Kujeruhiwa kwa Kibanda kwaahirisha kesi

 Aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Theophil Makunga

Muktasari:

“Mheshimiwa Hakimu tunaomba  tarehe nyingine ya kusikiliza kesi hii kutokana na mshtakiwa namba mbili kuvamiwa na watu ambao hawajafahamika na kisha kujeruhiwa

KESI inayomkabili aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited, Theophil Makunga na wenzake wawili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi Machi 26, mwaka huu kutokana na mshtakiwa namba mbili, Absalom Kibanda (45), kutofika mahakamani baada ya kujeruhiwa na watu wasiojulikana.


Wakili wa Serikali, Peter Maugo  alidai mbele ya Hakimu Waliarwande  Lema   kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kuendelea kusikilizwa kwa upande wa ushahidi upande wa mashtaka.
“Mheshimiwa Hakimu tunaomba  tarehe nyingine ya kusikiliza kesi hii kutokana na mshtakiwa namba mbili kuvamiwa na watu ambao hawajafahamika na kisha kujeruhiwa ambapo kwa sasa amelazwa  katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.


Makunga anadaiwa kufanya kosa hilo kinyume na kifungu cha 32(1)(c) na 31(a) cha sheria  ya magazeti, sura ya 229 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.


Kaganda alidai  kuwa Novemba 30,2011 Makunga  akikaimu nafasi hiyo alichapisha  waraka wenye kichwa cha habari “Waraka maalumu kwa askari wote” ambao uliandikwa na Samson Mwigamba kwenye gazeti la Tanzania Daima toleo  la 2553.