Mbarawa asema ujenzi reli ya kisasa Dar-Moro umefikia asilimia tisa

Muktasari:

Amesema hayo wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa reli hiyo kutoka Morogoro hadi Dodoma


Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa amesema ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro umefikia asilimia tisa, utakamilka baada ya miezi 30.

Akizungumza leo Machi 14, 2018 katika uzinduzi wa ujenzi wa reli ya kisasa kutoka Morogoro hadi Makutopora mkoani Dodoma, Mbarawa amesema ujenzi kutoka Dar es Salaam hadi Morogoro utakamilika Novemba 2019.

“Reli iliyopo sasa ya upana wa mita moja miundombinu yake imechoka sana treni huenda kwa kasi ya Kilometa 30 kwa saa. Rais (John Magufuli) ninaomba nikuhakikishie kuwa wizara ya ujenzi itaendelea kuwasimamia wakandarasi,” amesema.

“Tutahakikisha wakandarasi wanamaliza kazi ya ujenzi wa reli hii kwa wakati na kuhakikisha ubora. Hivi ninavyokuambia wakandarasi wanafanya kazi usiku na mchana kwa siku saba kwa wiki.”