Meya Jacob azungumzia kilichotokea kati yake na Lema

MEYA WA UBUNGO AKANUSHA KUPIGANA NA LEMA

Muktasari:

Taarifa hizo zimeeleza kuwa Lema alikuwa anamtuhumu Mbunge wa Kibamba(Chadema), John Mnyika kuwasaliti na kuwa na mipango ya kuhamia CCM ndipo Jacob aliposimama na kumwambia Lema aache kumsingizia Mnyika mambo ya kipuuzi ndipo Lema alipomrushia ngumi meya huyo

Dar es Salaam. Meya wa Ubungo(Chadema), Boniface Jacob ameeleza kilichotokea kati yake na Mbunge wa Arusha Mjini(Chadema), Godbless Lema baada ya taarifa kusambaa kuwa wamepigana kwenye kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho.

Taarifa hizo zimeeleza kuwa Lema alikuwa anamtuhumu Mbunge wa Kibamba(Chadema), John Mnyika kuwasaliti na kuwa na mipango ya kuhamia CCM ndipo Jacob aliposimama na kumwambia Lema aache kumsingizia Mnyika mambo ya kipuuzi ndipo Lema alipomrushia ngumi meya huyo.