MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Dk Slaa atajwa Urais Chadema  Send to a friend
Wednesday, 21 July 2010 08:32

Mussa Mkama
KAMATI kuu ya Chadema jana ilikutana jijini Dar es Salaam kujadili mambo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na mkakati wa kumpata mgombea urais wa chama hicho baada ya mwenyekiti wake, Freeman Mbowe kuamua kugombea ubunge.
 
Habari kutoka kwa viongozi wa chama hicho zinasema kuwa mbunge wa Karatu, Dk Wilbroad Slaa ndiye anayeangaliwa zaidi kushauriwa kujitosa kwenye nafasi hiyo baada ya mjumbe wa kamati kuu, Profesa Mwesiga Baregu kugoma kugombea urais.
 
Tayari Dk Slaa ameshachukua fomu za kutetea kiti chake cha ubunge cha Karatu, lakini habari zinasema kuwa Chadema inamtaka katibu huyo mkuu kugombea urais baada ya kulichangamsha Bunge kwa hoja nzito katika vipindi vyake alivyolitumikia jimbo hilo.
 
Chadema, ambacho kimeongezeka nguvu katika kipindi cha miaka mitano baada ya kuingiza wanachama machachari ndani ya Bunge, imekuwa ikisaka mgombea urais ambaye ataweza kuendeleza umaarufu wa chama hicho na vyombo vya habari vimekihusisha chama hicho na mipango ya kumshawishi waziri mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye na Spika wa Bunge, Samuel Sitta kuingia kwenye mbio za urais kwa tiketi ya chama hicho.
Hata hivyo, taarifa za vyombo vya habari zimeeleza kuwa vigogo hao wawili wa CCM wamekataa kukiasi chama chao.
 
Katika uchaguzi mkuu uliopita, Mbowe alishika nafasi ya tatu kwenye harakati za kuingia Ikulu baada ya kufanya kampeni zilizogusa sehemu kubwa ya nchi, akitumia helikopta, lakini safari hii atagombea ubunge wa Jimbo la Hai.
Kama Dk Slaa atajitosa kugombea urais kwa tikei ya Chadema, CCM watakuwa wamepata mteremko wa kuchukua jimbo la Karatu ambalo wamekuwa wakilisaka kwa udi na uvumba.
 
Mkurugenzi wa Mambo ya  Nje wa Chadema, John Mnyika alikataa kuzungumzia kikao hicho na kueleza kuwa waandishi watapewa taarifa kamili leo.
“Baada ya kikao  kumalizika kesho, tutaitisha mkutano na waandishi wa habari... kitafanyika wapi na saa ngapi tutawajulisha usiku,” alisema Mnyika.
 
Tayari CCM imeshamteua mwenyekiti wakr, Jakaya Kikwete kuwa mgombea urais wakati CUF imemteua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mgombea wake.
 
Mwenyekiti wa TLP, Agustine Mrema naye hatagombea urais kwa tiketi ya chama hicho baada ya kuamua kurejea Vunjo kugombea ubunge. Mrema pia alishawahi kuwa mbunge wa Temeke..


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Thursday, 22 July 2010 08:08
 

Comments 

 
+1 #90 2010-07-22 08:58
chadema mmeionyesha dunia kuwa mmekomaa kidemokrasia kwa kubadali wagombea kila uchaguzi mkuu wa taifa..hongera dr. slaa mwamini Mungu na utashinda.vivaaaaa slaa vivaaaaaaaaaaaa aaa
Quote
 
 
-2 #89 2010-07-22 08:49
hapa myama ameshatuzonga kwa kumpoteza mtu makini bungeni na wala ikulu si rahisi kuingia. ataishia mahakamni kushitaki ameibiwa kura, kesi itakayoendeshwa miaka mitano halafu uchaguzi mwengine unakuja anagoombea tena.
nasema hivi kwa kua kama wapo wanaofahamu Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini duniani basi ni mimi na wewe ambao tunatumia Internet na kufuatilia habari kwa ajili ya kazi zetu za kila siku. hadi leo nina hakika asilimia zaidi ya 50 hawafahamu ni nini richmond, epa wala kagoda. katika hao wanaofahamu basi wapo wanaopongeza hatua zilizochukuliwa na viongozi walioko madarakani eti kulishughulikia , pia kuna wanafiki wanaokunja uso kuponda yaliyofanyika lakini mioyoni mwao wanaimani kubwa na uongozi ulioko madarakani eti umefanya vizuri. tuliobaki ukweli ni kwamba tupo kidogo tusiokubali hali hii tuliyonayo. na hivyo mchango wettu kumueka dokta slaa madarakani utakua mdogo. ingekua Zanzibar Dr. angepita kwa kua ZNZ CCM sasa inashinda kwa kupindisha sheria, kutumia nguvu, vitisho, na wizi wa dhahiri lakini wananchi wameshaikataa. kwa hiyo nashauri tuangalie njia nyengine kwa docta ila uraisi itahitaji nguvu ya ziada na muda wa miezi mitatu hautoshi jamani. haya ni mawazo yangu
Quote
 
 
0 #88 2010-07-22 08:10
Mie nafikiri kila kitu kinaanza kwa matayarisho. Kwa Dr. Slaa kuingia sasa katika kinyang'anyiro cha Urais ni sawa kabisa. Najua hatapata lakini umma wote utapata kumfahamu na hasa wale wasiomjua hata kidogo watamfahamu. Then next step ni kukusanya nguvu zaidi ya kwa ajili ya uchaguzi wa 2015.
Quote
 
 
-1 #87 2010-07-22 07:55
Jamani watanzania wenzangu naomba tuchukuwe mambo kwa tahadhali na tafaakari ya kina,kupunguza nguvuya upinzani bungeni kwa madai ya ugombea Urais,mi bado sikubaliani na mawazo hayo hata kama yametoka kwenye kamati gani. Sababu kuu ya msingi na kwamba tunahitaji kwanza kuimarisha nguvu kaitika muhimili huu kwanza ambao ndio unaweza kuendelea kubeba sheria hovu au kuziondoa, je ni nani atakae tufanyia hayo na huku tunapunguza nguvu za hoja Bungeni? nafikiri hili lingekuwa na kura za maoni ya wananchi maamuzi ya kamati lazima yangebwagwa kwa kishindo,tunait aji Bunge LA NUSU KWA NUSU kwa upinzani wa hOja na SIO NUSU KWA NUSU za KIJINSIA kwanza hili tuandae mazingira mazuri ya kuingia Ikulu. Dr. kuwa makini katika hilo.
Quote
 
 
-1 #86 2010-07-22 07:15
Uraisi si lelemama
Nawashauri vyama vya siasa muda bado wa kuingoa CCM mwalimu alisema labda miaka 40 ndio CCM itatoka madarakani huu ni msemo wa kweli tu. Mimi nafikiri vingozi wote wa vyama vya upinzani wa ngazi ya taifa chukuweni fomu za ubunge kwani kuishinda CCM ni kuwa na viti vingi vya ubunge ili kila jambo ambalo si manufaa kwa watanzania halitapita kiurahisi kwa kura nyingi ambazo CCM wana viti vingi Bungeni, mkifanya hivyo tutaweza kuishinda CCM kwa hoja ambazo si za msingi kwa watanzania. nawashauri hivyo kwani katika uraisi CCM wamejipanga ila kwa wabunge hakuna hoja ingawa mimi ni sina chama chochote cha siasa.
Quote
 
 
0 #85 2010-07-22 07:13
Quoting yohani:
Quoting AMSI Hhando:
Quoting Bana:
Dr. Slaa hajakomaa kwa cheo cha URAHISI! Bora abakie na Ubunge ambao pia safari hii sijui kama atapona kule Karatu


Kwa hiyo URAIS UNAHITAJI AKILI KAMA ZA KIKWETE NA MAKAMBA SIO

....Kimsingi napenda kuheshimu mawazo ya watanzania wenzangu lakini pale yanapokuwa chini ya Kiwango cha uelewa wa Darasa la VII lazima tuseme, huyu Bana kinachomsumbua ni ushabiki wa undugu,uhasama, umbea au uwanaCCM ambao mimi ndo naufahamu kuliko yeye aliyeishia Kilima Tembo? Garma naas jiulize unawatakia mema watanzania au unajali zaidi maslahi yako? Umekuwa mpofu hauna mfano...wairaqw hatuna dalili ya ushabiki pasipo ukweli wa jambo. Ebu waeleze watanzania upungufu wa Sla'a' kuwa Rais tofauti na Kikwete. Tuache unafiki,nataka nijue ukweli wa moyo wako.

Yaani huyu jamaa sijui kama akili zake za kupambambanua mambo ziko sawasawa. Yaani akiwekwa Jk na Dr. Slaa kwa kusimamia hoja za msingi JK ataweza? Mfano ni hotuba ya kuahirisha Bunge kwenye mambo ya msingi ambayo yalikuwa ya kukalipia yeye alikuwa anacheka tena peke yake. Bwana Acha watanzania wanaotaka wananchi waneemeke washike nchi. Si kwamba CCM wote ni mabomu la!!! kuna vichwa vizuri tu lakini vimezungukwa na watu wasio faaa.
Quote
 
 
+1 #84 2010-07-22 03:02
kwanza watanzania tumshukuru MUNGU kwa kuwa na nafasi ya kumchagua kiongozi tunaye mtaka na pia tupambane kutafuta ukombozi wetu ukombozi aupatikani kirahi ila tukiungana na kupambana kisawasawa tunawezakuona mabadiliko kwa kutumia njia tofauti na siyo kuwa na imani ya njia moja tu.hivyo basi mwaka huu tujaribu njia ya kuwakataa mafisadi ccm, na kuwapa nafasi hizo watu wengine alafu tuangalie nini kitakacho tokea ndani ya miaka mitano.
Quote
 
 
+2 #83 2010-07-22 01:58
YES WE CAN hongera Dr., tunakuamini, tunakupenda na uko makini. Jamani hakuna haja ya kuhofia,kushind wa ni moja ya matokeo na ndo demokrasia yenyewe kama taratibu zote zitakuwa zimefuatwa.
Kwanza ww kama ww, amua kwamba utampa kura dr, halafu angalia familia yako, marafiki na jamaa zako wote, upande wa wafanyakazi sina shaka kura amepata
Quote
 
 
-1 #82 2010-07-22 01:42
ni habari njema kwa MTZ lakni ni neema kwa ccm karatu, bunge lijalo lita pwaya.maana sio siri.kwa mfumo wasiasa za bongo{winner takes all}Dr Slaa hapati kitu.maana mpaka jaji mkuu ccm kuna kupinga matokeo hapo?
Quote
 
 
+2 #81 2010-07-22 00:51
dr.tunakuhitaji sana kwani huu ndomuda mwafaka wa mabadiliko ktak nchi yetu.tuache uoga wa mawazo mgando watanzania tuamke kwan mabadiliko hayaji kama ccm itaendelea kukaa madarakan
Quote
 
 
+2 #80 2010-07-22 00:11
hakika watanzania tuamke habari ya kusema fulani hawezi fulani anaweza yamepitwa na wakati, wala hakuna anayeweza kuwa mungu wa watanzania, kila mtanzania pamoja na dr. slaa anaweza maadam watanzania tuamke, kama inawezekana kwingineko; kwa nini si tanzania, hongera dr. Slaa, taa ya watanzania ya kufichua ufisadi unalindwa kwa nguvu zote na thi thi em, Dr. inawezekana jipe moyo watanzania wenye nia na nchi yao wako nyuma yako tumechoka kukaa na umasikini kwa takriban miaka 50 ya uhuru wetu, tuwe tu kila siku moja kati ya nchi masikini kabisa 10 duniani wakati wenzetu wanapeta; tuangalie tu hata nchi ambazo tanzania ilisaidia kukomboa uhuru wao zinatupita kiuchumi kama msumbiji tumechoka na aibu hii ya watu kujaza matumbo yao na shingo wakati uchumi wa nchi wadidimia daima dumu!
Quote
 
 
+2 #79 2010-07-21 21:01
hi ni vita babu kubwa ila siasa ni game na wanaoelewa mchezo huo ni wanasiasa wenyewe
Quote
 
 
0 #78 2010-07-21 20:57
Quoting AMSI Hhando:
Quoting Bana:
Dr. Slaa hajakomaa kwa cheo cha URAHISI! Bora abakie na Ubunge ambao pia safari hii sijui kama atapona kule Karatu


Kwa hiyo URAIS UNAHITAJI AKILI KAMA ZA KIKWETE NA MAKAMBA SIO

....Kimsingi napenda kuheshimu mawazo ya watanzania wenzangu lakini pale yanapokuwa chini ya Kiwango cha uelewa wa Darasa la VII lazima tuseme, huyu Bana kinachomsumbua ni ushabiki wa undugu,uhasama, umbea au uwanaCCM ambao mimi ndo naufahamu kuliko yeye aliyeishia Kilima Tembo? Garma naas jiulize unawatakia mema watanzania au unajali zaidi maslahi yako? Umekuwa mpofu hauna mfano...wairaqw hatuna dalili ya ushabiki pasipo ukweli wa jambo. Ebu waeleze watanzania upungufu wa Sla'a' kuwa Rais tofauti na Kikwete. Tuache unafiki,nataka nijue ukweli wa moyo wako.
Quote
 
 
+1 #77 2010-07-21 19:52
Ni wakati mzuri sana sasa CHADEMA na CUF kuungana ili kuifuta Historia ya CCM. Kwa nini Mheshimiwa Hamad Rashid asikubali kuwa mgombea mwenza wa Dr Slaa? Nionavyo mimi iwapo vyama hivi vitaungana vinaweza kuwazoa wapiga kura wengi na hata wana CCM.
Quote
 
 
0 #76 2010-07-21 19:11
Quoting GODY:
Wapinzani nawashauri mgombee ubunge woteeeee, Kiti cha Urais Mwachieni Mwenyewe , ili muongeze nguvu Mjengoni. "Ikulu sio pa kukimbilia kama alivyowahi kunena Mwalimu"

Ninyi ndo watu ambao hatuwahitaji kabisa katika nchi yetu maana akili zenu bado ni finyu,hivi huoni kuwa unachokisema hujui maanayake! Kwa maana umekariri vibaya aliyoyasema mwalimu,kama huji ni bora uulize ili uambiwe na kufafanuliwa maana yake,kama hutapata wa kukufafanulia fikiria hotuba ya mwalimu aliitoa katika mazingira gani na wapi na kwa lengo gani! Usikariri! Kwa taarifa yako huu ni mda mwafaka wa kuhitaji mabadiliko;na hata kama hatutayapata wajukuu wetu watayaleta na kuishi maisha bora kuliko haya ya ushabiki na kuacha ndugu zetu vijijini wakifa kwa njaa na huduma duni za kiafya,eeeeeeee eeeeeee mungu ibariki Tanzania,AMEN
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner