Watu 11 washikiliwa kwa kuiba kompyuta 12 za Chuo cha Utumishi
Muktasari:
Kamanda wa polisi mkoa Dhahiri Kidavashari amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake leo kuwa watuhumiwa hao walikamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema.
Mbeya. Polisi mkoani hapa inawashikiliwa watu 11 akiwamo mlinzi wa Kampuni ya New Imara, (majina yanahifadhiwa) kwa tuhuma za kula njama na kuiba kompyuta 12 mali za Chuo cha Utumishi wa Umma Tawi la Mbeya.
Kamanda wa polisi mkoa Dhahiri Kidavashari amewaambia waandishi wa habari ofisini kwake leo kuwa watuhumiwa hao walikamatwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema.
Kidavashari alisema kuwa kompyuta hizo zilikamatwa nyumbani kwa mwanamke (jina limehifadhiwa ) anayejihusisha na biashara ya pombe haramu aina ya gongo katika Kata ya Nonde jijini hapa.
Alisema kuwa mara baada polisi kupata taarifa waliweka mtego nyumbani kwa mwanamke huyo na ndipo walipofanikiwa kuwanasa na baada ya kupekuwa walifanikiwa kukuta vitu mbalimbali vya wizi zikiwemo kompyuta 11 za chuo cha utumishi wa umma ambapo moja ilikuwa imeuzwa kwa bei ya Sh 20,000