MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Siasa Slaa awasilisha ushahidi kumbana Chenge
BOOKMARK THIS PAGE
Slaa awasilisha ushahidi kumbana Chenge  Send to a friend
Friday, 08 July 2011 21:32

Geofrey Nyang’oro

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa ameendelea kumkalia kooni Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na sasa amewasilisha serikalini uchambuzi wa ushahidi utakaosaidia kumtia hatiani mwanasiasa huyo, dhidi ya tuhuma za ufisadi katika ununuzi wa rada.

Dk Slaa aliwasilisha waraka wa uchambuzi wa kisheria kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mashtaka Nchini (DPP), Eliezar Feleshi, akiweka wazi kwamba Serikali ya Tanzania ina mamlaka ya kufanya uchunguzi dhidi ya uhalifu kwa watuhumiwa ambao ni raia wa Tanzania.

Katika waraka huo ambao Mwananchi umeuona, Dk Slaa ameweka wazi kuwa kazi iliyofanywa na Ofisi ya Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO) ililenga kubaini makosa ya kuvunja sheria nchini Uingereza na kwamba Tanzania ilipaswa kufanya uchunguzi wake katika jambo hilo.

“Kimsingi SFO ilikuwa inafanya upelelezi kuhusiana na uvunjifu wa sheria chini ya mamlaka yao yaani Uingereza, Wales na Ireland ya Kaskazini. Makosa ya ufisadi wa rada yaliyofanywa na Watanzania (na mawakala wao) ni makosa dhidi ya Sheria za Tanzania,” inaeleza sehemu ya waraka huo na kuongeza:“Ni  kwa msingi huo mimi niko “on record” ndani ya Bunge na nje ya Bunge kuitaka Serikali ya Tanzania nayo kuanzisha upelelezi wa kwake kwa mujibu wa Sheria za Tanzania kwani walioibiwa ni Watanzania na fedha zilizoibiwa ni za Watanzania”.

Dk Slaa alisema hakuna mantiki ya upelelezi wa ufisadi uliofanyika Tanzania kuachiwa mamlaka nyingine.
Aliliambia Mwananchi jana kuwa tayari amekamilisha uchambuzi huo na kwamba waraka husika ulikuwa katika mchakato wa kupelekwa kwa Feleshi.

Hatua hiyo ya Dk Slaa ni kuitika wito wa DPP ambaye juzi, alimtaka kuwasilisha nyaraka zenye ushahidi dhidi ya watuhumiwa wa rada  serikalini ili ziweze kufanyiwa kazi, akieleza kuwa ushahidi alionao hautoshi kumtia Chenge hatiani kama atafikishwa mahakamani.

Msimamo wa Feleshi unaungwa mkono na Mwanasheria Mkuu wa serikali, Jaji Fredrick Werema, ambaye pia alimtaka Dk Slaa asaidie kupelekea ushahidi kwa kuwa sheria inaruhusu.Kadhalika, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah pia alishaweka bayana kwamba taratibu za kuwasilisha ushahidi ofisini kwake ziko wazi, hivyo kumtaka Dk Slaa kutumia njia hizo ili ushahidi huo akaufanyie kazi.

"Kama Chadema wanao (ushahidi), kama alivyoeleza Dk Slaa, walete tutaulinganisha na ushahidi tulionao ili tuone kama unatosha kuitetea kesi hiyo mahakamani," alisema Dk Hoseah

Ambana Chikawe
Katika waraka huo, Dk Slaa alisema kwamba Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe alilidanganya Bunge pale aliposema kwamba Serikali haina ushahidi wa kumfikisha Chenge mahakamani.Alisema Serikali kupitia kwa AG iliandikiwa barua na SFO yenye Kumb.

Na SPCO1/D/MC ya Machi 21, 2008, iliyosainiwa na msimamizi wa kesi hiyo, Mathew Cowie kuhusu suala la rada.“Attorney General (Mwansheria Mkuu wa Serikali),  ndiye Mshauri Mkuu wa Serikali kwa masuala ya kisheria, na hivyo ni dhahiri barua hiyo Serikali inaifahamu. Kutokana na barua hiyo, ni dhahiri Chikawe alipotosha Bunge na Taifa kwa kusema kuwa Serikali haina ushahidi,” unasema waraka huo.

Alisema barua ya SFO inawataja wahusika wote kwa upande wa Tanzania na kwamba miongoni mwao ni Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati mkataba huo uliposainiwa.“SFO wanaeleza fika kuwa nyaraka za mkataba zilikuwa moja kwa moja chini ya usimamizi na maelekezo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali”.

Barua/Fax ya Mark Simpkins wa SPS  ya tarehe 30 Agosti, 1997 ni ushahidi dhahiri wa ushiriki wa Andrew Chenge,”anaeleza DK Slaa katika barua yake na kuongeza:“DPP anao mkataba wenyewe wenye kuonyesha dhahiri “Financial Arrangement” na kama hana Ofisi ya Mwanasheria Mkuu inao.


Dk Slaa aliweka bayana kuwa nyaraka zote husika ziko serikalini na kwamba wajibu wa raia mwema ni kutoa taarifa ya uhalifu kwa mujibu sheria zetu mbalimbali.“Isitoshe hisia za ufisadi huu hazikuanzia kwa raia tu bali hasa kwa chombo chenye wajibu wa kuisimamia Serikali yaani Bunge kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 63(2),(3),” unasema waraka huo na kuongeza:“Raia na wabunge hatuna vyombo vya dola. Kazi yetu ni kutoa mashaka (criminal suspicion na msingi wa suspicion hiyo). Kazi ya kupeleleza ni ya DPP na Dola”.


Kwa mujibu wa Feleshi kuna uwezekano wa nyaraka alizonazo Dk Slaa kuwa na ushahidi unaotofautiana na ushahidi uliopo serikalini hivyo kuwasilisha nyaraka hizo, kutasaidia kufanikisha jambo hilo.“Sheria zetu zina utaratibu mzuri wa kupokea ushahidi. Sheria ya Mwenendo wa Kesi na Makosa ya Jinai, kifungu cha Saba na ile ya kupambana na rushwa, kifungu cha 39, zinaeleza bayana kuwa mtu mwenye ushahidi anaweza kuuwasilisha kwenye vyombo vinavyohusika,” alisema Feleshi.

Feleshi alitoa kauli hiyo baada ya kutakiwa na gazeti hili azungumzie kauli ya Dk Slaa aliyoitoa Jumatano wiki hii kuwa Serikali ina ushahidi dhidi ya watuhumiwa wa ufisadi wa rada ila imeamua kuwalinda.

Sakata la Rada

Jumatano wiki hii Dk Slaa alisambaza ripoti ya SFO yenye kurasa 11 na kusisitiza kuwa ushahidi huo unatosha kumtia Chenge hatiani.Dk Slaa alisambaraza ripoti hiyo kufuatia kauli ya Chikawe aliyedai Serikali haina ushahidi wa kuwafikisha watuhumiwa wa kashifa ya rada mahakamani.

Kitendo cha Dk Slaa kukubali ombi hilo la Serikali kinabadili sura na msimamo waliokuwa nao yeye pamoja na chama chake wa kutowasilisha ushahidi na badala yake kufanya maandamano nchi nzima kuueleza umma kuhusu tuhuma hizo za rada.

Dk Slaa alisema amefikia hatua ya kukubali kuandaa na kuwasilisha ushahidi huo kufuatia kauli ya DPP iliyotaka afanye hivyo kwa maelezo kuwa unaweza ukawa una tofauti na ule ambao Serikali inao.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
 

Comments 

 
0 #49 2011-07-13 01:52
Quoting Marc Israel Katala:
its a shame, narudia tena ni aibu!!! mpaka mnasaidiwa na nchi ilikotokea rada kurudishiwa hela!! halafu mnasema hamna ushahidi wa kumtia mahakamani!? kama haitoshi mpaka upinzani wanawaletea ushahidi, nasema ni aibu kwa serikali na kiongozi wa nchi!!! Tanzania inasikitisha!! nini maana ya uongozi????! Tanzania tunaongozwa na kundi la watu wenye hofu!! nasema inauma!!


Usifikirie hao waingereza wana wema na sisi, hiyo ni chambo ndugu yangu ya kutusambaratish a ili wao watimize fikra zao za kutuvuruga. Ndugu hilo ni kaa la moto toka uingereza jifanyeni kulishabikia muone kitakachotokea.
Quote
 
 
0 #48 2011-07-13 01:25
Ndugu zangu watanzania huu si wakati wa kurudia yale yaliopita kama hakuna mapya tuimarishe nchi yetu kwani haya tumeyasikia sana, cha kufanya sasa ni kuziba yale mashimo yaliyofanya hayo yatokee kisha tusonge mbele. Hayana tija haya zaidi ya kutupotezea muda wa kufikiri kufanya mengine mazuri kwa maendeleo yetu kwani naona huu ni mtaji mwingine wa umaarufu. Kwani siasa hizi ndizo zilizotukosesha kununua mitambo ya dowans na leo tunaitegemea tukodishwe wakati tungeinunua wenyewe na kuwa mali yetu. Nimechoka na siasa uchwala za kutuongezea umaskini. Najua iko siku watanzania watatambua yapi ya kufuata na yapi ya kubeza na ndipo umaarufu kwa uzushi utakapoisha na kudharaulika kama waliopita.
Quote
 
 
0 #47 2011-07-13 01:08
Tatizo tuliowengi tunapenda mambo ya uzushi na ya kuchocheana halafu mwisho wa siku tunaoumia ni sisi tusiokuwa na maslahi na siasa. Hebu jiulize mwenyewe toka tumeanza kuathirika na uzushi ni watu gani wanaoumia kila siku kuanzia Arusha, Tarime mpaka Mwanza. Usidanganyike ndugu yangu hao wazushi wanapasipoti mkononi kukichafuka tu utawasikia wapo Uingereza, Ufaransa na kwingineko kuzuri, wewe utabakia kulowa damu na maisha magumu ukimbizini tena katika nchi zilizochoka. Mfano huyu Slaa kama kweli muungwana asingekubali kupokea Milioni saba kila mwezi za Wanachadema tena wengi wao wakiwa maskini wa kutupwa. Hana lolote huyo katumwa pesa na ndicho kinachomlazimis ha kila siku kutafuta uzushi na kuzunguka nchi nzima akikusanya posho za safari na kujilimbikizia mipesa. Kwa mshahara tu toka uchaguzi uishe amekusanya zaidi ya milioni hamsini, je wewe shabiki unazo? au unafurahia kulala na njaa wakati wenzio wanafurahia ushabiki wako. Tafakari chukua hatua.
Quote
 
 
0 #46 2011-07-11 13:31
Watanzania tuache kuwa na mtizamo finyu. Lazima jambo litizamwe kwa mapana yake! Uingerza wao wameuza rada kwa TZ, halafu waingereza hao hao, wakaona huruma kwamba nchi changa na maskini kama tz, wameuziwa rada kwa bei ya juu kuliko ilivyo - wakanusa mdudu rushwa. Wakaamua kutumia fedha za walipakodi wao na kufanya uchunguzi makini uliodhihirisha ukweli kwamba kulikuwa na rushwa, na kiasi kile cha mshiko wa juu kikaamriwa kirudishwe tanzania. Sasa tunashindwa vipi kukubali watanzania ndio waliokula hiyo rushwa? Inakuwaje vigumu kuelewa wote waliohusika kwenye mchakato mzima walipewa cha juu?? Na iweje sasa serikali iache kubeba jukumu lake na kusema wenye ushahidi wapeleke? Naona nisiendelee, manake si ajabu yakanitoka maneno mabaya
Quote
 
 
0 #45 2011-07-11 12:22
naaminI Dr Slaa ni docta wa ukweli mwenye sifa za kuwa rais wa jamuhuri ya muungano wa tanzania kwani sifa anazo, uwezo anao na sababu anazo hivyo namtakia maisha marefu na mungu ambariki
Quote
 
 
0 #44 2011-07-11 09:04
Nadhani [NENO BAYA] si kipimo cha uadilifu, jamaa anayejiita Basoul amekosa hekima na hafai kutoa maoni yake kwenye jukwaa hili. Huyu jamaa anafaa kuishi machungani na ng'ombe wenzie
Quote
 
 
-1 #43 2011-07-11 08:37
Quoting laiza:
Maajabu haya. Dokta Slaa amepeleka waraka unaomshauri Mwanasheria Mkuu wa serikali kuwa sheria za Tanzania zina weza kumshtaki Chenge, lakini hajapeleka ushahidi. Kinachotaiwa ni ushahidi ambao utaiwezesha jamhuri kushinda kesi na sio kumfurahisha dokta Slaa na wenzake kwa kumsimamisha Chenge Mahakamani halafu aje aishinde jamhuri na adai malipo lukuki.
Kwa hili niseme tu kuwa Dokta Slaa na mwandishi mmetaka umaarufu wa kisiasa na wa gazeti ili liuzike lakini hakuna hoja yenye mashiko mliyotuletea. Bado hatudanganyiki

Wewe laiza unafikiri kwa kutumia kiungo gani? wakati watanzania tunapambana na kero la mafisadi wanaosababisha maisha yawe magumu kiasi hiki wewe unabeza. Inaonekana na wewe fisadi jingine linaibukia.
Quote
 
 
-3 #42 2011-07-11 08:34
Jamani kama unaushahidi wewe unafungua kesi mahakamani kama raia una uhuru huo. Sasa hizi gilba za kuwasilisha maripoti kwa DPP ni politiki zisizo nz maslahi. Siku zote njia ya muongo ni fupi. Ndo maana porojo zote alizokuwa kitapika majukwaani wakati wa uchaguzi mkuu hakuzikumbuka kuziweka kwenye bajeti yao kuvulu. Hapo ndo mashaka yametanda kuwa kuna hila na mbinu za kungia ikulu na ukweli wa mambo ambao hata huyu Padiri muasi anafahamu. Kama Slaa alihasi kiapo cha upadiri urais ataweza? Alisema akiwa Rais atapunguza msharara wa rais kwa asilimia 20 lakini yeye hivi sasa anashinikiza CHAGA DEVELOPMENT MANIFESTO inamplipa mshahada mkubwa kuliko wa Rais. Jamani huu utapeli kweli hanadhani sisi wa Tanzania ni ma[NENO BAYA] kama wanachama wake wa Chadema wanaoongozwa kwa udikiteka ETI UKIMBISHIA mBWEA TU UNAINDIWA TUME. MADIWANI WA ARUSHA, CHACHA WANGWE, ZITO KABWE NA SASA SHIBUDA NI WAHANGA WA KWENDA KINYUME NA DEMOKRASIA YA KIFAMILIA YA MZEE EDWIN MTEI NA MUME WA BINTI YAKE FREEMANSON MBOWE
Quote
 
 
-2 #41 2011-07-11 08:26
Dr. Slaa anamdomo mkubwa Jamani duu amejitahidi kuukunja lakini bado umekaa kama Ngombr u e nyuma anakotole amkombora yake. Domo kavu kama ma ta ko ya Ngombe. Ikulu mzee ninndoto wadanganye hao hao wa kanda ya kaskazini.
Quote
 
 
0 #40 2011-07-11 08:24
SFO inawataja wahusika wote kwa upande wa Tanzania na kwamba miongoni mwao ni Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakati mkataba huo uliposainiwa - Ndivyo inavyosomeka sehemu ya ripoti tunayochangia. Hao wahusika wengine mbona hawatajwi. Wenye nasaba na akina Chenge wanaweza kupata wasiwasi wa kuwepo kwa dalili za ukabila. Tafadhali lifanyieni kazi hili maana nchi sasa ina mambo mengi mno. Tusishughulike suala la chenge afu tukazua makubwa
Quote
 
 
-4 #39 2011-07-11 08:22
SLAA KAMA KAWAIDA YAKE NIMUONGO NA SURA YAKE IMEKAA MKAO WA KUNYA. CHEKI DOMO LILIVYOJIKUNJA KWA UONGO. TUNATAKA USHAHIDI SIYO KUSEMA TUANZE KUPOTEZA PESA TENA KUCHUNGUZA. SLAA ALISEMA ANAUSHAHIDI ALETE HUO USHAHIDI. HUYU SLAA NI KUMBE HATARI SANA. NDO MAANA HATA KANISANI ALIKUWA KUDANGANYA WAUMINI NA KUTEMBEA NA WAKE ZAO. AMEJARIBU KUHUBIRI CHUKI NA KUWAANDAA VCIJANA KWA MAPAMBANO ILI KULINUFAISHA KUNDI LAO LA FREEMANSONS KUONA DAMU ZA WATANZANIA ZINATAPAKAA. LENGO ETI WAINGIE MADARAKANI. HATUNA MUDA NA CHAKUBANGA
Quote
 
 
0 #38 2011-07-11 06:17
Maajabu haya. Dokta Slaa amepeleka waraka unaomshauri Mwanasheria Mkuu wa serikali kuwa sheria za Tanzania zina weza kumshtaki Chenge, lakini hajapeleka ushahidi. Kinachotaiwa ni ushahidi ambao utaiwezesha jamhuri kushinda kesi na sio kumfurahisha dokta Slaa na wenzake kwa kumsimamisha Chenge Mahakamani halafu aje aishinde jamhuri na adai malipo lukuki.
Kwa hili niseme tu kuwa Dokta Slaa na mwandishi mmetaka umaarufu wa kisiasa na wa gazeti ili liuzike lakini hakuna hoja yenye mashiko mliyotuletea. Bado hatudanganyiki
Quote
 
 
0 #37 2011-07-10 14:40
Vita dhidi ya ufisadi ni mapambano hasa.Wakati serikali yetu haitaki mapambano haya, Chadema wanatafuta hata ushahidi. Ukweli utawekwa wazi. Chadema endelea na mapambano. Wananchi tunaona juhudi zenu.
Quote
 
 
+1 #36 2011-07-10 10:27
Quoting max:
Nashindwa kuwaelewa Mwandishi wa habari hii Godfrey Nyang'oro na Mhariri wake,iweje kichwa cha habari kinasema Dr. Slaa awasilisha ripoti kwa DPP ambapo habari yenyewe inasema Dr. yupo kwenye mchakato wa kupeleka waraka kwa DPP? Vinginevyo kichwa cha habari hii kilitakiwa kuwa Dr. Slaa Atawasilisha waraka kwa DPP Mwananchi kuweni makini kwenye uandishi wa habari nyeti kama hizi.

HATA MIMI KTK UJUMBE WANGU NAMBA 19 NIMEZUNGUMZIA KOSA LA MWANDISHI LKN NASHANGAA WATU WANANISHAMBULIA ! TUSIFANYE UWANJA WA MAONI KUWA KIJIWE CHA YANGA NA SIMBA. HAPA TUNAZUNGUMZIA MAMBO MUHIMU YA KUJENGA TAIFA. MWANDISHI AKIKOSEA LAZIMA TUSEME
Quote
 
 
+1 #35 2011-07-10 07:02
Nashindwa kuwaelewa Mwandishi wa habari hii Godfrey Nyang'oro na Mhariri wake,iweje kichwa cha habari kinasema Dr. Slaa awasilisha ripoti kwa DPP ambapo habari yenyewe inasema Dr. yupo kwenye mchakato wa kupeleka waraka kwa DPP? Vinginevyo kichwa cha habari hii kilitakiwa kuwa Dr. Slaa Atawasilisha waraka kwa DPP Mwananchi kuweni makini kwenye uandishi wa habari nyeti kama hizi.
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner