CWT Arusha yahofia uhakiki wanafunzi hewa

Rais wa chama cha walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba

Muktasari:

Akizungumza ofisini kwake jana, Kaimu Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Arusha, Andrew Ngazu  alisema chama kinamtaka  mkurugenzi wa jiji  kurudia uhakiki kwa sababu uamuzi uliotolewa  ulikuwa wa binafsi na haukufuata utaratibu maalumu.

Arusha. Chama cha Walimu Tanzania (CWT) Mkoa wa Arusha, kimetaka uhakiki wa wanafunzi hewa jijini hapa kuanza upya kwa madai  ya uwapo wa uamuzi wa chuki dhidi ya wakuu wa shule.

Akizungumza ofisini kwake jana, Kaimu Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Arusha, Andrew Ngazu  alisema chama kinamtaka  mkurugenzi wa jiji  kurudia uhakiki kwa sababu uamuzi uliotolewa  ulikuwa wa binafsi na haukufuata utaratibu maalumu.

“Tunamuunga mkono Rais Johh Magufuli kuhakiki shule zenye wanafunzi hewa, ila tunapinga kwa nguvu zote uhakiki uliofanyika   Arusha,” alisema Ngazu na kuongeza: “Tunaamini umefanywa na maofisa wa elimu kwa chuki dhidi ya walimu wa shule, hali iliyosababisha kuonewa kwa baadhi ya walimu huku shule zenye wanafunzi hewa zikiachwa.” Kaimu Katibu wa CWT, Nurueli Kavishe alisema mpaka sasa wana ushahidi  unaojitosheleza kuwa mwajiri wao ambaye ni mkurugezi wa jiji  hakutumia takwimu zilizopo.

Katibu wa CWT Wilaya ya Arumeru, Joyce Kizaji aliwataka wakurugenzi kuacha kuwatisha walimu kuhusu Mwenge kwani siyo lazima.