Madereva 33 mbaroni wakidaiwa kulewa

Kamanda Sirro

Muktasari:

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema walifanya operesheni dhidi ya madereva na kuwabaini hao wamelewa huku wakiendesha magari jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Dar es Salaam. Madereva 33 wamekamatwa kwa tuhuma za kuendesha magari huku wakiwa wamelewa wakati wa sikukuu ya Mwaka Mpya.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro amesema walifanya operesheni dhidi ya madereva na kuwabaini hao wamelewa huku wakiendesha magari jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

Sirro amesema katika operesheni hiyo Kinondoni walikamatwa madereva 15, Temeke 10 na Ilala wanane.

“Sasa hivi tukimkamata dereva akiwa amelewa hatumuandikii faini ya kulipa tumeona wengi wao wanaona rahisi na kuendelea kurudia makosa, hivyo tunawapelea mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake,” amesema.