Makunga ajiuzulu uenyekiti TEF

Muktasari:

Makamu wake, Deodatus Balile atakaimu nafasi hiyo hadi taratibu za kujaza nafasi hiyo zitakapokamilika


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga ametangaza kujiuzulu wadhifa wake kwa sababu binafsi.

Taarifa ya TEF iliyotolewa leo Machi 17, 2018 imesema: “Makunga amechukua hatua hiyo kwa kutumia uhuru wake binafsi kama mwanachama wa TEF.”

Imesema kutokana na uamuzi huo, mkutano mkuu wa dharura wa TEF uliokutana leo umeridhia kujizulu kwake huku ikieleza TEF itakosa uongozi na busara za Makunga ambazo zilikuwa bado zinahitajika kwa ajili ya ujenzi wa tasnia hii ya kitaaluma.

Kutokana na kujizulu, Makamu wake, Deodatus Balile atakaimu nafasi ya Makunga hadi taratibu za kujaza nafasi hiyo itakapokamilika.