MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Pingamizi la Chadema kwa JK latua kwa Msajili  Send to a friend
Tuesday, 31 August 2010 00:21

Geofrey Nyang’oro
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeteketeza azma yake ya kumwekea pingamizi mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete.

Taarifa zimeeleza kuwa chama hicho kiliwasilisha pingamizi hilo kwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini jana saa 7:30 mchana.

Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho John Mnyika, ndiye aliyewasilisha pingamizi hilo.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa alipoulizwa hakutaka kukubali au kukataa kuliona pingamizi hilo na akasema atazungumzia suala hilo leo.

Awali Chadema ilipanga kuweka pingamizi hilo la kutaka Kikwete azuiwe kugombea urais, Agosti 27 mwaka huu, lakini, ilisitisha kwa kile ilichoeleza kuwa inasubiri mambo mengi zaidi ambayo wangeyaingiza kwenye pingamizi hilo.

Chama hicho awali kilitaka kuweka pingamizi hilo kwa kile kilichoeleza kuwa  Rais Kikwete amekiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa kutangaza nyongeza ya mishahara ya wafanyakazi kwenye kampeni.

"Tulishindwa kupeleka pingamizi hilo jana kwa sababu tumesikia kwamba huku anakoendelea na kampeni zake, mgombea huyo ameendelea kufanya makosa mengine ambayo tutataka tuyaingize kwenye pingamizi hilo," alisema Mnyika mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na gazeti hili jana muda mfupi baada ya kuwasilisha pingamizi hilo, Mnyika alibainisha kuwa mambo mengine mapya yaliyoingizwa kwenye pingamizi hilo ni mgombea huyo wa CCM kuahidi kukilipia Chama cha Ushirika cha Nyanza deni la Sh 5 bilioni na kuahidi kununua meli kwa ajili ya watu wa mikoa ya Kagera na Mwanza.

Mnyika alisema tayari Chadema imewasilisha pingamizi hilo jana lakini, ina mashaka kama ofisi ya msajili itawatendea haki.

“Sisi tumeshawasilisha pingamizi letu kwa msajili wa vyama vya siasa kama Sheria ya Gharama za Uchaguzi zinavyoelekeza, lakini, tuna tumaini lenye shaka ndani yake kama tutatendewa haki,”alisema Mnyika na kuongeza.

“Mheshimiwa Kikwete wakati wa kipindi cha kampeni za uchaguzi, moja kwa moja akitumia nafasi yake kama rais, ameongeza na /au kuahidi kuongeza mishahara ya wafanyakazi kwa kupandisha kima cha chini kutoka Sh130,000 hadi Sh235,000,”inasema sehemu ya kwanza ya pingamizi hilo lenye sehemu tatu.

Katika pingamizi hilo, Chadema pia ilieleza kuwa mgombea huyo wa CCM, ameahidi kutoa Sh5 bilioni kwa chama cha Ushirika cha Nyanza ili kilipe madeni yake mbalimbali na kuahidi kuwa serikali itachukua madeni yote ya vyama vya ushirika.

Chadema pia imesema katika sehemu ya tatu ya pingamizi hilo kuwa mgombea Kikwete alitumia nafasi yake kwa kuwaahidi watu wa mkoa wa Kagera kuwa atawanunulia Meli mpya, kubwa na ya kisasa.

"Ahadi hizo ni sehemu ya mambo yaliyokatazwa kwa mujibu wa kifungu cha 21 (1) (a) na (e) cha Sheria ya Gharama za Uchaguzi namba 6 ya mwaka 2010," imeendelea sehemu ya pingamizi hilo.

Mnyika alifafanua kuwa kwa mujibu wa sheria hiyo, vitendo hivyo vilikuwa na nia ya kushawishi wapigakura wampigie kura mgombea huyo wa CCM.

Kuhusu ahadi ya kuchukua madeni ya Chama cha Ushirika cha Nyanza, alisema kitendo hicho nacho kililenga kuwashawishi wananchi wa Mkoa wa Mwanza kumpigia kura.

“Nyongeza ya mishahara, ahadi ya Sh5 bilioni na ahadi ya meli kutumika kama hongo/rushwa kwa hao wote wahusika ili wampigie kura Kikwete," alisema Mnyika na kueleza kifungu kinachozuia mambo hayo kuwa kinasema:

"Mgombea yeyote ambaye yeye mwenyewe, wakala wake au chama chake kitafanya kitendo ambacho kimekatazwa na kama ilivyoelezwa katika sehemu hii, atakuwa, au, kitakuwa kimepoteza sifa za kushiriki katika mchakato wa uteuzi na uchaguzi.”

Wakati huo huo, mgombea urais wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemshukia Meneja wa Kamati ya Kampeni CCM, Abdulrahman Kinana na kumtaka anyamaze kwani katika orodha ya uchafu wa watuhumiwa wa ufisadi nchini hatoki.
 
Juzi Kinana aliwaambia waandishi wa habari kwamba, Dk Slaa anawadanganya wananchi kuhusu suala la ufisadi na kumtaka aache kufanya hivyo na anadi sera zake.
 
Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara katika Jimbo la Mikumi Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro jana, Dk Slaa alisema fisadi ni fisadi tu na hana njia nyingine ya kumpamba kwa maneno mazuri mtu anayeiba mali za umma.
 
“Namuonya Kinana anyamaze, nisije nikamshukia kwa sababu katika orodha ya wana-CCM waliofanya uchafu hatoki kupitia kampuni zake,” alisema Dk Slaa.
 
Dk Slaa alimgeukia Waziri wa Fedha na Uchumi,  Mustafa Mkullo kwamba pamoja na cheo chake cha uwaziri na ubunge katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, lakini wilaya yake ni moja kati ya tano zilizopata orodha chafu sana .
 
Dk Slaa anaendelea ziara zake za kampeni na leo anatarajia kufanya mikutano kadhaa katika mkoa wa Dodoma kwa kutumia usafiri wa helikopta.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Wednesday, 01 September 2010 01:12
 

Comments 

 
0 #129 2010-09-03 17:19
kweli chadema wanastahili kumuwekea JK pingamizi maana kampeni zake zilikuwa kama ziara za kiserikali hana jipya badala ya kunadi sera yeye ni ahadi tu. na kwa kuwa uchaguzi unaendeshwa kwa mjibu wa sheria,na kama kuna mazingira ya kuashiria kukiukwa hana budi kupampnishwa na mkondo wa sheria, hamna aliye juu ya sheria.safi sana chadema japo Nec haina mazingire ya kutenda haki
Quote
 
 
0 #128 2010-09-01 18:04
namheshimu sana Jaji Mkuu -kama jina lake lilivyo, lakini namuomba asingie kwenye siasa kama anataka na yeye aende ccm wakutane na marando jukwaani lakini asingilie siasa kwani inamuuma nini mtu kuwafichua wezi yeye kama jaji, naomba mkuu chondechonde taaluma na waadhifa wako haustahili kuingia kwenye siasa na kuwalinda wezi wanaotajwa naomba usiwatishe wananchi wenye kuitakia kheri nchi hii, wewe ni msafi hata kama sisiemu wanakupa mikoba inayokiuka ethics zako kama lile la mgombea binafsi umetuangusha saaaana mkuu, anyway tunakuomba usiingie kwenye siasa wewe hakutoi mtuu hata awe nani tenda haki, acha watu ambao wanajilipua majukwaani waseme ukweli ili tukate mzizi wa fitina, ni dhambi kwa mungu wako kama utajaribu kupindisha ethics za kazi zako acha wezi waumbuliwe wewe wasubiri wakiletwa kwako then unawachinjia mbali -wewe ni jaji sio kada wa ccm acha makamba aongee nao ukiongea wewe watatuibia mpaka watoto na wake zetu kwa sababu wanajua wewe ni kinga yao
Quote
 
 
0 #127 2010-09-01 16:33
kama alivyowahi kusema Rais J F Kennedy wa Marekani akiwambia wamerekani -Kwamba wasiulize Serikali itawafanyia nini bali wao wasema wataifanyia nini Marekani, SASA ni wakati muafaka wa sisi wote akiwamo Msajili Tendwa tutaifanyia nini nchi hii iliyoporwa na wachache? tutaifanyia nini nchi hii yenye siasa kandamizi? tutaifanyia nini nchi hii yenye uchumi unaoporomoka kila kukicha? tutaifanyie nini nchi hii ipate viongozi waadilifu? tutaifanyia nini nchi hii ambayo imegubikwa na ufisadi? Msajili mimi najitolea kukwambia wewe itendee haki nchi hii kwa kuleta kiongozi mwadilifu -tenda haki kwa kizazi cha sasa na kijacho cha watanzania, watanzania tunahitaji viongozi na hasa mkuu wa nchi ambae haogopi kuwafukuza kazi mafisadi, ambae hana ushikaji kwa watu wanaokula mali ya umma, ambaye ni mwadilifu, ambae anao uwezo wa kuipa uwezo wa kiutendaji mihili mitatu -bunge, mahakama na serikali. Hatutaki longolongo sa sasa zimetuchosha -tunataka mtu kama nyerere baba wa taifa, tunamtaka DR.Slaa, ni mwadilifu, anaefanya tafiti, ni mkweli, ni mtu wa wote si kwenye picha za mabango, bali mtu wa watu kwelikweli, Sera zake na chama chake zinatupa amani ya kweli, achana na amani ya kwenye majukwaa huku wachache wanaishi kamavile wako peponi wakati wananchi wanaishi kama vile wako motoni nani kakwambia hiyo ni amnai -wanatumia utulivu wetu kutuonea, kutuibia, kutuzulumu wanatukandamiza hawa, Haya msajili utaindea nini nchi yako usiogope kibarua -kama wengi wanavyoogopa usifanye longolongo nafsi yako itakusuta milele. Lipua piga chini ahadi za majukwaani na mwondokea kwenye orodha ya wagombea anadanganya umma kwani hukusikia aliposema hawezi kulipa wafanyakazi anachotaka na kwamba hataki kura zao, sasa gafla pesa kazitoa wapi? kama sio rushwa ni nini -hawatufai hawa tupilia mbali tuingize kifaa white house.
Quote
 
 
0 #126 2010-09-01 01:43
watanzania tubadilike tuchague viongozi bora sio vyama.
Quote
 
 
+3 #125 2010-09-01 00:10
WATANZANIA WENZANGU NAOMBA TUANGALIE JAMBO HILI;JAMBO LA KWANZA TUACHE ITIKADI ZETU ZA SIASA TUANGALIE UTAIFA WETU.PILI TUANGALIE TULIKOTOKA TULIPO SASA NA TUNAKOKWENDA.KIMSINGI KIHISTORIA SISI NI WATU WA AMANI,NA AMANI HII HATUJAIPATA WENYEWE AU KUPEWA NA KIKUNDI CHA WATU FULANI BALI TUMEIPATA TOKA KWA MUNGU MWENYEWE NI (NEEMA)HAKUNA UBISHI KATIKA HILI.TANZANIA NI NCHI YENYE UPENDELEO TOKA KWA MUNGU,NA NDIO MAANA TUNA KILA KITU KWA UPANDE WA RASILIMALI.KILA MTANZANIA ANAFAHAMU HILI.SASA NAJARIBU KUTAFAKARI KWA NINI MAISHA YETU KIUCHUMI YANAKUWA DUNI??WEWE MTANZANIA JAMBO HILI UMELIONA AU BADO BLANKETI LA UMBUMBUMBU LIMEKUFUNIKA KIASI KWAMBA HUELEWI KINACHOENDELEA??KWA UPANDE WANGU PAMOJA KWAMBA WATANZANIA TUNA KILA KITU(RASILIMALI )LAKINI NAONA TUMEPUNGUKIWA NA KITU FULANI,NACHO NI ""UONGOZI BORA NA UZALENDO"TUNAHITAJI UONGOZI BORA NA UZALENDO.BABA WA TAIFA MWALIMU NYERERE ALISEMA:ILI TUENDELEE TUNAHITAJI:"WATU,ARDHI, SIASA SAFI NA UONGOZI BORA.WATU TUNAO(WENGI WAMEKOSA AJIRA)SIASA SAFI NADHANI TUNAYO.LAKINI UONGOZI BORA HATUNA.NYERERE AMEONDOKA NAO.ILI KUPATA UONGOZI BORA TUNAHITAJI MWELEKEO WETU TUUELEKEZE KWENYE MAMBO AU WATU WAPYA,AMBAO TUNAO.WATU KAMA AKINA DR SLAA NI WAPYA NA MAMBO YAO NI MAPYA KABISA.TUNAHITAJI MTU KAMA DR SLAA KUTUONGOZA.MWELEKEO WA CHAMA CHA CHADEMA NI CHAMA KINACHOJALI UTAIFA NA UZALENDO.CHADEMA NI CHAMA AMBACHO MFUMO WAKE UTADHANI NI CHAMA CHENYE MADARAKA,NI CHAMA AMBACHO HAKINA UTANI JUU YA MAENDELEO YA WATANZANIA WOTE.KINA KEMEA NA KUFICHUA UFISADI KIASI KWAMBA NCHI INAFARIJIKA.LAKINI JAMBO LA KUSHANGAZA WALE WALIOPEWA DHAMANA YA KUWACHUKULIA HATUA ZA KISHERIA WANAFANYA MZAHA.HAO NI CCM.SASA LIMEZUKA SWALA HILI LA UKIUKWAJI WA SHERIA ZA UCHAGUZI.ILIPOTUNGWA SHERIA HII,CCM ILISHINDWA KUELEWA KUWA SHERIA HII ITATUMIWA PIA NA WATU AMBAO HAWANA UTANI KATIKA SWALA LA KULETA MAENDELEO KWA WATANZANIA (CHADEMA),CCM IMESHINDWA KUTAMBUA KUWA CHADEMA WAMEJIANDAA KUTOKOMEZA RUSHWA NA UFISADI NA HAWANA MZAHA KATIKA HILI."UKICHEKA NA NYANI UTAVUNA MABUA"SASA KITU WANACHOFANYA CHADEMA NI KUITEKELEZA ILE SHERIA ILIYOPITISHWA NA WENYEWE CCM NA KU[NENO BAYA] SAINI NA MHESHIMIWA JAKAYA KIKWETU RAIS WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.NI VEMA KUIHESHIMU SHERIA HII MAANA INA MAMLAKA YOTE. WASWAHILI WANASEMA NDEGE MJANJA HUNASA KWENYE TUNDU BOVU.BAHATI MBAYA MHESHIMIWA KIKWETE AMENASA MWENYEWE.SHERIA ICHUKUWE MKONDO WAKE.TENDWA NI MTU MSOMI NA ANAELEWA MAANA YA WAJIBU WAKE.HIVYO BILA SHAKA ANAELEWA PIA KUWA SHERIA NI MSUMENO HUKATA MBELE NA NYUMA.TENDWA ANAWAPENDA WATANZANIA PIA ANAMPENDA KIKWETE.LAKINI TENDWA HAPENDI UVUNJAJI WA SHERIA.HIVYO KWA MSAADA WA MWENYEZI MUNGU ATATENDA HAKI KWA KUTIMIZA WAJIBU WAKE.WOTE TUFAHAMU KUWA;CHADEMA WAMEWEKA PINGAMIZI SIO KWA NIA MBAYA KWA WATANZANIA BALI NI KATIKA KUTUTHIBITISHIA WATANZANIA KUWA KATIKA KUPAMBANA NA RUSHWA CHADEMA HAWAMJALI YEYOTE HATA KAMA NI MKUBWA KAMA MLIMA KILIMANJARO LAZIMA WAPAMBANE NAE TU.NA NDIVYO WANAVYOFANYA SASA.DR SLAA NDIO CHAGUO LETU WATANZANIA NA NDIO KIONGOZI BORA ATAKAYE TUFAA.HABARI NDIYO HII.DR SLAA OYEEE!
Quote
 
 
+4 #124 2010-08-31 23:29
Mwenye macho na aone. Mwenye masikio na asikie. Uchaguzi mwingine hadi 2015. Kura yako ndio italeta tofauti. Tusilalamike mbeleni. Tupige kura tukijua nini tunataka, nini tunatarajia, nini tunatazamia na nini kifanyike vipi. Kiutendaji Dr. Slaa anafaa, Kimaendeleo Dr. Slaa anafaa, kimaslahi Dr. Slaa anafaa. Mnapopiga kura pia kumbukeni watoto wenu wa sasa. Je, mtataka waishi maisha mliyoishi nyie/nyinyi! Kama unampenda mwanao au ndugu yako tafadhali kuwa makini na mahala unapopeleka kura yako. Kama unampenda ndugu yako asome, jirani yako apate maendeleo ya shule, rafiki yako apate nafasi ya kujiendeleza kimasomo basi hakuna kitu bora kama huduma za afya bora, miundombinu bora na ELIMU kwa raia wetu. Chagua mahala ambapo kuna neema, chagua mahala ambapo kuna tunu ya maendeleo na fanya maamuzi kwa kumuangalia mwanao, jirani yako, ndugu yako au rafiki yako. Matibabu bora, hospitali bora na ELIMU bora tena ya bure kwa kila mtanzania primary hadi secondary. Kenya wameweza kutoa elimu ya bure Tanzania tushindwe nini? Ukipeleka kura yako kwa wasiofaa, mafisadi na wezi wa mali yako wewe nchini basi usije kulalamika huko mbeleni kwa kuwa nafasi nyingine utapewa ifikapo October 2015 baada ya kusota kwa sana tu. Kama unajali haya ya watoto wako/wenu, wadogo zako basi sasa ni muda wa kuelewesha jamii kwani pesa za hongo kwa watu ni za msimu tu ilihali elimu yako ukiipata ni yako milele na ndio itakuwezesha kuingia katika soko la ajira na kukupa upeo wa kugundua vitu zaidi na zaidi.
Quote
 
 
+2 #123 2010-08-31 23:27
Mi natatizwa sana na watu ambao wanapoteza muda mwingi kufanya mizaha wakati nchi iko kwenye msiba mkubwa wa ombwe la uongozi.Najua pia, kuwa wengi wa hao huja kujuta sana baada ya uchaguzi, wakiishia kutoa kamasi za njaa na machozi, wakiwa wamepigika kwa nguzi ya kichangani, wakitamani tone la maji katikati ya jua kali, na huku walisahau kuwa walipewa nafasi ya kujiandalia mito ya maji safi kupitia sanduku la kura, wakaishia kuvaa Tshirt, kofia na vipimo vya pombe za kienyeji, kama ujira wa kuuza utu wao na staha za familia zao. NI UCHUNGU WA KIZEZETA!

Wakari Dr.Slaa (mtumishi wa Mungu na mtumishi mwaminifu wa watu)anaainisha hoja za ufisadi,kutokuw ajibika na ukosefu waa maadili kama visababisho vikubwa vya kudumaa kwa Tanzania yetu kiuchumi,kisias a na kijamii.Na huku akitoa mapendekezo ya kitafiti yenye kutoa maono juu ya suluhisho la matatizo tetu,watu (wenye akili za ndiyo mzee)wanajibu hoja kwa kumtuhumu kwa kuacha upadre na kuingia kwenye siasa...MZAHA WA KINDONDOCHA!

Kimsingi,kwa mujibu wa dhana na falsafa ya Mabadiliko,kila mwenye akili timamu anajua nchi hii inahitaji mapinduzi(a complete change).Maono ya Dr.Slaa ni mabadiliko ya nchi yetu kimfumo,kifikya ,kimkakati na kiutashi,hasa utashi wa kisiasa.Na hapa tunaruhusiwa kuiga kwa vitendo, kauli mbiu iliyobadilisha historia ya Marekani, YES WE CAN!

Ndani ya miaka karibia 40 CCM imeonyesha kujaribu na kushindwa KABISA kusimamia mabadiliko hayo.Nimesema imejaribu mana nafahamu kimkakati kuna wakati Tanzania ilijengewa misingi ya utengamavu hasa na waasisi wake,wakiongozw a na (Mwenye heri) Mwl.Nyerere.Misingi hii hata hivyo imeshabomoka kwa namna isiyoweza kutengenezwa na walioibomoa...DHIKI KUU!

Jakaya kikwete (nafahamu hapendi kuitwa Doctor,mnampaka zia tu) alijitokea kam nuru ya asuuhi yenye matumaini chanya, Mtanzania nikasema"I think we gat somebody". Akakuruka pale mwanzo kwa ari kasi na nguvu mpya ndani ya kiriba cha zamani.Na kama maandiko matakatifu yasemavyo kwa habari ya ubora wa dhahabu kupimwa na moto; Ghafla dhahabu kikwete ikapitishwa kwenye moto wa "List of shame" kutahamaki chali mtoto wa Bagamoyo.....NGUVU YA SODA?

Anahitajika kiongozi anayetoka kwenye mfumo tofauti kupambana na ufisadi na kuushinda.Mana ni kweli Kikwete amepambambana na ufisadi kama aimbavyo makamba kila kukicha,lakini amepambana na kushindwa vibaya....AIBU!

Inashangaza kuwa wamemaliza "style" za kutudanganya na sasa wameamua kudanganyana wenyewe kwa msemo wa kifedhuli-tuliahidi,TUMET ELEKEZA! Jibu letu sabari hii ni jepesi sana...HATUDANGANYIKI! !

Tunahitaji kiongozi mwenye "Moral Authority" na si kutisha kwa nguvu za kimtandao wala kidola.Maana yake ni rahisi tu, kwamba huwezi kupambana na ufisadi kama nawe unanukia ufisadi.

Miaka 15 ya ubunge wa Daktari Slaa,halmashaur i ya Karatu imekuwa ikipata HATI SAFI kwa mipango,mikakat i na matumizi bora na yenye kuthamini pesa za maskini wa Tanzania.kama kiongozi, Dr amejitengenezea "authority" ya kunyooshea vidole waliofuja pesa za umma.

Je kikwete anaweza kukemea matumizi mabaya ya pesa za umma huku mawaziri wake wakitembea na zahanati nne za kisasa baranbarani?(Kwa mahesabu ya Dr Slaa, kila shangingi moja linathamani sawa na zahanati nne za sh. Milioni 50 kila moja) .

Ni mengi ya kuandika lakini lamaana hapa ni nchi yetu. Si kikwete, si slaa, wala vyama vya siasa na propaganda zao.Muda wa kulaumu umeshapita.Sasa ni muda wa kufikiri kwa vitendo.Ni mihimu watu tuamue sasa kama tunayahitaji kuboresha maisha yetu.

Mfumo wa Dunia ya sasa unalazimisha siasa kutegemeza nyanja zingine katika maisha ya mwanadamu hasa wa nchi zinazoendelea(p olitical determinism).Hatahivyo, ni mihimu sasa, wasomi wetu wakasaidia kuelimisha na kupevusha fikra za wananchi wote,tuwe na ufahanu wa msingi wa masuala ya msingi hasa yahusuyo uongozi wa kisiasa wa nchi yetu, na baadaye kuoanisha kiurari unaofaa na nyanja zingine muhimu kama uchumi na sekta ya kijamii,kwa namna ya kuwezesha mfumo wa kila sekta kutekeleza wajibu wake na huku zikisaidiana na kutegemeana(Str uctural Function) katika kuwaleta watanzania Maisha Bora na sio ahadi za Bora Maisha.

Miaka mitano imepita, Mama demokrasia anatupatia tena nafasi ya kuacha uchuro wa kukaa uchi wakati nguo tunazo!

kupiga miayo wakati ghala imejaa chakula!

Ni nafasi nyingine ya kuthaminisha maisha yetu na kupanga bei ya utu wetu.

Ni nafasi nyingine Mungu ametoa ya kufanya maamuzi mazito juu ya UHAI WETU na uhai wa Taifa letu.

Kila mtu aongozwe na utashi wa moyo wake na si utashi wa fulana, mabando wala ngonjera...ukisikiliza sauti ya ndani kabisa, kwa uaminifu kabisa na huku ukijaribu kufikiri kuwa utakaloamua ndilo kusudi la MUNGU; ukifikia hatua ya tafakuri ya namna hii, hakika utagundua kwa urahisi kabisa ni nani hasa anafaa kupewa kura yako, kwa uraisi, ubunge na udiwani.

Mungu Ibariki Tanzania
Uchaguzi mwema wapendwa

Robert LENGEJU
Morogoro,Tanzan ia
Quote
 
 
+1 #122 2010-08-31 21:07
tumechoka naufisadi madini yamejaa nchini lakini hatuoni faidazake maliasili kwawingi hakuna la maana ccm wameongoza miaka nenda rudi hakuna faidayoyote uchumi unazidikushuka tu bado tunawabembeleza ccm mimi sioni haja ya kuwarudisha ccm madarakani chadema washike nao tuwaone wanaopenda matumbo yao wale jeuriyao tusidanganyike ccm wakirudi madarakani ufisadi ndoutakuwa kama malipo yawafanyakazi fedha za EPA zina watosha wlendelee kula hizo zilizobaki zikiisha wajifunze
Quote
 
 
+6 #121 2010-08-31 21:06
Mtanzania yeyote mwenye akili timamu, asiye na mtindio wa ubongo wala utumwa na udumavu wa kiakili, asome kwa uangalifu na azingatie makala hii na awashirikishe ndugu, jamaa na marafiki zake popote pale walipo..

Dr Slaa yes we can! Huyu ni mtanzania wa pili baada ya Nyerere kuchukia ufisadi kwa vitendo. Ni mtanzania wa pili kuchukia umaskini wa watanzania kwa vitendo. Ni Dr. Slaa aliyesimama na kutaja majina ya wala rushwa na mafisadi. Akatata wale wanaopinga wampeleke mahakamani. Hakuna aliyethubutu kujitokeza kumpeleka mahakamani.

Ni Dr. Slaa aliesimama bungeni kuomba posho za wabunge kupungzwa kuelekeza zaidi kwa watanzania, ni Dr.Slaa amesimama bila woga kunyosha vidole kwa matumizi mabaya ya ofisi za umma, ni Dr.Slaa amekuwa mtanzania baada ya nyerere kutoa hoja zinazomlenga mtanzania maskini, ni Dr.Slaa anaeweza kuthibiti matumizi mabaya ya ofisi za umma. Ni Dr.Slaa anaeweza kuwapa elimu bure watoto wetu pale mlimani achana na longolongo za CCM kuwatoza ushuru watoto. Waulizeni majukwaani wao nyerere aliwatoza ada? kama si kutaka watanzania waendelee kuwa mambumbumbu ni nini? kama si kutaka watanzania tuendeleee kuwa watumwa ni nini?

Ni Dr. Slaa anaeongelea treni ya umeme kwenda kigoma, Dodoma, Tabora, na Mwanza. Waulize mpango wao ccm kama si kuwapa wahindi wanaoleta mabehewa ambayo mababu zetu walitumia wakati wa ukoloni. Hawa hawatutakii mema. Hawana tofauti na akina Carl Peters. Ni Dr.Slaa anaeongelea mfumko wa bei -nani hajajua dola leo hii ni sawa na tsh 1500. kwani kuna tofauti gani kati ya Tanzania, Kenya na Ethiopia, ambako ni chini ya 20 ya pesa yao? kwanini sisi tuna kasoro gani kuwa maskini kiasi kwamba mtu asafiri kutoka ethiopia kuja Dar es salaam afike kabla ya mtu anayetoka Kariakoo kwenda Mwenge?

Ni Dr.Slaa anaweza kuzuia wizi wa matrilion ya pesa kutoka migodi yetu ya buzwagi, geita, bulyankulu, tulawaka,nzega, tanzanite hawa wameshindwa kwa sababu ni washirka wakubwa na wameruhusu wizi huo. Ni Dr.Slaa anaeweza kuwalipa wafanyakazi zaidi ya shinilingi 350 achana na CCM ambayo imeshindwa kusimamia maliasili ambazo zingeliwapa wafanyakazi kima cha chini kinachokidhi mahitaji yao.

Ni Dr.Slaa anaeweza kusimamia mashirika ya jamii kuleta tija achana na CCM wanaofyonza michango yetu kule, kwani haya mashirkia yameshindwa nini kuwajengea nyumba wanachama wake? Mbona kwingine yameweza? Ni Dr.Slaa anweza kuongoza nchi bila woga, kwa utawala wa kweli wa sheria bila kuwaonea watu wala bila kulipiza visasi.

Ni Dr. Slaa ambae amepanga kubadili katiba ili Rais afuite matakwa ya walio mwajiri ambao ni wananchi. Waulize CCM hata kama mtu kaiba anapewa mda arudishe pesa? Hivi inaingia akilini kweli? hata kama mtu anasemwa ni fisadi hakuna hatua yoyote -naomba niwape heko ITV kwa kuturejeshe kwenye hotuba za mwalimu -katika hotoba yake moja alisema waziri mmoja kule uingereza aliandikwa kidogo tu gazetini juu ya kashfa, yule waziri alijiuzulu na waziri mkuu hata hakumjibu bali aliteua mtu mwingine.

CCM hawawezi hayo? eti wanataka ushahidi. Nani kawambia rushwa tule wawili harafu tutoe vielelezo? Tunaiona rushwa kwa matokeo yake. Matengenezo ya barabara ya bilion 200, baada ya siku mbili imeharibika. Kwanini usimfukuze waziri na katibu wake wa wizara kwanza? CCM hawawezi! eti wanataka vielelezo! Ni

Dr.Slaa anaeweza kufanya hayo si tumeona mnazi mmoja aliwataja mafisadi wote! hapo akiwa ni mbunge tu. Je akiwa rais watakimbia nchi nawambia tumpe miaka mitano tu awakurupue muone moto utakavyowaka? Tutapata dawa, tutapata shule za bure, tutapata madawati-jamani hivi kweli karne ya leo watoto wanasoma wamekaa chini? we must be serious! Hivi kweli dunia ya leo watu wanavuliwa nguo njiani kwenda Mwanza, Shinyanaga, Tabora, kigoma, mbeya,lindi, mtwara kwa sababu ya usafiri wa malori?

Nani asiye jua madakitari wetu wengi bingwa wapo botswana wakati hapa kwetu watu wanakufa tu? Nani asiejua matatizo ya umeme, maji, makazi, maradhi, yanavyotutesa? Nani asiejua wakulima wetu wasivyokuwa na masoko ya mazao yao? Nani asiejua asilimia 85 ya watanzania wanatumia vibatari au makoroboi kama mwanga? nani asiejua tunavyonyonywa na hawa wakoloni waliokuja kuchukua kila kitu??

Jamani wafanyakzi, wakulima, na wanafunzi ni jukumu letu kupeleka habari hata kama vyombo vyetu vya habari ni vya hao hao. Hawasemi tu ukweli, hata wao ni maskini na wanakubali kupitia vyombo vyao tuendeee kusema piga na shavu la kushoto.

Ni Dr. Slaaa, mzalendo wa kweli na sio kwa ajili ya sifa, anaweza kutuvusha tulipo. Nchi hii ni maskini na umaskini wenyewe ni wa kujitakia. Tanzania ni tajiri tuna kila kitu mito, maziwa, national parks, migodi, mazao ya misitu, na kila kitu. Naona huruma wenzangu waliokunywa maji ya bandari.

Hivi kuna mtu hajui mapolisi wanalala kwenye vibanda vya mabati? Hivi kuna ambao hawajui mapolisi watendaji wanalipwa laki moja? wamekosa nini hawa? Jamani tuache woga inawezekana. Mbona Kenya wameweza? Mbona malawi wameweza?Mbona zimbabwe wameweza? Mbona Ghana wameweza? Kufanya mabadiliko sahihi, inawezakana na nafasi ni hii tuitumia. Tumtume Dr.Slaa kuwakurupusha wezi wote na atuwekee katiba sawa. Huo ndio msingi wa yote. Ni Dr. Slaa asiyeogopa kuwepo na mgombea binafsi. CCM hili hawaliwezi.

Jamani 2010 hakuna kudanganyika! enough is enough. Acheni kudanganyika. Nawatamani watu wa kule Mara -hakuna kura inaibiwa zote zinasimamiwa. Tukibadilika inawezekana tena ni rahisi. Peleke ujumbe huu kwa marafiki, ndugu, jamaa, babu na bibi yako kule kijiji kwa simu kama ipo, au kwa njia ya posta, mradi tu wale jamaa waliochoka kuishi wasiikwapue barua wakidhani ni hela.
Quote
 
 
+3 #120 2010-08-31 20:36
Uchaguzi mkuu wa mwaka huu ni muhimu sana kuliko wakati mwingine wowote katika historia ya nchi yetu.Inawezekana tumefanya majaribio mengi na utani wa kina aina kama vile rais aliyepata zaidi ya kura asilimia 80 anasema hata yeye hajui kwanini watanzania wengi wamekuwa masikini.Sasa ni nafasi nzuri sana kwa kila raia wa nchi hii kufanya maamuzi magumu kwa kuwachagua viongozi wanaojua matatizo yetu ya msingi,watu waadilifu wenye upeo wa kuona mbali.Lakini kuhusu suala la CHADEMA na pingamizi lao,nathani wanatimiza haki yao lakini kimsingi hamna kitakachofanyik a,kwani ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ni sehemu ya rais,na hilo ni moja ya mambo yanayotakiwa kufanyiwa mabadiliko na serikali nyingine tofauti na ya CCM.Pia nawashauri CHADEMA wajipange vizuri kwani ni chama kinachoonekana kuwa mbadala wa CCM siku za usoni,waeleze mipango na sera zao zitakazolenga kutatua matatizo ya wananchi ambayo yameshindwa kutatuliwa na CCM kwa zaidi ya miaka 40 sasa.
Quote
 
 
+3 #119 2010-08-31 19:56
Mi natatizwa sana na watu ambao wanapoteza muda mwingi kufanya mizaha wakati nchi iko kwenye msiba mkubwa wa ombwe la uongozi.Najua pia, kuwa wengi wa hao huja kujuta sana baada ya uchaguzi, wakiishia kutoa kamasi za njaa na machozi, wakiwa wamepigika kwa nguzi ya kichangani, wakitamani tone la maji katikati ya jua kali, na huku walisahau kuwa walipewa nafasi ya kujiandalia mito ya maji safi kupitia sanduku la kura, wakaishia kuvaa Tshirt, kofia na vipimo vya pombe za kienyeji, kama ujira wa kuuza utu wao na staha za familia zao. NI UCHUNGU WA KIZEZETA!

Wakari Dr.Slaa (mtumishi wa Mungu na mtumishi mwaminifu wa watu)anaainisha hoja za ufisadi,kutokuw ajibika na ukosefu waa maadili kama visababisho vikubwa vya kudumaa kwa Tanzania yetu kiuchumi,kisias a na kijamii.Na huku akitoa mapendekezo ya kitafiti yenye kutoa maono juu ya suluhisho la matatizo tetu,watu (wenye akili za ndiyo mzee)wanajibu hoja kwa kumtuhumu kwa kuacha upadre na kuingia kwenye siasa.

Kimsingi,kwa mujibu wa dhana na falsafa ya Mabadiliko,kila mwenye akili timamu anajua nchi hii inahitaji mapinduzi(a complete change).Maono ya Dr.Slaa ni mabadiliko ya nchi yetu kimfumo,kifikya ,kimkakati na kiutashi,hasa utashi wa kisiasa.

Ndani ya miaka karibia 40 CCM imeonyesha kujaribu na kushindwa kusomamia mabadiliko hayo.Nimesema imejaribu mana nafahamu kimkakati kuna wakati Tanzania ilijengewa misingi ya utengamavu hasa na waasisi wake,wakiongozw a na Mwenye heri Mwl.Nyerere.Misingi hii hata hivyo imeshabomoka kwa namna isiyoweza kutengenezwa na walioibomoa.

Jakaya kikwete (nafahamu hapendi kuitwa Doctor,mnampaka zia tu) alijitokea kam nuru ya asuuhi yenye matumaini chanya, Mtanzania nikasema"I think we gat somebody". Akakukuruka pale mwanzo kwa ari kasi na nguvu mpya ndani ya kiriba cha zamani.Ghafla dhahabu kikwete ikapimwa na moyo wa "List of shame" kutahamaki chali mtoto wa Bagamoyo!

Alihitajika kiongozi anayetoka kwenye mfumo tofauti kupambana na ufisadi na kuushinda.Mana ni kweli Kikwete amepambambana na ufisadi kama aimbavyo makamba kila kukicha,lakini amepambana na kushindwa vibaya!

Tunahitaji kiongozi mwenye "Moral Authority" na si kutisha kwa nguvu za kimtandao wala kidola.Maana yake ni rahisi tu, kwamba huwezi kupambana na ufisadi kama nawe unanukia ufisadi.

Miaka 15 ya ubunge wa Daktari Slaa,halmashaur i ya Karatu imekuwa ikipata HATI SAFI kwa mipango,mikakat i na matumizi bora na yenye kuthamini pesa za maskini wa Tanzania.kama kiongozi, Dr amejitengenezea "authority" ya kunyooshea vidole waliofuja pesa za umma.

Je kikwete anaweza kukemea matumizi mabaya ya pesa za umma huku mawaziri wake wakitembea na zahanati nne za kisasa baranbarani?(Kwa mahesabu ya Dr Slaa, kila shangingi moja linathamani sawa na zahanati nne za sh. Milioni 50 kila moja) .

Ni mengi ya kuandika lakini lamaana hapa ni nchi yetu. Si kikwete, si slaa, wala vyama vya siasa na propaganda zao.Muda wa kulaumu umeshapita.Sasa ni muda wa kufikiri kwa vitendo.Ni mihimu watu tuamue sasa kama tunayahitaji maisha bora ama la.

Mfumo wa Dunia ya sasa unalazimisha siasa kutegemeza nyanja zingine katika maisha ya mwanadamu hasa wa nchi zinazoendelea(p olitical determinism).Hatahivyo, ni mihimu sasa, wasomi wetu wakasaidia kuelimisha na kupevusha fikra za wananchi wote,tuwe na ufahanu wa msingi wa masuala ya msingi hasa yahusuyo uongozi wa kisiasa wa nchi yetu, na baadaye kuoanisha kiurari unaofaa na nyanja zingine muhimu kama uchumi na sekta ya kijamii,kwa namna ya kuwezesha mfumo wa kila sekta kutekeleza wajibu wake na huku zikisaidiana na kutegemeana(Str uctural Function) katika kuwaleta watanzania Maisha Bora na sio ahadi za Bora Maisha.

Miaka mitano imepita, Mama demokrasia anatupatia tena nafasi ya kuacha uchuro wa kukaa uchi wakati nguo tunazo!

kupiga miayo wakati ghala imejaa chakula!

NI nafasi nyingine ya kuthaminisha maisha yetu na kupanga bei ya utu wetu.

Ni nafasi nyingine Mungu ametoa ya kufanya maamuzi mazito juu ya UHAI WETU na uhai wa Taifa letu.

Kila mtu aongozwe na utashi wa moyo wake na si utashi wa fulana, mabando wala ngonjera...ukisikiliza sauti ya ndani kabisa, kwa uaminifu kabisa na huku ukijaribu kufikiri kuwa utakaloamua ndilo kusudi la MUNGU, ukifikia hatua ya tafakuri ya namna hii, hakika utagundua kwa urahisi kabisa ni nani hasa anafaa kupewa kura yako, kwa uraisi, ubunge na udiwani.

Mungu Ibariki Tanzania
Uchaguzi mwema wapendwa

Robert LENGEJU
Morogoro,Tanzan ia
Quote
 
 
+2 #118 2010-08-31 19:28
Mi natatizwa sana na watu ambao wanapoteza muda mwingi kufanya mizaha wakati nchi iko kwenye msiba mkubwa wa ombwe la uongozi.

Wakari Dr.Slaa (mtumishi wa Mungu na mtumishi mwaminifu wa watu)anaainisha hoja za ufisadi,kutokuw ajibika na ukosefu waa maadili kama visababisho vikubwa vya kudumaa kwa Tanzania yetu kiuchumi,kisias a na kijamii.Na huki akitoa mapendekezo ya kitafiti yenye kutoa maono juu ya suluhisho la matatizo tetu,watu (wenye akili za ndiyo mzee)wanajibu hoja kwa kumtuhumu kwa kuacha upadre na kuingia kwenye siasa.

Kimsingi,kwa mujibu wa dhana na falsafa ya Mabadiliko,kila mwenye akili timamu anajua nchi hii inahitaji mapinduzi(a complete change).Maono ya Dr.Slaa ni mabadiliko ya nchi yetu kimfumo,kifikya ,kimkakati na kiutashi,hasa utashi wa kisiasa.

Ndani ya miaka karibia 40 CCM imeonyesha kujaribu na kushindwa kusomamia mabadiliko hayo.Nimesema imejaribu mana nafahamu kimkakati kuna wakati Tanzania ilijengewa misingi ya ukuaji hasa na waasisi wake,wakiongozw a na Mwenye heri Mwl.Nyerere.Misingi hii hata hivyo imeshabomoka kwa namna isiyoweza kutazamika.

Jakaya kikwete (nafahamu hapendi kuitwa Doctor,mnampaka zia tu) alijitokea kam nuru ya asuuhi yenye matumaini chanya, Mtanzania nikasema"I think we gat somebody". Akakukuruka pale mwanzo kwa ari kasi na nguvu mpya ndani ya kiriba cha zamani.Ghafla dhahabu kikwete ikapimwa na moyo wa "List of shame" kutahamaki chali mtoto wa Bagamoyo.

Alihitajika kiongozi anayetoka kwenye mfumo tofauti kupambana na ufisadi na kuushinda.Mana ni kweli Kikwete amepambambana na ufisadi kama aimbavyo makamba kila kukicha,lakini amepambana na kushindwa vibaya.

Tunahitaji kiongozi mwenye "moral. Authority" na si kutisha kwa nguvu za kimtandao wala kidola.Maana yake ni rahisi, huwezi kupambana na ufisadi kama nawe unanukia ufisadi.

Miaka 15 ya ubunge wa Daktari Slaa,halmashaur i ya Karatu imekuwa ikipata hasi safi kwa mipango,mikakat i na matumizi bora na yenye kuthamini pesa za maskini wa Tanzania.kama kiongozi, Dr ana "authority" ya kunyooshea vidole waliofuja pesa za umma. Je kikwete anaweza kukemee matumizi mabaya ya pesa za umma huku mawaziri wake wakitembea na zahanati nne za kisasa kwenye nyumba za starehe?(Kwa mahesabu ya Dr Slaa, kila shangingi moja linathamani sawa na zahanati nne za sh. Milioni 50 kila moja) .

Ni mengi ya kuandika lakini lamaana hapa ni nchi yetu. Si kikwete, si slaa, wala vyama vya siasa na propaganda zao.Ni mihimu watu tuamue sasa kama tunayahitaji maisha bora ama la.

Mfumo wa Dunia ya sasa unalazimisha siasa kutegemeza nyanja zingine katika maisha ya mwanadamu hasa wa nchi zinazoendelea(p olitical determinism).Hatahivyo, ni mihimu sasa, wasomi wetu wakasaidia kuelimisha na kupevusha fikra za wananchi wote,tuwe na ufahanu wa msingi wa masuala ya msingi hasa yahusuyo uongozi wa kisiasa wa nchi yetu, na baadaye kuoanisha kiurari unaofaa na nyanja zingine muhimu kama uchumi na sekta ya kijamii,kwa namna ya kuwezesha mfumo wa kila sekta kutekeleza wajibu wake na huku zikisaidiana na kutegemeana katika kuwaleta watanzania Maisha Bora na sio ahadi za Bora Maisha.

Mungu Ibariki Tanzania
Uchaguzi mwema wapendwa.
Quote
 
 
+3 #117 2010-08-31 19:22
IF you dont have mental slavery pass this to your inbox list,and post to your village and you can expand as you wish -yes we can.

" Dr SLAA, yes we can, huyu ni mtanzania wa pili kwa nyerere kuchukia ufisadi kwa vitendo, ni mtanzania wa pili kuchukia umaskini wa watanzania kwa vitendo, ni Dr. Slaa aliesimama mnazi mmoja kutaja majina ya wala rushwa na mafisadi, ni Dr. Slaa aliesimama bungeni kuomba posho za wabunge kupungzwa kuelekeza zaidi kwa watanzania, ni Dr.Slaa amesimama bila woga kunyosha vidole kwa matumizi mabaya ya ofisi za umma, ni Dr.Slaa amekuwa mtanzania baada ya nyerere kutoa hoja zinazomlenga mtanzania maskini, ni Dr.Slaa anaeweza kuthibiti matumizi mabaya ya ofisi za umma, ni Dr.Slaa anaeweza kuwapa elimu bure watoto wetu pale mlimani achana na longolongo za sisiemu kuwatoza ushuru watoto waulizeni majukwaani wao nyerere aliwatoza ada? kama si kutaka watanzania waendelee kuwa mambumbu ni nini? kama si kutaka watanzania tuendeleee kuwa watumwa ni nini? ni Dr. Slaa anaeongelea treni ya umeme kwenda kigoma,dodoma,t abora, mwanza, waulize mpango wao sisiem kama si kuwapa wahindi wanaoleta mabehewa mababu wetu waliyotumia wakati wa ukoloni hawa hawatutakii mema, hawa hawana tofauti na akina kalupeters, ni Dr.Slaa anaeongelea mfumko wa bei -nani hajua dola leo hii ni sawa na tsh 1500. kwani kuna tofauti gani tanzania na kenya, ethiopia, ambako ni chini ya 20 ya pesa yao? kwanini sisi tuna kasoro gani kuwa maskini kiasi kwamba mtu asafiri kutoka ethiopia kuja dar es salaam afike kabla ya mtu anatoka kariakoo kwenda mwenge? ni Dr.Slaa anaweza kuzuia wizi wa matilion ya pesa kutoka migodi yetu ya buzwagi, geita, bulyankulu, tulawaka,nzega, tanzanite hawa wameshindwa kwa sababu ni washirka wakubwa wameruhusu wizi huo, ni Dr.Slaa anaeweza kuwalipa wafanyakazi zaidi ya shinilingi 350 achana na sisiemu inayoshindwa kusimamia maliasili ambazo zingeliwapa wafanyakazi kima cha chini kinachokizi mahitaji, ni Dr.Slaa anaeweza kusimamia mashirika ya jamii kuleta tija achana na sisiemu wanafyonza michango yetu kule kwani haya mashirkia yameshindwa nini kuwajengea nyumba wanachama wake? mbona kwingine yameweza? ni Dr.Slaa anweza kuongoza nchi bila woga, kwa utawala wa kweli wa sheria bila kuwaonea watu, bila kulipiza visasi, ni Dr,Slaa ambae amepanga kubadili katiba ili Rais afuite matakwa ya waliemwajiri ambao ni wananchi, waulize sisiemu hata kama mtu kaiba anapewa mda arudishe ela? hivi inaingia akilini kweli? hata kama mtu anasemwa ni fisadi hakuna hatua yoyote -naomba niwape heko ITV kwa kuturejeshe kwenye hotuba za mwalimu -katika hotoba yake moja alisema waziri mmoja kule uingereza aliandkwa kidogo tu gazetini kwamba amekutwa na [NENO BAYA] yule waziri alijiuzulu na waziri mkuu hata hakumjibu bali aliteua mtu mwingine, sisiemu hawawezi hayo? eti wanataka ushahidi nani kawambia rushwa tule wawili harafu tutoe vielezlezo? tunaiona rushwa kwa matokeo yake -barabara bilion 200 siku mbili imeharibika kwanini usimfukuze waziri na katibu wake wa wizara kwanza? hawawezi sisiemu eti wantaka vielelezo -ni Dr.Slaa anaeweza kfanya hayo si tumeona mnazi mmoja aliwataja wote! hapo ni mbunge je akiwa rais watakimbia nchi nawambia tumpe miaka mitano tu awakurupue muone moto utakavyowaka? tutapata dawa, tutapata shule za bure, tutapata madawati-jamani hivi kweli karne ya leo watoto wanasoma wamekaa chini? we must be seriuos stupid??????? hivi kweli leo watu wanavuliwa nguo njiani kwenda mwanza, shinyanaga, tabora, kigoma, mbeya,lindi, mtwara kwa sababu ya usafiri wa malori???????? fikiaria ni wewe umevuliwa nguop mbele ya mama mkwe wako>??? harafu unaipiagia kula sisiemiu???? nani asie jua madakitari wetu wengi bingwa wapo botswana/ HAPA watu wanakufa tuu, nani asiejua matatizo ya umeme, maji, makzai, maradhi, yanavyotutesa? nani asiejua wakulima wetu waivyokuwa na masoko ya mazao yao, nani asiejua asilimia 85 ya watanzania wanatumia vibatari au makoroboi kama mwanga, nani asiejua tunavyonyonywa na hawa wakoloni waliokuja kuxchuua kila kitu?? jamani wafanyakzi, wakulima, wanafunzi ni jukumu letu kupeleka habari hata kama vyombo vyetu vya habari ni vya hao hao, hawasemi ukweli hata wao ni maskini na wanakubali kupitia vyombo vyao tuendeee kusema piga na shavu la kushoto, ni Dr. Slaaa dr wa ukweli sio dr wa misifa anaweza kutuvusha tulipo, nchi hii ni maskini wa kujitakia, Tanznia ni tajiri tuna kila kitu mito, maziwa, national parks, migodi, mazao ya misitu, na kila kitu? naonea huruma wenzangu waliokunywa maji ya bendari hivi kun mtu hajui mapolisi wanalala kwenye vibanda vya mabati? hivi kuna mabae hajui mapolisi watendaji wanalipwa laki moja,? wamekosa nini hawa? jamani tuache woga inawezekana mbona kenya wameweza? mbona malawi wameweza?mbona zimbabwe wameweza?mbona ghana wameweza? mbona tunwea kufnya mabadiliko sahihi, inawezakana na nafasi ni hii tuitumia, tunamtuma Dr.Slaa kuwakurupusha kuweka katiba sawa huo ndio msingi wa yote, ni Dr. Slaa asiopgopa mgo,mbea binafsi hawa sisiemeu wanaogopa hwawezi kabisaaaaaaaaaa a, jamani 2010 hakuna kudanganyika, enough is enough achani kudanganyika, nawatamani watu wa kule mara -hakuna kura inaibiwa zote zinasimamiwa, tukibadilika inawezekana tena ni rahisi, peleke ujumbe huu kwa babu na bibi kule kijiji kwa simu kama ipo, au posta, au gari ili mradi wale jamaa waliochoka kuishi wasi ikwapue barua wakidhani ni ela mara daabda ya kuwavua nguo abiria, hii inatia aibu miaka 49 ya uhuru? karne ya 21 shida zote hizi inakera inaudhi na haivumiliki hawa sio wenzetu baba mbunge mjomba katibu wa wizara, biinamu waziri mkuu, wao wao wao na wanataka watiu wasisome ili wasiwe kuhoji wasome wao tuuuuuuuuuuuuuu uuu, wengine 40% ya ada kima cha chini laki 2, utalipaje hiyo 40% tunaonewa tunadhulumiwa, hawtundei haki -yaani wamefika sehemu wansema vijisenti ntamani yule mgaya angepata hivyo vijisent pengine asingejitoa mhanga inauma, hao hao wameandikwaaaaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaa lakini bado wanangangania hawakumbuki maneno ya mwalimu kuhusu wazir wa uengereza, mkubwa nae amewachia tuuuuuuuuuuuuuu uuu si washikaji acha tule good tym jamani tunaumia pisheni wanaoweza waongoze? jamani ifike sehemu ubinadamu uwepo, tupige kura na ninwashauri tongotongotongo zetu zitatuumiza haya Dr.Slaa huyoooooooooooo ooooooooooooooo ooooooooooooooo ooo mpeni shoka amalize misitu tuanze upyaaaaaaaaaaaa aaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaaaaaaaaaaa aaaaaa bila hakuna kitu,

Mtanzania mwenye haki ya kikatiba kutoa mawzo yake bila woga tuangane jamani sisi wote ni wana sisiemu lakini maji yamevuka shingo hapa hamna kitu kura tunampa Slaaa lakini tunabaki kuwa sisiemu cha msingi maendeleo bwana kuna ndani hamna kitu
Quote
 
 
0 #116 2010-08-31 18:32
Quoting Weka Chachala:
Inavyoontyesha Chadema wanaanza kuweweseka juu ya ahadi za JK. Wajue JK ni Rais aliye madarakani kwa hiyo kutoa ahadi kwa wanachi wake ni kitu cha kawaida. Na wao Chadema watoe ahadi lukuki kama wanaweza na siyo kulialia kama watoto wa paka waliokimbiwa na mama yao. Slaa kama ameasi upadiri, kisha kumtelekeza Rose Kamili na kuchukua dogo dogo ingine hivi ataaminikaje mtu mzinzi kiasi chake? Kuoa na kuacha kwake ni kawaida. Hatuhitaji kuwa na Rais wa namna hiyo. Arudi Mbulu kwa wambulu wenzake akachunge mbuzi. Roger1

JAMANI GUEST HOUSE ZIKO WAPI? HUYU MISS CHACHALA ANAHITAJI MWANAMME WA SHUGHULI ILI KUMZINDUA MAANA KALEWA NA CHUKI BINAFSI! TUNACHOTAZAMA HAPA NI JINSI YA KUMPATA MTANZANIA MZALENDO WA KWELI, ATAKAYETUONYESH A DIRA YA MAENDELEO YA KWELI YA KIUCHUMI. SASA KAMA AKILI YAKO IMEDUMAA KIASI KWAMBA HUNA HOJA ZA KUCHANGIA, UTUJULISHE MAPEMA ILI TUKUTAFUTIE MWANAMME WA KUKUZINDUA ILI UAMKE KUTOKA USINGIZINI, KULIKO KUTULETEA UTUMBO NA UFUKUNYUKU HAPA!
Quote
 
 
-3 #115 2010-08-31 18:21
"FOR THOSE WHO ARE NOT PREPARED, ARE PREPARING TO FAIL"
THE WHOLE OPPOSITION HAVE FAILED US FOR NOT PREPARING US KISAWASAWA.
I COMMEND CCM FOR THE GOOD MATAYARISHO THAT THEY HAVE DONE SO FAR.
who did know that Dr. SILAHA would contest the presidency?let him try next time!BTW iam not for CCM,i dont see any good strategy tht will see us sail through!!!
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner