNAWAPONGEZENI REDET KWA KAZI NZURI NA YENYE KUJIUZA. NO ONE WILL AGREE THE TRUE BUT ONLY WHO KNOWS ITS IMPORTANT,WELL THE RESULT PREDICT WHAT WILL HAPPEN AND NOT WHAT WAS HAPPENED OR WHAT IS HAPPENING,SO WHY YOUR BLAMING BE PATIENT YOU TANZANIAN.MY ADVISE TO REDET AND OTHER RESEARCH INSTITUTION IS THAT THEY SHOULD USE A PRESENTABLE SAMPLE SO AS TO AVOID BIAS, BUT ALSO THEY SHOULD BUILD A HABIT OF SEARCHING IMPORTANT THINGS THAT DIRECT AFFECT THE SOCIETY AND NOT ONLY THIS ISSUE.WHY CAN'T THEY SEARCH ON IMPACT OF COMING TUCTA BOYCOTT OR THE ON GOING LECTURERS STRIKE AND ASSES WHOSE BURDEN IS THIS WHO GETS EFFECTS OR WHY ROAD ACCIDENTS HAPPENS NOW AND THEN,WHY WE ARE NOT SERIOUS WE TANZANIAN, WHY CAN'T SAY OF THE BIASED DEVELOPMENTAL ACTIVITIES THAT HAPPENS ON ONE SIDE OF THE COUNTRY,OR WHY CANT WE USE THOSE FUND TO GET MORE DETAIL ON THE DANGEROUS DISEASE.PLEASE USE OUR RESOURCES FOR DEVELOPMENT AND NOT OTHERWISE 'THANKS FROM HIDDEN HEAVEN'
Quote
 
 
0 #33 2010-04-28 20:39
kila mtu anapiga mkwala sijui sheikh yahya atatoka na lipi safari hii au atayesimama kugombea kiti cha urais ataota manyoya?

nawapongeza mwananchi kwa website yenu mpya na hasa ktk ukurasa huu wa maoni sasa hivi upo fair maana nilishaanza kupoteza imani na nyie, maoni yalikuwa yanawekwa ya baadhi ya watu wanaojulikana utakuta mtu mmoja kurasa moja maoni 5 wengine kapuni,mimi nilishaacha kutuma maoni kwenu kama nilivyokoma kwenye blogu fulani.TUNAWAAMINI KAZI NJEMA!
Quote
 
 
+1 #32 2010-04-28 20:21
chaguzi ndogo za majimbo ya kiteto,busanda, biharamulo,tari me,mbeya zilitupa majibu ya octoba 2010 japokuwa chama cha masela kinajua kiliyoyatenda, mpk mnafikia hatua ya kununua shahada na bado haikutosha kushinda mkaficha kura/kuiba kura kila mnapokwenda mnazomewa hawawataki tena hiyo ni vijijini ambapo ndiyo ngome kuu yenu!lol watawala subirini mje mjini sasa. Uchaguzi ukienda haki nadhani itakuwa ni kinyume na utafiti wa chama
Quote
 
 
+3 #31 2010-04-28 17:53
Quoting mpashe:
Pamoja na takwimu hizo, ambazo kwa kiasi kikubwa hazikidhi uhalisia wa hali ya kisiasa nchini, kutokana na ukweli kwamba huwezi kupata majibu sahihi ya nani atachaguliwa jimbani kwa maoni ya watu 50 tu, hapa dr. bana na REDET yake kachemsha. na kwa nini hawafanyi tafiti zingine zaidi ya nani atakuwa raisi, nani atakuwa mbunge. labda kwa kuwasaidia wafanye tathimi ya tafiti walizofanya na hali halisi ya sasa. tafiti zao nyingi ni irelevant. inavyoonekana wapo kwa ajili ya kuwasafishia njia watu fulani fulani tu. na mpaka hapo hawana mchango wowote kwa maendeleo ya nchi hii. ngoja ifike october an waone kama huo utafiti wao utaendana na matokeo.


Utafiti huu ni njia ya kupikia matokeo. Watafanya kila njia kufix matokeo haya na ya uchaguzi. Uchaguzi ukiwa huru na haki CCM itapata wabunge chini ya 50% na Kama JK atashinda basi hatavuka 55% ya kura zote, huko Zanzibar CCM ndiyo watashindwa kabisa.
Quote
 
 
-4 #30 2010-04-28 16:48
NAUNGA MKONO HOJA YA UTAFITI ULIYO FANYWA NA REDET. BINAFSI NIMEKUWA NIKIFUATILI MCHAKATO HUU KATIKA VYUO MBALIMBALI, MAJIBU YAMEKUWA SAMBAMBA NA REDERT. HII NI ISHARA TOSHA YA KUKIRI KUWA WAKIRISHI WA WANANCHI BUNGENI WATAKUWA KATIKA WAKATI WA JOTO LISILO NA KIKOMO.
Quote
 
 
+1 #29 2010-04-28 16:34
Kazi kubwa inayofanywa na REDET kwa niaba ya CCM ambao ndiyo wanatoa fund ya utafiti biased ni kuwaandaa wadanyika kuwa wapole pindi KURA ZITAKAPOIBWA, au manipulated to favour CCM "Voter fraud" na kuwadanganya wafadhili kuwa uchaguzi ulienda vizuri kwani maoni ya watanzania yalioneshwa hata kabla ya Uchaguzi.

REDET Imepoteza credibility katika research zake biased wanachofanya ni kuganga njaa ili serikali ya CCM iendelee kuwapatia fedha za walipa kodi waendelee kudanganya umma wa watanzani
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner