MwanzoContactsEmail
Home Habari Habari za Kitaifa Mahakama yafuta hati ya kumkamata Chenge
BOOKMARK THIS PAGE
Mahakama yafuta hati ya kumkamata Chenge  Send to a friend
Wednesday, 29 September 2010 09:08

Ummy Muya

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi wa Kinondoni imefuta hati yake ya kuruhusu kukamatwa kwa mwanasheria mkuu wa zamani, Andrew Chenge iliyotolewa juzi kutokana na mshtakiwa huyo kushindwa kutokea mahakamani.

Hakimu Sundi Fimbo alitoa hati hiyo juzi wakati Chenge, ambaye anatetea kiti chake cha ubunge wa Jimbo la Bariadi Mashariki akiwa kwenye mkutano wa kampeni ambako alipigiwa debe na mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete ambaye kwa sasa yuko mikoa ya Kanda ya Ziwa.

   Lakini mwendesha mashtaka wa mahakama hiyo, David Mwafwimbo aliiambia Mwananchi jana kuwa mdhamini wa Chenge aliibuka juzi akiwa amechelewa na akamuomba hakimu afute hati hiyo na ombi lake likakubaliwa.

"Mdhamini wake anayeitwa Masanja alimrudisha Hakimu Fimbo mahakamani ili kuomba kufutwa kwa kibali cha kumkamata mshtakiwa... ingawa mdhamini huyo alifika mahakamani hapo akiwa amechelewa, alienda kumuomba hakimu afute  hati hiyo na akakubaliwa" alisema Mwafwimbo.

Mwafwimbo alisema baada ya mdhamini huyo kufika, hakimu aliitisha tena jalada hilo na kuifuta amri hiyo ya kukamatwa kwa mshtakiwa huyo.

Chenge alitakiwa kuanza kujitetea jana katika kesi inayomkabili ya kuendesha gari kizembe na kufanya makosa mawili ya kusababisha vifo vya watu wawili na jingine la kuendesha gari bila bima halali.

 Chenge anadaiwa kugonga pikipiki ya maguruduma matatu, maarufu kama Bajaj iliyowabeba wasichana wawili na kusababisha vifo vyao ambavyo kisheria huchukuliwa kama makosa mawili tofauti.

Kutokuwepo kwake kulimfanya Hakimu Fimbo kuahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 5.
Lakini Zulfa Mfinanga na Herman Meza wanaripoti kutoka Shinyanga kuwa Jeshi la Polisi mkoani humo lilikuwa halijapokea hati ya kumkamata.

Afisa upelelezi mkoani humo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi((SSP),  Adam Nyakipande alikiri kusikia habari hiyo, lakini akasema walishindwa kuitekeleza kwa kuwa hawakupata kibali cha mahakama hiyo.

"Ninachoweza kusema ni kwamba sisi tunasubiri hati ya kumtia nguvuni... kwa ufupi bado hatujapewa kibali cha kumkamata lakini tukipata tutalifanyia kazi," alisema.


Add this page to your favorite Social Bookmarking websites
Reddit! Del.icio.us! Mixx! Free and Open Source Software News Google! Live! Facebook! StumbleUpon! TwitThis Joomla Free PHP
Last Updated on Wednesday, 29 September 2010 10:25
 

Comments 

 
+3 #23 2010-09-29 18:43
Chenge ni mzoefu wa kuvunja sheria. Kwanza ni mtuhumiwa kwenye ununuzi wa radar na vijisenti ameviweka huko majuu. Zamani akiwa mwanasheria mkuu alikuwa na sifa ya kubadilisha miswada baada ya kupitishwa na Bunge. Gari anaendesha bila bima usiku wa manane. Lakini huyu ndiye anasimamia maadili ya CCM. Na hayo ndiyo maadili ya CCM. Tumefika pabaya
Quote
 
 
-1 #22 2010-09-29 18:25
msitufanye sie [NENO BAYA] nyie waandishi mbona habari yenyewe haieleweki masanja huyo hana jina la pili? pia huyo masanja ni nanini? na kesi ya chenge mbona hamja eleza ni kwa nini amefikishwa hapo hebu muwe mna pambanua maelezo jamani yani mnakuwa kama hamjawai.
Quote
 
 
+3 #21 2010-09-29 17:22
si mna mchekea kikwete na ccm yake mtaona kweli mtanzania bado unakubali ahadi kem kem za juu hata nyumba ya kulala huna na unajichora mwili mzima ccccm du akili ni mali kila mtu ana zake poleni nchi ni ya kikwete na familia yake inayo tamba nchi nzima na watu wenye akili wanasalimu shikamooo baba ridhiwani,kweli ni raisi wa nchi anaamusha majozi ya watu kwa kumnadi mramba,chenge na luwasa kwa wenye akili acha ushabiki kweli inaingia akilini?Hata kwa ccm yenyewe usafi uko wapi hapo lakini mtaji wa ccm ni umbumbu wawatanzania kielimu masikini.
Quote
 
 
+5 #20 2010-09-29 14:41
KITENDO CHA KIKWETE KUWANADI LOWASA, MRAMBA, CHENGE, MIONGONI MWA MAFISADI WENGINE KINAASHIRIA NINI KWA WAPIGA KURA ZAIDI YA KUKIZIKA SIKU YA UCHAGUZI? KIKWETE MWENYEWE ANATUPA TASWIRA GANI YAKE MWENYEWE: handsome,in nice glasses, and ever smiling?

SIKU HIYO HATA WASIOONA HAWAHITAJI KUFUMBULIWA MACHO NDIPO WAIFANYIE KUFURU CCM!!!!!!!!!!!! !!!!!!
Quote
 
 
+5 #19 2010-09-29 14:39
Hati za kukamatwa ni kwa ajili ya vibaka tu sio kwa wazee kama hawa. Ingekuwa Chenge alikuwa kwenye Bajaji na wale marehemu kwenye gari lililowagonga wangeshaozea keko. Kesi zote za mahakamani ni kuwafool wananchi kwamba Serikali inafanya kazi wakati haifanyi chochote. Wote wenye kesi mahakamani jioni wanakunywa kahawa na JK pamoja na hao majaji, hapo unategemea nini? Zindukeni!!!!!
Quote
 
 
+3 #18 2010-09-29 14:32
....Huyo hakimu anataka kazi au kujeruhiwa.... na asirudie tena... au nae ni mwanasiasa tumjue... ole wake...
Quote
 
 
+5 #17 2010-09-29 14:24
TANZANIA INAYOSHUHUDIA HAKI INABATILISHWA, SHERIA INAKIUKWA, WANYONGE WANAONEWA, NA MAFISADI WANA-TRIUMPH OVER THE JUDICIARY- SIYO TANZANIA HURU. KAMA NI HURU BASI IMEUZWA KWA MAFISADI WALIOIBUKIA MIKONONI MWA KIKWETE.

NAFASI YA PEKEE KWA TAWZ KUREJESHA HAKI NA UADILIFU, UKOMBOZI HALISI WA MTANZANIA, KUREJESHA HADHI YA MAHAKAMA KWA KUCHUKUA HATUA MADHUBUTI KWA MAFISADI NI KUIPELEKA CHADEMA IKULU.

TUKIFANYA KOSA LA KUIRUDISHA CCM IKULU, TUTAKUWA WASHIRIKA WA MAFISADI KATIKA KULIANGAMIZA TAIFA LETU NA LAANA ITAKUWA JUU YETU.

LET'S SHOUT, "WE ARE THE LIBERATORS OF TANZANIA, AND WE SHALL LIBERATE IT BY VOTING IN DR. SLAA FOR PRESIDENT".
Quote
 
 
+4 #16 2010-09-29 13:58
Hakika,Siku ya mwisho ya kiama kila mmoja atahukumiwa kutokana na matendo yake.Uwe hakimu ambaye ulishindwa kutenda haki,machozi ya walioonewa yatakuwa hukumu yako,Uwe mshtakiwa uliyenunua haki hasira ya Mungu itakuwa juu yako.
Quote
 
 
+3 #15 2010-09-29 13:45
nadhan mahakama ipo ju ya serikali na vyombo vya habari ikiwemo hata mwananchi ni moja wapo wa vyombo vyenye kujenga na kubomoa wakati huo huo hi ni kwa ukosaji wao umakini katika kazi zao!!!!
Quote
 
 
+2 #14 2010-09-29 13:38
Kama hujui watu waliozivalia boot sheria za Tanzania na wanazikanyaga kanyaga kama watembea kwenye jamvi ndiyo kama hao kina Mh Chenge, je walimshitukiza kuhusu siku ya kuripoti mahakamani au alifahamu siku nyingi, jibu obvious alikuwa anafahamu isipokuwa ali[NENO BAYA]a.
Quote
 
 
+2 #13 2010-09-29 13:32
jamani kweli sheria zina wenyewe tena akina sisi kabwela
Quote
 
 
-2 #12 2010-09-29 12:52
MKUBWA NI MKUBWA TU.
Quote
 
 
+2 #11 2010-09-29 12:39

Uchakachuaji!
Uchunguzi unaendelea!
Upembuzi yakinifu!
Tathmini inafanyika!
kesi inaendelea!
Mkandarasi anatafutwa!

YOOOOTE Haya ni UCHAKACHUAJI NA BLAAAH BLAAAH za Mafisadi

Believe Me!

Justice Delayed is Justice Denied!!

WAO WANABEBANA sisi TUTAAMUA 31/10/2010
VIVA Dr Slaa
Quote
 
 
+2 #10 2010-09-29 12:18
Haya sasa serikali ya JK inafuata mkondo wa sheria kweli? Kisa kampeni mshitakiwa hafiki mahakamani? Mhhhhh haya wakubwa
Quote
 
 
+3 #9 2010-09-29 12:17
hicho ndio kilitufanya tuhame hiyo nchi tutarudi siku ccm ikipigwa na chini
Quote
 

Add comment

Tumia jukwaa ili kutoa maoni ambayo yatasaidia kulijenga taifa letu. Kumbuka, maoni yako yatapitiwa kwanza kabla hayajarushwa hewani!!!!!!


Banner
Banner
Banner