MwanzoContactsEmail
Home Habari Uchumi na Biashara FFU yazuia wanafunzi kwenda Ikulu
BOOKMARK THIS PAGE
FFU yazuia wanafunzi kwenda Ikulu  Send to a friend
Thursday, 10 March 2011 20:47

Nora Damian
KIKOSI cha Kutuliza Ghasia cha Jeshi la Polisi (FFU) jana kilitawanya maandamano ya wanafunzi wa baadhi ya shule za msingi na sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam waliokuwa wakielekea Ikulu kupinga ongezeko jipya la nauli za daladala.

Kundi la kwanza la wanafunzi hao lilijikusanya katika Viwanja vya Mnazi Mmoja majira ya mchana na kuanza maandamano hayo yaliyokuwa na lengo la kumfikishia ujumbe Rais Jakaya Kikwete wa kutoridhishwa na ongezeko hilo la nauli. Kundi jingine la wanafunzi lilianzia maandamano hayo katika Uwanja wa Karume.

Mwandishi wa habari hii alipofika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja aliwakuta wanafunzi hao wakijipanga kuanza maandamano hayo huku wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali. Baadhi ya mabango hayo yalisomeka: ‘Kama ni maji ya pilipili, hayawezi kuwa suluhisho la migomo.’

Baadhi ya wanafunzi walisema wameamua kupinga nauli hiyo mpya kwa maandamano ili kuishinikiza serikali iifute wakitaka kurejeshwa kwa ile ya zamani ya Sh100 ili kuwapunguzia mzigo wazazi wao kuwasomesha.
“Sisi wengine kwa siku tunapanda magari matatu hadi kufika shule na hapo bado hujala. Sasa kwa hali hii kweli tutasoma?" Alihoji mmoja wa wanafunzi hao.

Mwanafunzi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Habib Juma alisema nauli ya Sh150 kwa mwanafunzi ni kubwa mno kuimudu akisema kipato cha  wazazi wengi ni duni na baadhi yao wanashindwa hata kutoa michango mbalimbali ya shule.

Hata hivyo, jitihada za wanafunzi hao kufikisha ujumbe wao Ikulu ziligonga mwamba baada ya kudhibitiwa na FFU muda mfupi tu baada ya kuingia barabarani.Askari hao waliokuwa na pikipiki walitanda barabarani na kuwatawanya wanafunzi hao na baadaye waliwashikilia wanafunzi wawili wa kiume baada ya wenzao kukimbia. Wanafunzi hao walipakiwa kwenye gari la polisi na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Msimbazi.

Nauli hizo mpya za daladala zilizotangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), wiki iliyopita zilianza kutumika rasmi jana.Ofisa Mfawidhi wa Sumatra katika Kanda ya Dar es Salaam, Conrad Shio alisema nauli hizo zimegawanywa katika makundi matatu kwamba wanafunzi watatozwa Sh150 kwa safari, kundi la pili ni njia zenye nauli moja ya Sh300 na la tatu ni la njia zenye nauli zaidi ya moja na kwamba nauli hizo zimeongezeka kwa Sh50 katika nauli za awali, katika kila safari moja.

Shio alitoa mfano akisema kwa njia ambayo abiria wake walikuwa wanatozwa nauli ya Sh250 kwa safari, sasa watatozwa Sh300.Alisema katika Kanda ya Mashariki nauli ya juu zaidi itakuwa Sh1,700 kwa safari kati ya Kigamboni na Pembamnazi, eneo ambalo awali nauli yake ilikuwa Sh1,300.

Sumatra imeongeza nauli hizo baada ya kupokea maombi ya wamiliki wa mabasi mwishoni mwa mwaka jana wakilalamikia kupanda kwa gharama za uendeshaji.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
+1 #26 2011-03-12 08:24
kuna mwandishi mmoja zamani aliwahi andika kitabu kiitwacho PEPO ZA MA[NENO BAYA]!! kama sijakosea alikuwa akiitwa Harrison Mwakyembe! sina hakika kama ni huyu waziri wa sasa ama mwingine kitabu hiki kina kila kitu kihusianacho na kizazi tulicho nacho sasa!
Quote
 
 
+2 #25 2011-03-12 05:44
Hii yote ni matatizo ya uongozi bora kama mnanunua bajaji moja dola za kimarekani 5000Us hivi ni miakamingapi tanzania inaitaji kurekebishwa awamu zote zimeshindwa,Nja a,maladhi,Maish a kuwa magumu kwa asilimia 90 ya watanzania.ANGALIA WATOTO WANAOSOMA PRIVATE NA SHULE ZA SIRIKALI WATAKUTANA WAPI? KWANI PRIVATE NAZO ADA MLIMA UKIGUSA UNWEKUFA KWA SHINIKIZO LA DAMU
MAONI.tunaiomba sirikali iwekeze shule zake na ipige marufuku shule za private kupandisha ada ovyo ili eti list tuballance kamavipi binafsisha shule kwa wawekezaji.MIGODI,MAFUTA,U RANIUM,ALMAS,NI KEL,TANZANITE,W ATALII.cheki utajili huo.??????????????????duuuu noma aibu????????jama
Quote
 
 
+2 #24 2011-03-12 03:39
Mimi nasema serikali iaache kununua mashangingi na badala yake iwekeze kwenye mabasi ya wanafunzi mbona inawezekana? Hawa viongozi wetu watoto hao hawapandi mabasi wanachukulia na madereva ambao bila hata aibu anaacha gari inanguruma ili apate A/C wakati waziri yupo kwenye mkutano ni matumizi mabaya ya fedha.
Quote
 
 
+1 #23 2011-03-11 20:14
Haya bhana CHADEMA wakisema ukweli wanaambiwa kuwa wanawashinikiza wananchi kuondoa amani mmmhhh sasa hawa wanafunzi ni viongoz wa chadema????
Kiukweli JK nchi imekushinda, tufike mahali tuache unafiki na tuseme ukweli nchi imekushinda...
Quote
 
 
+2 #22 2011-03-11 19:01
Viongoziwa Tanzania musipoangalia nchi mutaipeleka pabaya,mifano mushaiona katika baadhi ya nchi, kwa hio ukimuona mwenzio ananyolewe na wewe tia maji, yale mambo yakuambiwa serikali ya Tanzania bado ni changa, hayo hakuna tena, muheshimiwa Raisi Kikwete usipoangalia basi nchi utaipeleka pabaya, halafu unakaa unasema chadema wanavuruga amani mimi nasema ccm nchi imewashinda kuiongoza na nyinyi ndio munavuruga amani ya nchi sio chadema, mwenye macho haambiwi tazama,,76%ya watanzania wanashida kubwa ya kimaisha
Quote
 
 
+3 #21 2011-03-11 18:05
Suruhisho hapa n kupatikana kwa mabasi ya wanafunzi, serikali wekezeni katika mabasi msaidie watoto wafike shule kwa urahisi, pili maandamano kwenda ikulu mgewaacha wakaenda maana rais mwenyewe hata hayuko huko, kwa nini msiandamane kwenda kwenye wizara husika, hapo tujifunze namna ya kutatua matatizo
Quote
 
 
+1 #20 2011-03-11 17:36
Mini binafsi sina imani sana na uongozi wetu wa Tanzania.Kipindi cha nyuma waliahidi wange toa mabasi yakusaidia wanafunzi yakowapi?au ndo machenga ya macho.Nirahisi sana kuuzunguka mbuyu nasio kuukumbatia.Vijana komaeni na kazeni buti mtafanikiwa.Kinacho niudhi Tanzania ukidai haki wanasema unahamasisha uvunjifu wa amani.What is this by then?
Quote
 
 
+1 #19 2011-03-11 16:15
Sio tu kudai kupunguziwa nauli ya daladala, bali serikali (iwe ya jiji, mkoa au serikali kuu) ina wajibu wa kutumia kodi za walipakodi vizuri na kuwapatia usafiri wa bure wanafunzi wa shule za msingi na sekondari (kwa maana uliolipiwa na walipa kodi). Kwa maneno mengine, usafiri wa bure (mabasi yanayomilikiwa na serikali kwa ajili ya wanafunzi au hata kuwapa vocha za kupandia daladala) ni haki ya msingi ya wanafunzi. Kwa bahati mbaya wadanganyika wanafikiri kudai hivyo ni dhambi. Kama serikali haiwezi kufanya hivyo basi iache kukusanya kodi au jukumu hilo wamwachie mtu anayeweza. keep it up wanafunzi - inatia faraja na matumaini kuona mmeanza kutambua haki zenu na kufanya jitihada za kuzidai.
Quote
 
 
-2 #18 2011-03-11 15:26
kwa nini tumlaumu kikwete wakati mwenye zamana hiyo ni waziri?anaye usika ni waziri tuache kumlaumu raisi kwa mengine.hapo wa kulaumiwa ni waziri
Quote
 
 
+1 #17 2011-03-11 15:24
kwa kweli tukiangalia uharisia wa mambo watoto wa maskin watazida kuteseka na kushindwa kufikia lengo la kusoma na kuwapata viongozi bora watakao lijenga taifa hili.suala la kuipandisha nauli kwa wanafunzi ni dalili ya unyanyasaji kwao.serikari ilitazame upya hili suala.
Quote
 
 
+1 #16 2011-03-11 13:46
serikali iliondoa kodi ya kuingiza magari makubwa nchini ili kurahisisha usafirishaji na kupunguza gharama za usafiri 2010/11. wenye akili ztu tulisema hii ni kuwapa ahueni matajiri wakubwa kwani masikini hawezi kununua scania mil 200/=
sasa tunaona gharama za usafirishaji zilivyoshuka, JK baba kamua baba.
mimi sina la kujutia kwasababu sikuchagua sisiemu 2010
Quote
 
 
+1 #15 2011-03-11 12:57
Mimi naona Kikwete nchi imemshinda, sasa hawa watoto nao ni CHADEMA??,
Hata kikwete kusema jaman nimeshindwa nao ni ujasiri tutamheshimu kwa hilo, au la akijifanya Kingang'anizi yaweza tokea ya Misri na Tunisia hapa TZ.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Quote
 
 
+5 #14 2011-03-11 11:38
Mh. Mkapa alikaa madarakani Miaka kumi na nauli ilikua sh. 50 mpaka anatoka ikulu huyu Mkwere kaingia tu hata hajamaliza miaka yake nauli ime triple...mpaka 2015, hali itaku tata sana!!
Quote
 
 
+4 #13 2011-03-11 10:55
Serikali makini zote duniani hutumi a maandamano yoyote ya amani kama darasa ili kujua hisia za umma juu ya mambo muhimu yanayowaathiri. Kwa serikali kandamizi zisizotaka kujifunza kuzima maandamano au kutokuwapo kwa maandamano ndio kipimo cha utulivu wa nchi. Viongozi wake huwa hawataki kusikiliza na kujua hisia za wananchi moja kwa moja bali kupitia kwa usalama wa taifa ambao mara nyingi huwadanganya viongozi wao kwa kuwapa hali tofauti na zilivyo hisia za umma. Ajabu kabisa ujio wa IGP msomi na mwenye exposure ya mahali kwingine duniani kama Said Mwema (alikuwa Interpol b4 becoming TZ - IGP)haijasaidia nchi badala yake ndo Jeshi la Polisi limezidisha kupiga na kuua raia
Quote
 
 
+4 #12 2011-03-11 10:47
naona ,taifa linakoelekea ni hatari,serikali iache ubabaishaji,yaa ni,hakuna inachoweza kufanya ikasifiwa! vyote ubabaishaji, viongozi wenyewe wanapingana kauli!!!!!!!! ila yote haya yanatokana na misimamo yetu wananchi kwa kuchagua viongozi kwa mazoea na ushabiki, matokeo yake wanaboronga. nashauri tuwe tunawapa muda ,akishindwa kutekeleza majukumu na ahadi zake, tunampiga chini...tuanze na uchaguzi ujao...kuanzia chini dawa ndo hiyo!
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner