Mtalii afariki dunia akipanda mlima

Muktasari:

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbrod Mutafungwa amesema raia huyo aliyekuwa na hati ya kusafiria yenye namba 28890496  alipofika eneo la Simba Cane ndani ya hifadhi ya mlima huo  aliugua ghafla na kufariki dunia wakati akishushwa chini kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Moshi. Raia wa Norway, Johan Signmundstad (54) amefariki dunia wakati akipanda Mlima Kilimanjaro.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Wilbrod Mutafungwa amesema raia huyo aliyekuwa na hati ya kusafiria yenye namba 28890496  alipofika eneo la Simba Cane ndani ya hifadhi ya mlima huo  aliugua ghafla na kufariki dunia wakati akishushwa chini kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Hata hivyo, hakueleza ugonjwa uliosababisha kifo chake.

Mutafungwa alisema mwili wa mtalii huyo umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC kwa ajili ya uchunguzi wa kitabibu kabla ya taratibu nyingine kufanyika.