MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Bunge latoa masharti kupokea shangingi la Mbowe  Send to a friend
Wednesday, 22 June 2011 22:58

LAMTAKA AACHE KILA KITU ALICHOPEWA, MTIKILA AMUUNGA MKONO
Kizitto Noya, Dodoma na Raymond Kaminyoge, Dar
OFISI ya Bunge imemtaka Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kususia pia huduma zingine anazopewa na Serikali kulingana na wadhifa wake, badala ya kukataa gari, dereva na mafuta pekee.

Akizungumza na gazeti hili mjini hapa jana, Kaimu Katibu wa Bunge, John Joel alisema huduma zote anazopewa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni zipo kisheria, hivyo hawezi kuchagua masharti anayotaka kuyafuata na mengine kuyakataa.

"Haya ni mambo ya kisiasa na sisi kama watendaji hatutaki kujiingiza kwenye siasa. Lakini niseme tu kwamba, lile gari hakupewa kufanyia shughuli za kisiasa ni la Serikali kwa ajili ya kazi zake kama Kiongozi wa Upinzani Bungeni," alisema Joel na kuongeza:
"Wabunge wote wanaongozwa kwa masharti, Spika ana masharti yake, Kiongozi wa Upinzani Bungeni ana masharti yake na wabunge wengine nao wana masharti yao. Sasa mtu huwezi kukubali masharti fulani na kukataa mengine, huku ni kuvunja sheria."

Joel alisema moja ya masharti aliyopewa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni ni kupokea gari la Serikali, dereva na kuwekewa mafuta kwenye gari hilo wakati wa shughuli za Bunge.

"Sasa pamoja na kupewa gari, Ofisi ya Bunge pia inawajibika kisheria kumpa kiongozi huyo nyumba mbili; Dar es Salaam na Dodoma na mlinzi wa kulinda usalama wake wa kila siku," alisema Joel.Aliendelea,"Sasa akisema gari sitaki, huu ni utashi wake, lakini kwa nini akatae gari tu wakati kuna huduma zingine anazopewa?"

Juzi baada ya kupitishwa Bajeti ya Serikali, Kambi ya Upinzani ilitangaza mgogoro na Bunge wa kutochukua posho za vikao vya Bunge kuanzia jana. Lakini hili lingefanyika baada ya kuwasilisha taarifa rasmi bungeni jana.
Sakata la kugomea posho za vikao, lilitangazwa kwa mara ya kwanza na Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Zitto Kabwe na tayari ameandika barua ya kuikataa posho hiyo.

Hata hivyo, wakati kambi hiyo ikitoa msimamo huo wa pamoja, Mbowe  alitangaza kuacha kutumia gari alililopewa na Serikali, dereva na mafuta kama sehemu ya kuonyesha kutoridhishwa na hatua ya Serikali kudharau mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa na kambi hiyo kuiboresha bajeti.

"Tumewaita hapa kueleza msimamo wetu kama Kambi ya Upinzani baada ya Serikali kuyakataa baadhi ya mapendekezo yetu. Serikali haikukubaliani nasi kuondoa sitting allowances (posho ya vikao),"alisema Mbowe na kuongeza:
"Haikukubaliana nasi pia kuuza mashangingi ya anasa, kuondoa misamaha ya kodi kwenye makampuni ya madini, katika susala la pension kwa wastaafu na kupunguza gharama za kuwasafirisha viongozi wa umma kwenye first class (daraja la kwanza)."

"Sisi tunaamini kuwa viongozi wanaopaswa kusafirishwa kwa ndege katika daraja la kwanza ni Rais na mke wake, Makamu wa Rais na mkewe, Waziri Mkuu na mke wake, Spika wa Bunge na mwenza wake. Halafu mawaziri wanapaswa kusafiri kwa daraja la kawaida na wabunge wote,"
Aliendelea" Na kwa kuwa hawataaki kukubaliana nasi kuuza magari ya fahari, mimi kuanzia sasa (juzi), silitaki gari lao, dereva wao na hata mafuta yao, habari ndio hii."

Barua ya Chadema haijafika Ofisi za Bunge
Lakini Joel alisema kuwa hadi jana mchana, hakuwa amepokea barua yoyote kutoka Chadema ya wabunge wake kukataa posho wala Mbowe, kugoma kuendelea kulitumia gari, dereva wala mafuta.

"Siwezi kufanya kazi kwa taarifa za vyombo vya habari. Mbowe hajanipa gari wala sijapata barua ya wabunge kukataa posho. Mambo hayo yapo kisheria muulizeni (Mbowe) kanipa lini gari hilo?"alihoji

Bunge kuendelea kuwalipa posho
Kuhusu wabunge hao kutochukua posho, Joel alisema posho hizo hazitasitishwa kutolewa kwao hadi utaratibu utakapobadilishwa. "Haya mambo yapo kisheria jamani, nisipowalipa posho mimi nashtakiwa," alisema.

Aliendelea"Mbunge anapewa posho kama sharti namba 3. Sasa kusitisha posho hizo ni mlolongo mrefu ambao hauwezi kufanyika kwa haraka kiasi hicho. Kinachoweza kufanyika, ni kila mbunge anayetaka kutochukua posho kuniandikia barua na sio kama kambi kwa sababu posho hizo ni za mbunge."

Akishaniandikia barua, alisema " Kuna njia mbili; moja ni mimi kumpa posho yake halafu yeye airudishe serikalini au mimi niikatie risiti halafu niirudishe serikalini, lakini haiwezi kupelekwa kwingine kokote zaidi ya kuwapa wabunge wenyewe."

Joel alipuuza madai ya kambi hiyo kutaka kuwe na fomu mbili bungeni;  kulipana posho bungeni na fomu ya mahudhurio ili wao wasaini fomu ya mahudhurio tu, wasipewe posho hizo, akisema "Fomu iliyopo ni ya mahudhurio, wanataka fomu gani sasa?

Lissu adai Mbowe alirejesha shangingi
Mbowe jana hakupatiakana ofisini kwake kuzungumzia suala hilo, lakini, Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu alisisitiza kuwa tayari alirejesha gari hilo tangu Jumatatu.
"Ni kweli barua hatujapeleka ila itapelekwa kesho, lakini tayari Mbowe amerudisha gari hilo tangu juzi (Jumatatu) na ameanza kutumia usafiri binafsi," alisema Lissu.

… apongezwa kwa kurudisha shangingi
Katika hatua nyingine, baadhi ya wanasiasa, wasomi na wananchi wamepongeza uamuzi wa Mbowe wa kurudisha gari la Serikali ili kuipunguzia gharama za uendeshaji.
Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila aliunga mkono uamuzi huo na kusema hata katika nchi tajiri viongozi wenye nyadhifa za uwaziri wanatembelea magari ya kawaida.

“  Uingereza nchi tajiri, lakini mawaziri wake wanatembelea vigari vidogo vinaitwa Austin, lakini sisi na umaskini wetu mawaziri wanatembelea magari ya kifahari,” alisema Mtikila na kuongeza.
“ Inashangaza sisi walalahoi, lakini viongozi wanatembelea magari ya kifahari kuwashinda wanaotupa misaada, hivi viongozi hawa hawajifunzi,” alisema Mtikila.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, (UDSM), Dk Benson Bana alisema, Mbowe ana hoja ambayo inapaswa kuungwa mkono na watu wengi wenye kuitakia mema nchi hii.
Dk Bana alisema ingawa hoja hiyo inamjenga Mbowe kisiasa, lakini ukweli unabaki kuwa Serikali inatumia fedha nyingi kuyahudumia magari hayo.

Naye Shaaban Mtawa,  fundi wa magari wa Kinondoni jijini alisema kitendo cha Mbowe kurudisha gari hilo kimemfurahisha na kuwataka viongozi wengine kuiga mfano huo.
“Viongozi wengi wanaishi Dar es Salaam, wanatembelea magari ya kifahari bila ya sababu ya msingi wakati yanatumia fedha nyingi,” alisema.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Julius Mtatiro alisema kinachofanywa na Mbowe ni propaganda za kisiasa zenye lengo la kumpatia umaarufu.

“Mbowe ni Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni, amepewa gari kwa ajili ya kazi hiyo, anarudisha gari kwa sababu yeye ni tajiri, angekuwa hana uwezo kama wabunge wengine angefanya hivyo?,” alihoji Mtatiro.
Mtatiro alisema Mbowe asijifanye kuwa anawahurumia Watanzania maskini wakati maisha anayoishi ni ya kifahari yasiyofanana na wananchi wa kawaida.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Thursday, 23 June 2011 23:38
 

Comments 

 
0 #146 2011-06-24 16:30
Bwana Beano: Asante. Lakini nadhani unachanganya mambo. Ukiangalia Mabunge ya Wenzetu kazi ya upinzani si kutoa ushauri kwa Serikali iliyopo madarakani ila ni kuonesha kuwa Serikali iliyopo Sera zake mbuvu ila za upinzani ndiyo nzuri. Angalia vizuri Japani, Uengereza, Marekani upinzani unavyofanya.

Hata hivyo nakushukuru kwa kueleza kuwa baadhi yetu waTZ tunamalezi yasiyotusaidia kujua hoja ipi ni hoja ya nguvu na ipi ni ya nguvu ya hoja!!
Quote
 
 
0 #145 2011-06-24 15:54
kwa mtatitiro si ajabu kuropoka hivyo kwa akiwa kama mpinzani ndani ya wapinzani lazima ajisikie vibaya chadema wanapofanya mambo yanayowaletea heshima kwa wananchi.kwa ujumla ni uamuzi sahihi kurudisha shangingi kwani yote yakirudishwa yakapigwa mnada hatukosi japo vibilioni vitatu vy akununulia matrekta tukaleta mapinduzi makubwa ya kilimo.
Quote
 
 
-1 #144 2011-06-24 11:31
kweli wanasiasa mnabwembwe Mbowe kama wewe unamachungu na nchi na wananchi wake tutaona vinginevyo utatoa mtaji kw [CCm,siku zijazo.
Quote
 
 
+1 #143 2011-06-23 23:08
Ama kweli siasa inamanbo. Hongera Freeman! Sasa umekuwa huru. Kule Kenya Wabunge nafisadi nao hawataki kulipa kodi. Huku Tz hawataki posho na Mashangingi yaondolewe ili fedha ziokolewe na kumfikia mwananchi. Tutaona hatima yao muda si mrefu!
Quote
 
 
0 #142 2011-06-23 22:02
Anajiita mtoto wa mkulima wakati wa watoto wake wapo arkansas marekani na amerudisha gari ikawa ni sawa bali mbowe inaonekan kuwa nawaambua basi wanamletea vikwazo huyo handsome boy aliporudisha shangingi lake alinyang'anywa na ulinzi au huduma nyingine!???
Mbona hawa viongozi wanongozwa na jaziba na mjungu kama huyo spika ni roboti tu hakuna nachofnya hapo zaidi ya kufanya anachoambiwa na wazee.
Paka tuanze kujilipua wenyewenywe ndio mtaona tumechoka u[NENO BAYA] wa wenu mafisadi
Quote
 
 
+2 #141 2011-06-23 21:06
hongera sana mbowe kwn ma2miz yacyo ya lazma yanarudsha maendeleo ya tanzania nyuma,hata km ikiwa ni kwa kiac kidogo.wote wakiiga mfano huo tanzania itasogea!!
Quote
 
 
-1 #140 2011-06-23 20:32
Jamani ee si mashangingi na posho tuu bali tujadili na mishahara yao
Quote
 
 
+3 #139 2011-06-23 19:32
mimi naishi hapa uingereza. nilikuwa tanzania mwezi wa pili na nikapata nafasi ya kwenda kuona makao makuu Dodoma. Jambo ambalo limenikasirisha sana kuona magari ya serikali mashamgigi yakiwa yananguruma, na dereva kuwasha air condition na kulala hapo ndani akimngojeaya mheshimiwa anakunywa chai na vitafuniyo. Piya mtindo huwo niliona sana magari yote ya serikali kupoteza mafuti mengi mno madereva kukaa ndani na kutumiya kifahari hizo air condition. Jamani mbona zamani wakati wa mwalimu mawaziri walikuwa wakitumiya landrover 110. Na maofisi ya serikali ilikuwa hazina air condition. kwa nini mawaziri wanavaa masuti wakati hali ya hewa Dar ni joto sana. Ni lazima tutumiya kaunda suit kama ni viongozi, lakini hizo suti ndiyo zimesababisha umeme kutumiwa sana maofisi yote ya serikali. Nchi haitaendeleya, bali serikali ni jeuri haitaki kusikiya watanzania.
Quote
 
 
+3 #138 2011-06-23 19:18
mtatiro wewe ni mropokaji tunakujua toka chuo. uwezo wak ni mdogo sana. rudi shule ujifunze kuonea kipaji cha uongozi huna
Quote
 
 
+2 #137 2011-06-23 19:13
Quoting Omtemi Nyamranga:
Najua nitapata alama za hasi nyingi sana kwa hili nitakalo ongea hapa chini. Na hii inatokana na watu tuliowengi kuchangia hoja kwa kuangalia Chama badala ya mantiki ya hoja.

Mie nadhani upinzani unaongozwa na CHADEMA kwa hili wanakosea. Ukisema kuwa kwa kuwa ushauri wao wa kuboresha Bajeti ya Serikali umekataliwa basi wanasusu masuala fulani!! Inabidi tujiulieze vizuri kuwa upinzani kazi yao ni nini? Navyojua mie kazi yao si kushauri Serikali iliyopo madarakani, bali kazi yao kuu, katika mfumo wa vyama vingi, ni kutoa Bajeti mbadala na kuonesha wao ambavyo wangetenda. Kwa namna hiyo wananchi wanaendelea kupima kuwa nani angewaletea maisha bora zaidi kupitia Bajati na kwa hali hiyo inaboresha ushindani katika Uchaguzi ujao. Kwa maana fupi ni kuwa wananchi wataona kumbe Serikali mbadala ni hii na hivyo kuipa ushindi katika uchaguzi. Nje ya mfumo huo tunajichanganya kuwa ushauri wao unapashwa kusikilizwa na kutekelezwa!! Hii inanipa shaka kiasi fulani kuwa "hivi kweli tunajua maana ya mfumo wa vyama vingi?

Mungu tubaliki Watanzania

Shida ya watu wengi kama wewe ni malezi. Malezi yetu waafrika yanatuongoza ktk manung'uniko na malalamiko pasipo kuwa na matendo. Sikuelewi unaposema kuwa kazi ya upinzani ni kutoa bajeti mbadala na kukaa kimya kusubiri uchaguzi ujao. Angalia mabunge ya wenzetu jinsi nguvu ya upinzani inavyochochea maendeleo. Bila kutumia nguvu ya umma hiii hali ya viongozi kuwa walaji wa fedha za umma haitamalizwa kwa majadiliano. Kuna mambo ambayo hayawezi na hayatakiwi kusubiri uchaguzi.
Quote
 
 
+2 #136 2011-06-23 19:09
hivi nyie mnaosema kuna sheria na masharti ya kuzingatia mlikuwa wapi pinda alivokata gari kama mbowe? Mtatiro yeye anajua wamefunga ndoa na ccm kwa vovote hawezi ku support hilo.Mbowe anataka gari na bei rais ndo mantiki yake.CCM kazi yao kung'ang'ania posho na anasa wanajua ubunge waliupata kwa gharama lazma walipe sasa.India,Maleysia, singapore,zilie ndeleakwa viongozi kuonesha mfano.Rwanda2 imepiga hatua kubwa si kagame alipiga bei hayo mashangingi kwa nini tusiige?
Quote
 
 
0 #135 2011-06-23 19:08
Kwenye maslahi ya nchi yabidi tuache mambo ya itikadi za vyama,CHADEMA,w ameonyesha kwambamatumii yasiyo na faida ya msingi kwa wananchi lazima yapigwe vita na yakataliwe daima,hongera sana CHADEMA
Quote
 
 
-3 #134 2011-06-23 18:00
MIMI NAFIKIRI KAMA MBOWE NI MZALENDO ANGEANZA PALE HOTELINI KWAKE.HOTELI YA MACHAME AISHI INAYOMILIKIWA NA MBOWE CHINI YA PROTEA HOTELS INA WAFANYAKAZI WA KENYA ZAIDI YA 80% SASA KUKATAA GARI NI GERESHA ZA KISISA TU AACHE KUTUDANGANYA.HIYO GARI NA ZILE HELKOPTA NI KIPI CHA GARAMA?
Quote
 
 
+3 #133 2011-06-23 17:48
gari anaweza kurudigari posho na marupurupu, lakini nyumba na ulinzi lazima apewe kwa usalama wake akiwa bungeni ni haki yake; kama mna garilisilo shangingi mpeni atapokea lakini hilo kakataa kama alivyyokataa pinda, mbona hamkusema ni la kisheria?
Quote
 
 
+2 #132 2011-06-23 17:35
Kwa ujumla michango mingi ya CHADEMA Bungeni imeshinda ile ya CCM kwa hoja zenye maslahi kwa Taifa ila haikupita kwa kuwa ni wachache Bungeni
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner