MwanzoContactsEmail
Home
BOOKMARK THIS PAGE
Masha ang'oa vitasa ofisi ya Mbunge Mwanza  Send to a friend
Tuesday, 30 November 2010 01:46

Frederick Katulanda, Mwanza
ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, amehamisha vifaa mbalimbali vya ofisi ya Bunge Jimbo la Nyamagana, kwa madai kuwa alivinunua mwenyewe kipindi uongozi wake. Akizungumza na Mwananchi jana, Mbunge wa Nyamagana, Ezekiel Wenje, alisema baada ya kutoka Bungeni alikwenda kuingia katika ofisi hiyo, lakini baada ya kukabidhiwa alikuta vitasa vya mlango, simu ya mezani picha ya Rais na samani za kukalia vikiwa zimechukuliwa.
 
Kwa mujibu wa Wanje, baada ya kufuatilia aliambiwa kuwa vifaa hivyo viliondolewa na Masha kwa madai kwamba, alivinunua kwa fedha zake mwenyewe.

“Nimefuatilia kwa DAS (Katibu Tawala wa Wilaya) nikaambiwa amechukua Masha, nikafuatilia kwa Katibu Tawala wa Mkoa yeye alijibu kuwa naye alifuatilia suala hilo kupitia kwa Das na kupewaa majibu kama yangu, sasa sijajua ni kwa nini, ninavyojua ofisi haipaswi kukosa samani kwa vile kuna fedha za kununulia vitu hivyo,” alisema.

Kwa Upande wake, Masha alikiri kuondoka na vitu hivyo na kwamba, asingeweza kuacha vifaa vyake binafsi katika ofisi hiyo.

Masha alisema vifaa alivyoondoka navyo ni vile tu ambavyo ni mali yake.

“Wakati naingia hapa nilikuta ofisi ikiwa na kiti kimoja na meza tu, vifaa vingine niliweka vyangu, kama kompyuta na meza zake, simu na samani nyingine kulingana na mahitaji yangu,” alisema Masha.
Alisema Wenje anapaswa kuwasiliana na ofisi ya mkuu wa wilaya, ili kupewa vifaa vya ofisi hiyo ambavyo yeye aliviondoa alikuwa havitumii kwa vile wao wanajua vilipo.

“Jamani vifaa vya ofisi anapaswa kuuliza ofisi ya mkuu wa wilaya, sasa kama anataka nimwachia na vyangu binafsi, mie nimetoa vyangu…hivyo vya ofisi vipo, nadhani amefika na kukutana na kiti kimoja na meza vile vingine vilivyokuwemo pia vilikuwa mali ya ofisi,” alieleza Masha.

Hata hivyo, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza (RAS), Doroth Mwanyika, hakuweza kupatikana kuzungumzia suala hilo kutokana na kuwa nje ya ofisi, lakini ofisa mmoja wa ofisi yake alithibitisha kuwepo kwa malalamiko ya Wenje na kwamba, yalikuwa yakishughulikiwa.

Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Thursday, 07 April 2011 11:31
 

Comments 

 
0 #65 2010-12-17 14:18
hahahahaha MR Masha hujatumia busara hata kama umevinunua kwa fedha zako ungeonyesha mchango wako katika ofisi hiyo uliyoiacha...vipi ungenunua ambulance, zima moto vipi ungetunyang'anya pia?
Quote
 
 
+1 #64 2010-12-03 14:20
ok Marsha, unataka kutuambia nini hapa?? Hata vitasa? jamani utu uzima utoto? hata hukuogopa elimu yako? Ukirudi Madarakani utavirudisha??? Usitukane mamba kabla hujavuka mto kaka, Umri wako bado unadai na Elimu yako hujiatumia ipasavyo,. Punguza ghadhabu na hasira
Quote
 
 
0 #63 2010-12-03 14:11
Mimi sishangai Ya Masha kungo'a vitasa, kwani ukifikiria hela alizokuwa anapata na thamani ya vitasa jibu unalo. Ushauri wangu kwake mtu yeyote awae dhalimu kwa mambo madogo atakuwa dhalimu kwa makubwa pia. Aige mfano kwa mzee Ndesamburo kule Mawenzi Hosptal
Quote
 
 
+15 #62 2010-11-30 14:07
Hii ya kung'oa vitasa haingii akilini hata kidogo. Hivi ni kweli Masha unakiri kabisa kuwa umeondoa vitu ulivyonunua? Nini mchango wako kwa wananchi? Unataka kutwambia kuwa na Sitta angekosa ubunge angeenda kubomoa ile ofisi aliyozindua JK kule Urambo?

Nafikiri unahitaji uangalizi wa karibu huenda kukosa ubunge kumekuathiri kisaikolojia.

Nakuomba chonde chonde JK, hata kama unampenda vipi Masha, ukimchagua hata ukuu wa wilaya Wananchi hatutakuelewa hata kidogo. Kati ya watendaji waliokusababish ia upate kura chache na Masha yumo.

Hii aibu aliyoitafuta mwenyewe kamwe haitofutika maishani mwake.

Amuulize mzee Malecela kwanini mpaka leo Watanzania wanaangalia kila anachokifanya na kukitenda. Pamoja na kuomba radhi, dhambi ya maneno yake ya dharau bado inamtafuna mpaka leo.

Hebu tueleze Masha,umekaa bungeni miaka mitano. Posho ya jimbo kama sikosei ni Tshs 500,000 x 12months x 5years = Tshs 30,000,000/=

Hizo pesa zote umefanyia kitu gani mpaka leo unang'oa mpaka vitasa? Tutakukumbuka kwa lipi wananchi wa jimbo la Nyamagana?

MASHA UMEJIHARIBIA NA HUFAI KABISA KWA UONGOZI HATA WA NYUMBA KUMI.
Quote
 
 
+11 #61 2010-11-30 13:33
Je huko ni kutibu majeraha ya uchaguzi au ni kuongezamaumivu ??
Quote
 
 
+7 #60 2010-11-30 13:24
Bwana mdogo Masha, umri wako bado mdogo sana. Mpaka utapokuwa mzee utakuwa umevunja vitasa vingapi? Vipi na kitasa cha wizara ya mambo ya ndani umeshavunja? Mrema Lyatonga alikikuta na akakiacha pamoja na kwamba alifukuzwa.
Quote
 
 
+6 #59 2010-11-30 13:17
yapo mapungufu kwa DAS na Masha.

Katika mazingira ya kistaarabu, Masha alitakiwa kufanya makabidhiano ya ofisi katika mazingira ya wazi kabisa. Kuonyesha kilicho chake na mali za ofisi.

DAS alitakiwa kutunza inventory ya vifaa vya ofisi. Yeyote anayeingia na kutoka anatakiwa kuona na kujua kilichopo kwa uwazi kabisa.
Quote
 
 
+4 #58 2010-11-30 13:12
Heeeeeee,huyo MASHA kumbe mpuuz hivyo!!Ushamba gan huo wa kutoa vitu vya ofisi eti kisa umeshindwa!!Wan anchi hawakutaki hasira za ki[NENO BAYA] za nini sasa!Kama hizo samani anadai kanunua yeye na atueleze fedha za serikali za kununua vifaa vya ofisi alizipeleka wapi??Sio analeta u[NENO BAYA] wake kama GUMEGUME!Shiiii it...
Quote
 
 
+7 #57 2010-11-30 13:02
shame on u, which kind of lawyer are u?, kwa kuwa umekosa ubunge hata picha ya mh.raisi unatoa, inamaana hautatoa ushirikiano wowote?, nini mchango wako kwa watu wa jimbo hilo kama hautajari mazingiara mazuri kwa aliyechukua kiti chako?,wapi tunakwenda kama watu watakuwa wabinafsi kama huu?
Quote
 
 
+5 #56 2010-11-30 12:57
Hao ndio wateule wetu.
Quote
 
 
+4 #55 2010-11-30 12:40
masha amekuwa sio mfano wa kuigwa tena inawezekana hata kugombea ubunge alilazimishwa.. kiongozi gani huyo asiye tambua demokrasia nini,, kama kafanya hivyo sizani,, hata anaweza kusalimiana na wenje.. inaonekana kabisa.. alimfanyia fitina kwenye suala la uraia.. anahitaji kubadilika na kuamini siasa kuna mawili kushindwa au kushinda.. hainiingii akilini afadhali angetoa samani za ofis.. anatoa hadi vtasa.. HUKO NI KUJISHUSHIA HESHIMA..
Quote
 
 
+2 #54 2010-11-30 12:20
Masha hata kama ulinunua wewe vitasa hukupaswa kuvitoa kwanjia hiyo,bali unjesubiri Mbunge mteule aingie katika ofisi hiyo kisha umweleze kwa udhibitisho kuwa vitasa ni vyako hapo angeamua kukurusu au kukulipa garama ulizotumia,wala umma usinge shangaa
Quote
 
 
+4 #53 2010-11-30 12:01
Hata picha ya Rais umenunua kwa pesa yako , kweli ni vituko, angekuwa mchagga storia ingekuwa ndefu. Mungu atalipa hapa hapa duniani. Mkumbusheni kingine alichosahau ni zile kadi za CCM alizowapa wananchi aje azichukue ni mali yake.
Quote
 
 
+8 #52 2010-11-30 12:00
Kwa mfano huo aliouonyesha Masha kwa jamii inaelekea wazi kabisa siku ambayo Chama cha upinzani kikishinda ktk matokeo ya urais 2015....Wana CCM watavuruga na kuchukua hata mali ambazo ni za wananchi na kwa ajili ya maendeleo ya Taifa ili mradii tu kuwakomoa......Kama kweli ni vyake angejaribu kuchukua njia ya kiungwana kidogo ili aweze kurudishiwa na mkuu wa wilaya aadabishwe kwani kwa vyovyote kuna fungu walipata kuhusu manunuzi ya thamani hizo za ofisi.........
Quote
 
 
+3 #51 2010-11-30 11:58
Mie binafsi nadhani ni wakati wa wanasiasa kutumia busara zaidi masha anachotakiwa kujua ni kwamba kushindwa uchaguzi huu si mwisho wa maisha yake ktk siasa. Asioneshe umma dhahili kuwa ameuchukia kiasi hicho kwani baada ya muda wa wenje kuisha anaweza kuchaguliwa.

Hivi Mhe.alipoambiwa kuwa na mwl.kuwa subiri, je kama angekuwa na hurka ya kukosa subira si angejikuta amehama chama ama kuwa na mgogoro na viongozi wenzake serikalini? Mbona alitulia na mwisho wake si amekuwa rais wa nchi yetu?

Subira na uvumilivu ni mihimili mikubwa ktk maisha ya binadamu yeyote.

Mungu ibariki Tanzania; amina
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner