MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Babu aenda msibani chini ya ulinzi
BOOKMARK THIS PAGE
Babu aenda msibani chini ya ulinzi  Send to a friend
Wednesday, 27 April 2011 21:50

Mussa Juma, Samunge
MCHUNGAJI Ambilikile Mwasapila anayetoa tiba ya magonjwa sugu huko Samunge Loliondo, juzi jioni aliondoka hapa kwenda Babati, Manyara kuhudhuria mazishi ya mtoto wake huku safari yake hiyo ikiratibiwa na Serikali na akipewa ulinzi mkali wa maofisa usalama na polisi.

Aliondoka Samunge saa 12:20 jioni na gari la Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro akiwa na maofisa hao wa usalama, polisi na wasaidizi wake.
Kabla ya kuondoka Samunge, watu mbalimbali walikuwa wamejitolea kumpatia usafiri mchungaji huyo lakini walizuiwa kutokana na sababu za kiusalama.

"Tulikaa kama kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya, tukaona ni busara tuchukue jukumu la kumsafirisha Mchungaji hasa kutokana na sababu za kiusalama," alisema ofisa mmoja mwandamizi wa serikali wilayani hapa.
Alisema mchungaji huyo atalindwa akiwa msibani na atakaporejea Samunge.

Warundi, Wakenya, Waganda wakwama
Zaidi ya raia 100 kutoka Kenya, Burundi na Uganda, wamekwama Samunge kutokana na kusitishwa kwa tiba hiyo hadi Ijumaa.
Licha ya hatua hiyo ya kusitishwa kwa huduma kutangazwa mapema, maelfu ya watu, wakiwamo raia hao wa kigeni, waliendelea kumiminika Samunge kupata matibabu hayo.

Profesa Hakizimana  Godefroid kutoka eneo la Muyumba, Burundi akiwa na ujumbe wa watu saba alisema wametumia siku saba kufika hapa na kwamba hatua hiyo imewasikitisha."Gari hili tumekodi kutoka Burundi hadi hapa, tunasikitika sana kukuta hakuna huduma na tunaambiwa ilitangazwa hapa Tanzania pekee kitu ambacho si kizuri," alisema Godefroid.

Alisema kutokana na taarifa ya tiba ya Mwasapila kusambaa karibu nchi zote za Afrika na nje ya bara,Serikali ilipaswa kutoa taarifa za kusitishwa kwa huduma hiyo katika balozi zake zote zilizopo nchini."Tumeondoka Burundi tukijua kuwa huku Tanzania tiba inatolewa tena tulijua hata siku za Pasaka tiba inaendelea. Taarifa zingesambazwa mapema tusingekuja sasa," alisema Godefroid.

 Ofisa Uhamiaji ambaye yupo Samunge, Suleiman Saanane akishirikiana na polisi, juzi na jana walitumia muda mwingi kuwaelimisha raia hao wa nchi jirani juu ya kusitishwa kwa tiba hiyo na namna Serikali inavyoisimamia. Raia wa Kenya na Uganda, Peter Kimath na Joram Batengi, walishauri Serikali ya Tanzania kuipa hadhi tiba inayotolewa na Mchungaji Mwasapila wakisema, inawaponya watu na inavyoonekana, maelfu ya watu watafika Samunge.

 "Hatuoni kama huyu mzee anapewa usaidizi ila tunachoona ni Serikali kukusanya kodi tu hapa ya magari na helikopta. Sasa kama wanapata fedha nyingi waitambue rasmi hii tiba na kuweka utaratibu mzuri," alisema Kimath.  Batengi aliishauri Serikali kuboresha mazingira ya Samunge hasa barabara na eneo la tiba ili watu wanaotoka nchi za nje waamini kwamba tiba hiyo inaponya.

"Uganda wengi wanajua tiba hii na kuna ambao wanasema kuwa wamepona ila ukifika hapa huwezi kuamini kama tiba hii ni nzuri kwani mazingira ya hapa siyo mazuri na hata njia za kufika hapa ni mbaya sana," alisema Batengi.

 Raia hao wanalazimika kubaki Samunge hadi Ijumaa siku ambayo Mchungaji Mwasapila atarejea na kuendelea kutoa tiba.  Mchungaji Mwasapila anatarajiwa kurejea Samunge leo baada ya kushiriki katika mazishi ya mtoto wake Jackson (43), yaliyofanyika jana.

Msaidizi wa Mchungaji huyo, Frederick Nisajile aliliambia gazeti hili jana kuwa baada ya kurejea, wataanza maandalizi ya kuchemsha dawa ambayo itatumika Ijumaa.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #25 2011-04-29 01:00
Acheni kulumbana na mammbo ya kishirikina cha ajabu hapa, mbona huyu babu kashindwa kumponya mtoto wake sasa mna maneno gani ya kudanganyana hapo, jiulizeni wenyewe jibu ni hilo.
Quote
 
 
+1 #24 2011-04-28 19:48
Quoting Mahfoudh Said:
HIKI KIKAFIRI CHA LOLIONDO LAZIMA KIPIGWE RISASI KIULIWE ILI HABARI ZA LOLIONDO ZIISHE, GAZETI LA MWANANCHI HALINA HABARI ZA MAANA ZA KUANDIKA

Haya uliyoyaongea ndio yanachafua dini ya uislamu...BABU kakukosea nini wewe kwani..sawa unamuita kafiri kwa kuwa wewe ni mtu safi sio..ungekuwa ni mtu safi ungemtusi mwenzio...embu kuwa mtu mwenye akili na sio kuongea mambo ya kuchafua jamii...
Quote
 
 
0 #23 2011-04-28 19:46
usilolijua ni kama usiku wa giza...mlitaka mzungu au falme za kiarabu zigundue dawa ndio muamini??acheni mawazo mgando na kufikiri kwa kutumia tumbo badala ya kichwa...babu toa dozi,watakukuba li muda ukifika...
Quote
 
 
0 #22 2011-04-28 19:20
Dawa ya Babu inaponya. Wachawi Msiopenda watu wanapopona kajitundikeni.

Pesa tunalipa sisi tunaokwenda, nyie msiokwenda kinachowauma nini? mshindwe sana

Hongera serikali kumlinda Babu. Kwanza ametuletea maendeleo Loliondo
Quote
 
 
-5 #21 2011-04-28 15:57
HIKI KIKAFIRI CHA LOLIONDO LAZIMA KIPIGWE RISASI KIULIWE ILI HABARI ZA LOLIONDO ZIISHE, GAZETI LA MWANANCHI HALINA HABARI ZA MAANA ZA KUANDIKA
Quote
 
 
+2 #20 2011-04-28 12:40
Quoting mtanzania:
Quoting Smartboy:
"Serikali ilipaswa kutoa taarifa za kusitishwa kwa huduma hiyo katika balozi zake zote zilizopo nchini" Godfroid Hakizimana

Hivi, SERIKALI ya TZ imesha- declare kuwa Loliondo kwa babu kuna tiba RASMI? wadau nisaidieni jibu.


The so called "tiba ya babu" bado haijawa declared kama tiba rasmi. Inanitia kichefuchefu sana serikali inavyotumia fedha ya walipa kodi kumhudumia mganga wa kienyeji. Ole wa viongozi vipofu wanaoliongoza taifa kuwaendea waganga wa kienyeji na wenye mapepo ya utambuzi - 1Nyakati 10 : 13 -14

Sibora hata hiyo pesa itumike kumsapoti babu, kuliko inavyotumika na mafisadi kwa manufaa yao na mahawara zao! shit
Quote
 
 
+3 #19 2011-04-28 12:05
WEWE UNAYEPINGA DAWA YA NAFIKILI UNA MATATIZO YA AKILI.HIVI HOSPITALI SI KUNA DAWA YA MAGONJWA YA MOYO LAKINI WATU WANAKUFA VILEVILE KUNA DAWA YA MARALIA WATU SI WANAKUFA ACHA WATU WANYE WEWE KAJIPIME KAMA UNA MAGONJWA SUGU NA WEWE NENDA
Quote
 
 
-4 #18 2011-04-28 11:56
Jamani watanzania acheni u[NENO BAYA], hii dawa ya babu ni mazingaombwe matupu, lakini kwa kuwa wengi wa watanzania ni mbumbumbu basi wanajiendea tu Loliondo, tatizo watu wako frustrated na maisha kwa hiyo wako radhi hata wakiambiwa wale Kinyesi wanakula,Embu angalieni Watanzania wenzangu ni watu wangapi wamejitokeza na kusema wana tiba ya magonjwa sugu? wako wengi sana sasa kwa nini msijiulize Interest yao kubwa ni nini,huu ni utapeli zindukeni,Na msione eti viongozi mbali mbali wameenda kunywa basi mkaona ni dili, hii ni sisa wandg zangu hakuna kitu hapo,kule mnaenda kupata tu infections, we angalia kila mtu anatumia kikombe hichohicho,watu maelifu kwa maelfu,Huu mchezo wa kikombe ulitokea Nigeria watu walikufa kama Kuku wa Kideri, kwa hiyo madhara yake tutayaona very soon
Quote
 
 
+4 #17 2011-04-28 11:54
Binafsi ninaona kwamba babu yupo sawa sawa. Tatizo linabaki kwetu sisi watumiaji. Kwa nini kama mwanzoni ulikuwa mgonjwa wa Ukimwi na vipimo unavyo pamoja na nyaraka zinazoonyesha kuathirika kwako, baada ya kwenda kwa babu na kupata kikombe ukapona hukuenda kuhakiki tena hospitali?
Quote
 
 
-3 #16 2011-04-28 11:32
Quoting A:
Ziara hizi kwa huyu aitwae Babu zitamalizika mara tu baada ya watu kuelimika kuwa tiba hii na mazingaombwe tu na wala hakuna lolote jingine ma watu watapoanza kutumia akili zao na kuanza kudodosa na kutaka kuoneshwa wale waliokuwa na maradhi suguu kama ukimwi, cancer, ugonjwa wa akili na mengineo kuwa kwelikweli wamepona kwani mpaka leo hii bado hakuna anaeuliza wala kutaka kufahamu kitu. Kuna wale wanaoamini kuwa waliotangaza kupona kuwa ilikuwa dili tu kuwa watangaze hivo ili watu waamini. Baada ya kujuwa ukweli ndipo itapokuwa mwisho wa ziara hizo na kuwa mambo hayo kubakia katika historia na wala hakuna jenginelo. Hilo haliko mbali.


wewe sema yote uliyo nayo moyoni kwako. Hatulazimiki kukusikiliza wewe wala kufuata ushauri wako wa ki[NENO BAYA]. Sisi tuliofaidika na uponyaji wa Babu na kuondokana na taabu tulizokuwa nazo kwa siku nyingi, ndio tunaojua umuhimu wake na tunaiunga mkono Serikali kwa uamuzi wake wa kuratibu tiba hii iliyosaidia wengi. Hatuna haja ya kukuletea wewe ushaihidi wetu wa kupona kwa kuwa hatuna uhusiano na wewe na ugonjwa ni jambo binafsi linalomhusu mgonjwa na familia yake. Kwani ulishaletewa vyeti vingapi vya kupona vya Muhimbili???? Acheni kudodosa mambo binafsi ambayo hayawahusu. BABU Mungu akulinde na azidi kukubariki. Hao wanaosubiri siku za mwisho wanazoimba kila siku, ni zao wenyewe. GOD BLESS YOU BABU AMBI!!!
Quote
 
 
+1 #15 2011-04-28 11:03
Binafsi sina tatizo na huduma ya babu,kwani inahusu mambo ya imani km mwenyewe anavyosema,ila sijaelewa kuna nini nyuma ya pazia hadi serikali kuwa karibu zaidi na bubu wa loliondo na kutowatilia maanani makaka,madada wa vikombe na vijiko wanaoendelea kujitokeza?ni kwa kuwa babu anachangia mapato makubwa serikalini au kwa kuwa watu wanapona!
Quote
 
 
0 #14 2011-04-28 10:39
halazimishi mtu kwenda kwa babu ww kama una wasi wasi na tiba inayotolewa kwa bubu usinde acha wenye imani zao wakapate tiba acheni kutishia watu ati cku za mwisho kasema nan msiwe kama thomaso tatizo ibani waumini wengi hawaend wala maandiko hawasomi wanajiropokea tu
Quote
 
 
-2 #13 2011-04-28 09:59
Wewe unaelewa biblia au unajifanya BUSH LAWYER? Tatizo lako ni fikra potofu uliyoambukizwa na wakoloni walioleta dini huku wakibeza dini zetu za asili eti ni za mashetani. Kwa taarifa yako, biblia imetumika kufanya uhalifu dhidi ya watu weusi kuliko kitu kingine chochote kile. Mimi nakushangaa, unaitaje wenzio shetani wakati hata hiyo biblia imejaa ushetani? Acha u[NENO BAYA] kushabikia vitu usivyovijuwa.Quoting charles:
Hivi lakini hamwelwewi kuwa Biblia inasema wazi kuwa huzi ni suku za mwisho?.Maandiko yanasema waziwazi kuwa waalim na manabii wa uongo watatumiwa na shetani na kufanya hata moto ushuke kutoka mbinguni uje kwa wanadamu ili watu wadanganyike,hi lo alilisema Yesu mwenyewe.Dawa na moto kushuka kutoka mbinguni lipi kubwa?.Jamani tusome maandiko,hizi ni siku za mwisho.

Quoting charles:
Hivi lakini hamwelwewi kuwa Biblia inasema wazi kuwa huzi ni suku za mwisho?.Maandiko yanasema waziwazi kuwa waalim na manabii wa uongo watatumiwa na shetani na kufanya hata moto ushuke kutoka mbinguni uje kwa wanadamu ili watu wadanganyike,hi lo alilisema Yesu mwenyewe.Dawa na moto kushuka kutoka mbinguni lipi kubwa?.Jamani tusome maandiko,hizi ni siku za mwisho.

Quoting charles:
Hivi lakini hamwelwewi kuwa Biblia inasema wazi kuwa huzi ni suku za mwisho?.Maandiko yanasema waziwazi kuwa waalim na manabii wa uongo watatumiwa na shetani na kufanya hata moto ushuke kutoka mbinguni uje kwa wanadamu ili watu wadanganyike,hi lo alilisema Yesu mwenyewe.Dawa na moto kushuka kutoka mbinguni lipi kubwa?.Jamani tusome maandiko,hizi ni siku za mwisho.
Quote
 
 
0 #12 2011-04-28 09:34
Nadhani Suala la ugonjwa ni la mtu mwenyewe kwani hata kwa mganga wa kienyeji bado watu wanaenda. Jambo la babu ni la kawaida na ndo maana hata imani ni ya mtu mwenyewe na si ya jumuiya flani. Hata mganga mwenye leseni ya kazi hiyo pia serikali yaweza kumpa ulinzi ipasavyo kama tajiri mwenye hela zake. Tuweni wapole kwa suala la Imani ya mtu
Quote
 
 
+2 #11 2011-04-28 09:25
HUNA HAJA YA KUTAA DAWA AU KUIKUBALI. KAMA NI HIVYO WEE KAA KIMYA TU.
ANAYEIKUBALI NI YEYE NA USIMHUKUMU MWINGINE KWA KITU USICHOKIJUA.

WATANZANIA AMKENI.

MAMBO YA SIKU ZA MWISHO NI GIZA KWA HIYO WENGINE MSIDANGANYE WATU KWA KUTUMIA NENO WAKATI HAMLIJUI BALI UBABAISHAJI TU.

MWACHENI BABU NA BIBI WAFANYE AMBACHO MUNGU KAWAPA.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner